KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Sunday, May 31, 2009

Sri Lanka yakataa uchunguzi wa kimataifa HAKUNA TAFAUTI YA MAUAJI YANAO SIBU NCHI ZETU ZA AFRICA. WEMA WETU SISI WAANGALIAJI NI NINI ?





Norway Interfering in the Internal Affairs of Sri Lanka - By K.T.Rajasingham - Norway is interfering in the internal affairs of Sri Lanka. Jon Westborg, the Ambassador of Norway in Sri Lanka, it is alleged that, he is behaving like a "Viceroy". ...... Liberation Tigers of Tamil Eelam (LTTE) has made it clear that, “LTTE does not operate with the concept of a ‘Separate State’. “We operate with a concept of ‘Homeland and self determination’. ‘Homeland’ does not mean a separate state as such.” This statement of the LTTE reminds us of the future coexistence with the Sinhalese in a united Sri Lanka. Therefore, it has become incumbent on the part of every peace loving Sri Lankan, to examine these allegations carefully and seriously





Kalyanapura, Gomarankadawala Massacre on 23 April 2006




There could be a significant amount of oil around Sri Lanka, perhaps 10-50 million barrels in the North / West of Sri Lanka as per the Norwegian seismic company estimates . It is likely that Norwegian companies have a better chance to get exploration permits from the LTTE than from the Government of Sri Lanka. For the time being the LTTE has no legal rights to grant such exploration permits. This fact could have been an incentive to help the LTTE with funds, technology, equipment and flying the LTTE leaders around Europe, portraying that the LTTE leaders as legitimate politicians and sole representatives of the Tamils. Below we have included some links to newspaper articles in English related to Norway and Oil business in Asia.




Sri Lanka imekataa kuruhusu mashirika ya kimataifa kufanya uchunguzi, au kuwashtaki wanajeshi wa nchi hiyo, kwa tuhuma za uki-ukaji wa haki za kibinaadamu, katika vita na wapiganaji wa Tamil Tigers.









Sri Lanka imekataa kuruhusu mashirika ya kimataifa kufanya uchunguzi, au kuwashtaki wanajeshi wa nchi hiyo, kwa tuhuma za uki-ukaji wa haki za kibinaadamu, katika vita na wapiganaji wa Tamil Tigers.
Waziri wa mashauri ya Nchi za Nje, Rohitha Bogollagama, alisema mahakama ya Sri Lanka, yana uwezo wa kushughulika na swala hilo.

Waziri huyo amesema kuwa Sri Lanka, ni nchi huru yenye mfumo wake wa sheria, na mahakama yake huru yatafanya uchunguzi kama kuna malalamiko yoyyote.

Bwana Rohitha Bogollagama, alizitoa maanani, shutuma kwamba mauaji ya kikabila yalitokea siku za mwisho za mapambano na wapiganaji wa kiTamil.

Ameelezea tuhuma za makundi ya kupigania haki za kibinaadamu kuwa ni uzushi, uliokusudiwa kulipa sifa mbaya jeshi la Sri lanka.

Mashirika ya haki za kibinaadamu, na maafisa wa Umoja wa Mataifa, wametoa wito kufanywe uchunguzi, kuhusu mauaji ya maelfu ya raia, katika mapambano hayo.

Serikali ya Sri Lanka, ilitangaza wiki mbili zilizopita, kuwa imewashinda wapiganaji; na Waziri wa Mashauri ya Nchi za Nje, amesema anataraji kuwa kumalizika kwa vita, kutasaidia kukuza uchumi wa nchi kwa asili-mia-tatu kila mwaka.

Tuesday, May 26, 2009

Mdororo wa Uchumi waivaa Afrika kusini



Waziri Trevor Manuel wa Afrika kusini
Uchumi wa Afrika kusini umekumbwa na mdororo kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1992, kufuatia kupungua kwa kasi ya uzalishaji viwandani halikadhalika sekta ya madini.
Uchumi wa nchi yenye Uchumi bora barani Africa imerekodi upungufu wa kiwango cha hadi asili mia 6.4% kati ya mwezi Januari na March, ikilinganishwa na kipindi kama hiki mwaka jana.

Hiki ndio kiwango kikubwa cha upungufu tangu mwaka 1984 kikifuatiwa na mdororo wa asili mia 1.8% kila mwaka katika kipindi cha miezi mitatu iliyopita.

Sekta ya ujenzi hata hivyo imeimarika kutokana na mashindano ya mpira ya Kombe la Dunia yanayopangwa kufanyika huko.

Afrika kusini imenufaika chini ya mpango kabambe wa serikali wa uwekezaji katika mipango ya mashindano ya mpira ya mwaka 2010.

Takwimu zilizofanywa na kampuni huru 'Statistics South Africa, imebaini kupungua kwa uzalishaji viwandani pamoja na uwindaji wanyama pori vimechangia mno mdororo huo.

Makampuni ya kuchimba migodi yameathiriwa na mdororo wa uchumi duniani

Tanzania imekuwa ikiendelea kutafuta ufumbuzi wa tatizo la mauaji ya albino














Tanzania imekuwa ikiendelea kutafuta ufumbuzi wa tatizo la mauaji ya albino, ambalo limesababisha mauaji ya watu wasiopungua 45 kwa kipindi cha miaka miwili iliyopita.
Vitendo vya mauaji ya albino vimeenea zaidi katika maeneo ya kanda ya Ziwa Victoria. Uovu huo umejikita katika mikoa ya Mwanza, Mara, Shinyanga na Kagera.


Bonyeza hapa kumfuatilia Vicky Ntetema katika blogu yake

Maeneo hayo ya historia ya kisirani cha kuwaua vikongwe katika miaka ya 1970, hasa kutokana na macho yao mekundu.

Mapema mwaka 2008, mwandishi Vicky Ntetema wa BBC alianza uchunguzi kudadisi kiini cha mauaji ya albino katika maeneo hayo ya Ziwa Victoria.

Ilikuwa safari ndefu, nyeti, yenye utelezi na hatari huku ikihitaji subira na ujasiri. Siku baada ya siku, Vicky alikutana na wahusika mbalimbali katika biashara hiyo ya kiza.

Kwa taarifa za kina, ukitaka kujua wanaohusika na mauaji ya albino, basi soma blogu ya Vicky Ntetema. Unapewa fursa ya kuchangia mada kwa kutoa maoni.

Nyerere na Amin walipokutana



Nyerere na Amin walipokutana

Watoto wa Nyerere na Amin walipokutana kwa mara ya kwanza, tangu kumalizika vita....








Ilikuwa ni siku ya Alhamisi, tarehe tisa Aprili 2009, wakati historia ya Afrika Mashariki ilipoandikwa upya. Mtoto wa kiume wa Idi Amin aliyekuwa rais wa Uganda na mwingine wa rais wa kwanza wa Tanzania, Julius Nyerere walikutana kwa mara ya kwanza miaka 30 tangu nchi hizo zilipopigana vita.

Angalia picha za Butiama

Kwa mtizamo wa Jaffar Amin, familia hizo mbili zilitakiwa kuwa zimeshakutana kwasababu “wao ndiyo walikuwa vinara”. Ilichukua muda mrefu kumshawishi Madaraka Nyerere, lakini hatimaye alikubaliana na wazo “kwasababu baba zetu sasa walishafariki.”

Taarifa kwa vyombo vya habari kutoka kitengo cha mahusiano ya umma cha BBC ikitangaza mpango wa kuwakutanisha Madaraka Nyerere, 47, na Jaffar Amin, 42, ilipokelewa kwa hisia tofauti.

Baadhi walimaka: “Huu upuuzi! Haiwezekani na wasiruhusiwe kukutana.” Wengine walikuwa na mtizamo tofauti wakaimwagia BBC sifa kwa kubuni wazo la kuwakutanisha.

Mipango ya kuwakutanisha wana hao wawili ilianza katikati ya mwaka 2008, wakati kikosi cha Idhaa ya Kiswahili ya BBC kilipozuru Arua, kaskazini magharibi mwa Uganda na kufanya mahojiano marefu na Jaffar.


Madaraka na mgeni wake Jaffar walishiriki matangazo ya BBC baada ya kukutana Butiama, Aprili 9, 2009.



“Tumekuwa tukitengwa kisiasa”, Jaffar alisema huku akimwelezea baba yake kwa fahari, ambaye alibebeshwa majina yote mabaya: muuaji, mla watu, mpenda wanawake na mbaguzi wa rangi - kwa kuwafukuza raia wenye asili ya Asia kutoka Uganda mwaka 1974. Orodha ya maovu yanayodaiwa kufanywa na baba yake ni ndefu isiyo na mwisho.

Utawala wake ulisambaratishwa na Rais Nyerere ilipofika April 1979 wakati wanajeshi wa Tanzania walipoingia mji mkuu Kampala kwa kishindo, Idi Amin pamoja na familia yake walikimbilia uhamishoni, kwanza Libya na baadaye Saudi Arabia ambako alifariki dunia mwaka 2003.

Changamoto
Baada ya kufanikiwa kupata ridhaa ya Jaffar na Madaraka, changamoto nyingine ilikuwa kutafuta mahali pa kufanyia mkutano wao huo mkubwa, kulikuwa na wazo la kufanyia katikati - isiwe Butiama wala Arua.

Lakini Jaffar alisisitiza kuwa yuko tayari kusafiri kwenda Butiama kutoa heshima kwa to mtu ambaye alimng’oa baba yake madarakani na kukimbilia uhamishoni. Madaraka alikubali mara moja kuwa mwenyeji. Kwa baadhi ya wasikilizaji wetu hili halikuwa jambo walilolikubali kwa urahisi.

Safari ya Jaffar kwenda Tanzania ilianza Jumatatu, tarehe 6 mwezi Aprili, kutoka nyumbani kwake Arua akielekea mji mkuu Kampala kabla ya kuvuka mpaka na kuingia ardhi ya Tanzania.


Angalia picha za Butiama

Huku Jaffar akifanya safari yake katika njia walikopita wanajeshi wa Tanzania wakati wa vita, Madaraka Nyerere alikuwa akifanya maandalizi ya mwisho kumpokea mgeni maalum kutoka Uganda.

Mchana wa Alhamisi, tarehe tisa, gari aina ya Toyota Prado iliyokuwa imembeba Jaffa iliingia katika lango la makazi ya hayati Mwalimu Julius Nyerere. Akiwa katika vazi la kiafrika, alitoka nje ya gari huku akitabasamu.

Mwenyeji wake, pia katika vazi la kiafrika, hakuficha shauku yake. Wawili hao walikumbatiana na kucheka kabla ya kuingia kwenye jengo lenye kaburi la Mwalimu Nyerere aliyefariki mwaka 1999.

Akiwa mbele ya kaburi la hayati Nyerere, Jaffar ambaye ni mswalihina alisoma dua zake. “Nimekuja hapa kwa amani,” alisema kabla ya kuweka shada la maua.

Mazungumzo
Ilikuwa wazi kuwa wana hao wawili wa kiume walikuwa na mtizamo sawa na haikushangaza watu waliokuwepo, pale walipoomba kufanya mazungumzo ya faragha. Yaliyozungumzwa bado ni siri kati yao wawili.

Umati ulilipuka kwa nderemo, ngoma za jadi za kabila la wazanaki zilirindima wakati wana hao waliposhika vinasa sauti kuanza kuzungumza.

“Imepita miaka 30 ambayo katika familia zetu hakuna aliyefikiria wazo la kukutana,” Jaffar alisema, “Madaraka na mimi tulifanya uamuzi mgumu lakini wa kihistoria. Tusingependa kuwa upande mbaya wa historia.”

Katika machache aliyozungumza kumkaribisha mgeni wake, Madaraka alimwelezea baba yake kuwa ni mpenda amani. “Hata baada ya vita, angekubali kukutana na Idi Amin na hata kumwalika Butiama.”

“Tofauti zozote walizokuwa nazo kabla, tunachoweza kufanya sasa ni kujifunza na yaliyotokea na kuanza ukurasa mpya.”

Uhasama
Siasa za Afrika Mashariki kunako miaka ya 1970, zilitawaliwa na uhusiano mbaya kati ya Nyerere wa Tanzania – msomi na mpigania ujamaa na Amini wa Uganda ambaye hakuwa na elimu kubwa na mtoto wa mkulima aliyeinukia kutoka jeshini kabla ya kufanya mapinduzi ya kijeshi na kunyakua madaraka.

Katika matukio tofauti, wawili hao waliwahi kurushiana maneno. Nyerere wa Tanzania alimwita Idi Amini mpuuzi, mdhalimu na kibaraka wa nchi za Magharibi, wakati Amin alimwita mwenzake wa Tanzania mwoga.


Jaffar alifika kutoa heshima kwenye kaburi la hayati Mwalimu Nyerere.



Jitihada za kumng’oa Amin zilipamba moto wakati majeshi ya Uganda yalipovamia na mkoa wa Kagera, ulioko kaskazini magharibi mwa Tanzania mwezi Oktoba 1978.

Wanajeshi wa Tanzania waliingia Uganda, si tu kuwatimua wavamizi, lakini kwenda mpaka Kampala kumng’oa Idi Amin.

Takriban watu milioni moja waliuawa na uchumi wa mataifa hayo mawili kuathirika kwa kiasi kikubwa.

Nani angedhani miaka 30 baadaye, wana wa kiume wa Amin na Nyerere wangeweza kuweka kando tofauti za baba zao? Kama alivyosema mzungumzaji mmoja katika mkutano huo wa Aprili tisa 2009, historia imeajiandika upya, kwa hisani ya BBC.

Misitu yaangamia kwa kasi kubwa Afrika



Misitu yaangamia kwa kasi kubwa Afrika

Ripoti iliyotolewa inaonesha misitu barani Afrika inatoweka kwa kasi kuliko ilivyo sehemu nyingine za dunia kutokana na kukosekana kutokuwepo umiliki wa aradhi unaotambulika.


























Ripoti iliyotolewa inaeleza misitu ya Afrika inaangamia kwa kasi kubwa tofauti na maeneo mengine duniani kutokana na kukosekana mikakati ya kumiliki ardhi.
Kwa mujibu wa ripoti ya Shirika la Haki na Mali chini ya asilimia mbili ya misitu ya Afrika ipo chini ya umiliki wa jamii, ikilinganishwa na nchi za Amerika Kusini na Asia.

Kiwango cha ukataji miti Afrika ni kikubwa mara nne zaidi ya wastani wa ukataji isitu katika sehemu nyingine za duniani.

Kwa kiwango cha sasa, itachukua miaka 260 kwa nchi za Bonde la mto Congo kufikia hatua ya mageuzi iliyopatikana katika misitu ya Amazon.

Hatua ya kumilikisha ardhi inaweza kusidia kuinusuru misitu, kupunguza athari za mabadiliko ya hali ya hewa na pia itasaidia kuondoa umasikini, kwa mujibu wa ripoti iliyopewa jina Ukaguzi wa Umilikaji wa Misitu ya nchi za Joto, Hali ilivyo, Changamoto na mikakati.

Taarifa ya uchunguzi huo ilitolewa mjini Yaunde Cameroon, katika mkutano wa wawakilishi wa jamii zinazoishi katika maeneo ya misitu katika Afrika, Amerika Kusini na Asia.









Ripoti iliyotolewa inaeleza misitu ya Afrika inaangamia kwa kasi kubwa tofauti na maeneo mengine duniani kutokana na kukosekana mikakati ya kumiliki ardhi.
Kwa mujibu wa ripoti ya Shirika la Haki na Mali chini ya asilimia mbili ya misitu ya Afrika ipo chini ya umiliki wa jamii, ikilinganishwa na nchi za Amerika Kusini na Asia.

Kiwango cha ukataji miti Afrika ni kikubwa mara nne zaidi ya wastani wa ukataji isitu katika sehemu nyingine za duniani.

Kwa kiwango cha sasa, itachukua miaka 260 kwa nchi za Bonde la mto Congo kufikia hatua ya mageuzi iliyopatikana katika misitu ya Amazon.

Hatua ya kumilikisha ardhi inaweza kusidia kuinusuru misitu, kupunguza athari za mabadiliko ya hali ya hewa na pia itasaidia kuondoa umasikini, kwa mujibu wa ripoti iliyopewa jina Ukaguzi wa Umilikaji wa Misitu ya nchi za Joto, Hali ilivyo, Changamoto na mikakati.

Taarifa ya uchunguzi huo ilitolewa mjini Yaunde Cameroon, katika mkutano wa wawakilishi wa jamii zinazoishi katika maeneo ya misitu katika Afrika, Amerika Kusini na Asia.

Al-Shabaab wakiri kufanya shambulio

Al-Shabaab wakiri kufanya shambulio

Kundi la wanamgambo wa Kiislamu la Al- Shabaab nchini Somalia limedai lilihusika na mashambulio ya mabomu ya kujitoa muhanga yaliyotokea katika mji mkuu Mogadishu.





























Wapiganaji wa Al Shabaab wamedai kuhusika na mashambulio
Kundi la wanamgambo wa Kiislamu nchini Somalia , Al- Shabaab , linaloaminika kuwa na ushirikiano na kundi la kigaidi la Al- Qaeda limedai kuhusika na mashambulio ya mabomu ya kujitoa muhanga mjini Mogadishu.
Kiongozi wa kisiasa wa kundi hilo Shaykh Husayn Ali Fiidow amesema walimtumia mvulana mmoja mdogo kufanya shambulio hilo ambalo liliwauwa wanajeshi sita na raia mmoja.

Mlipuaji huyo aliendesha gari aina ya Pick-up hadi kwenye chuo cha kutoa mafunzo kwa maafisa wa Polisi.

Ongezeko la mapigano mjini Mogadishu katika muda wa majuma mawili yaliyopita yamelazimisha karibu watu 60,000 kuutoroka mji huo.

Takriban watu mia mbili wanadhaniwa wameuwawa tangu mwanzoni mwa mwezi Mei , huku wanamgambo wa Kiislamu wakijaribu kuiangusha serikali ya mpito.

Wanataka kulazimisha kuzingatiwa kwa sheria kali za Kiislamu katika utawala na wanataka kikosi cha kulinda amani cha umoja wa Afrika kiondoke Somalia.

Mara ya mwisho shambulio la bomu la kujitoa muhanga kutokea mjini Mogadishu ilikuwa mwezi wa Februari kwenye kituo cha kikosi cha AU, ambapo wanajeshi 11 kutoka Burundi waliuwawa.

Wanajeshi 4,300 wa AU hawahusiki kwenye mapigano hayo kwa kuwa hawana idhini ya kuwashambulia wanamgambo.

Rais mwenye msimamo wa wastani kuhusu Uislamu Sheikh Sharif Sheikh Ahmed alichaguliwa na serikali ya mseto mwezi Januari chini ya mpango wa amani ulioungwa mkono na umoja wa mataifa.

Lakini hata baada ya kiongozi huyo kuanzisha utawala wa Sharia katika nchi hiyo yenye waislamu wengi , hatua hiyo haijawaridhisha wanamgambo wa kiislamu.
Al-Shabaab wakiri kufanya shambulio

Kundi la wanamgambo wa Kiislamu la Al- Shabaab nchini Somalia limedai lilihusika na mashambulio ya mabomu ya kujitoa muhanga yaliyotokea katika mji mkuu Mogadishu.

UN yalaani hatua ya Korea Kaskazini

UN yalaani hatua ya Korea Kaskazini

Baada ya kufanya mkutano wa dharura, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limeshutumu vikali hatua ya Korea Kaskazini ya kufanya jaribio la silaha za nyuklia.


































Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa baada ya kukutana kwa dharura, hatimaye limeshutumu vikali hatua ya Korea Kaskazini kufanya jaribio la kinyuklia.
Baraza hilo lilikutana kwa dharura saa chache tu baada ya jaribio hilo kufanywa na limeonya hatua kali zitachukuliwa dhidi ya Korea Kaskazini.

Kauli ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa imetolewa muda mfupi tu baada ya serikali ya Korea Kaskazini kutangaza imefanya jaribio lililofanikiwa la Kombora la nyuklia lililo kubwa zaidi ya lile iliyolipua mnamo mwaka wa 2006.

Mataifa wanachama sasa wanataka hatua kali zichukuliwe dhidi ya Korea Kaskazini ambayo tayari iko chini ya vikwazo vya baraza hilo la usalama la Umoja wa Mataifa. Lakini serikali ya Korea Kaskazini imepuuza kauli hiyo na kusema iko tayari kukabiliana vilivyo na wapinzani wake wote.

Wataalamu wa makombora wa Urusi wanasema kombora lililolipuliwa lina uwezo sawa na yale yaliyoangushwa na Marekani katika miji ya Hiroshima na Nagasaki nchini Japan wakati wa vita vya pili vya dunia.

Hata China ambayo imekuwa ikiunga mkono Korea Kaskazini chinichini sasa imesema itakubaliana na azimio lolote la Baraza la Usalama wa Umoja wa Mataifa.

Ili kuelewa wasiwasi huu ambao umekumba jamii ya kimataifa ni muhimu kuelewa uwezo wa zana za Kinyuklia.

Kulingana na shirika moja la utaalamu wa kivita la Marekani, Center for Defense Information, makombora matano au sita ya aina iliyofanyiwa majaribio siku ya Jumatatu, yakilipuliwa mara moja yana uwezo wa kuharibifu duniani kote na kuwaacha manusura wachache sana.

Ikiwa na silaha kama hizi, si ajabu Korea kaskazini sasa imeionya Marekani itakabiliana nayo kivita iwapo serikali ya Rais Obama itajaribu kuishambulia

Sunday, May 24, 2009

Afrika day














Kesho ni siku maalum ya bala afrika! ni siku ya kusherehekea kwa baadhi ya watu kwakuwa kuna nchi nyingine zenye matatizo ya kila aina mojawapo ni vita kama vile kongo,somalia,sudani, uganda, na magonjwa kama vile maleria, ukimwi na umasikini wa khali ya juu. Pia swala la elimu bado ni la chini sana. Tunawatakia sherehe njema! Mungu ibariki Afrika! Mungu ibariki Tanzania! Aluta Kontinua!

Pakistan yadai Taliban wanazidiwa






















Forcing America into the 1991 Gulf War, the Afghanistan War, and now the Iraq War to
reconfigure the Middle East and establish a war-profiteering nightmare, resulting in 4,000 American soldiers being killed along with an uncounted number of Afghani and Iraqi civilians














Jeshi la Pakistan linasema kuwa limefanikiwa kuyadhibiti tena maeneo kadhaa ya Mingora, mji mkuu katika bonde la Swat, wakati mashambulio dhidi ya wanamgambo wa Taliban yakiendelea.
Afisa mmoja wa usalama amesema wanajeshi sasa wanafanya kazi ya kutegue mabomu ya ardhini katika maeneo yaliyo chini ya udhibiti wa serikali.

Lakini mapigano bado yanaendelea huku wanajeshi na wanamgambo wakiwa katika makabiliano ya uso kwa uso kwenye baadhi ya njia panda kuu za mji huo, kwa mujibu wa taarifa za jeshi.

Haja ya ushindi
Mapigano yalianza baada ya amani kuvurugika mapema mwezi huu. Mamia ya watu wameuawa na wengine zaidi ya milioni moja wamekimbia makazi yao katika eneo la Swat tangu kuanza kwa mapambano ya kuwasaka wanamgambo wa Taliban.

Mafanikio ya jeshi la Pakistan yanategemea ushindi wa kutosha katika eneo la Mingora, kwa mujibu wa mwandishi wa BBC aliyeko Islamabad.

Mashambulio hayo mapya dhidi ya Taliban yanaungwa mkono kikamilifu na Marekani, ambayo imebainisha kuwa Pakistan na Afghanistan ndiyo maficho makuu ya mapambano ya ugaidi wa kimataifa.

Aliyekuwa Rais wa Korea Kusini ajiua



Raia wa Korea Kusini wameonyesha kushtushwa sana na kifo cha ghafla cha rais wao wa zamani Roh Moo-hyun, aliyejiua baada ya kusakamwa kwa tuhuma za rushwa.




























Raia wa Korea Kusini wameonyesha kushtushwa sana na kifo cha ghafla cha rais wao wa zamani Roh Moo-hyun, aliyejiua baada ya kusakamwa kwa tuhuma za rushwa.
Bwana Roh, aliyekuwa na umri wa miaka 62, alikufa baada ya kuanguka kutoka mlimani karibu na nyumba yake. Msemaji wake amesema aliacha waraka mfupi unaoelezea anajiua.

Rais Lee Myung-bak amesema anashindwa kuamini taarifa za kifo hicho na ni masikitiko makubwa. Mwezi uliopita Bwana Roh aliomba radhi kutokana na tuhuma za familia yake ilichukua rushwa ya dola milioni 6 wakati alipokuwa madarakani baina ya mwaka 2003-2008, lakini kamwe hakukiri kufanya jambo lolote kinyume na sheria.

Kiongozi huyo wa zamani ametokea katika familia isiyo na makuu, lakini alipanda ngazi hadi nafasi ya urais kutokana na usafi uliooneshwa na serikali na maridhiano yaliyofanywa na Korea Kaskazini.

Mwili wa Bwana Roh ulichukuliwa kwa msafara kutoka hospitalini katika mji wa kusini wa Busan siku ya Jumamosi mchana hadi katika mji alikozaliwa wa Gimhae, ambapo wasaidizi wake wamesema ndipo atakapozikwa.

Mamia ya askari polisi wakiwa katika sare zao pamoja na waombolezaji wengine walijipanga barabarani wakati mwili wake ulipokuwa ukisafirishwa.

11 wafariki katika tamasha Morocco






Watu wasiopungua 11 inaarifiwa wamefariki katika mji mkuu wa Rabat nchini Morocco na wengine 40 kujeruhiwa baada ya kukanyagana katika tamasha ya muziki ya Mawazine.









Watu wasiopungua 11 wamefariki katika mji mkuu wa Morocco, Rabat, baada ya kukanyagana katika tamasha ya kimataifa ya muziki ya Mawazine.
Kulingana na waandishi habari, inadhaniwa kwamba watu wengine 40 walijeruhiwa baada ya uzio wa senyenge kuporomoka.

Tukio hilo lilifanyika usiku wa Jumamosi, wakati zaidi ya watu 70,000 walijaa pomoni katika uwanja wa michezo wa Hay Nahda, kumtizama mwanamuziki wa Morocco, Abdelaziz Stati.

Katika tamasha mwaka huu walioshiriki ni pamoja na Kylie Minogue, Khaled na Alicia Keyes.

Wadadisi wanasema kwamba tamasha hiyo ya wiki moja ya Mawazine ni kati ya mipango ya Morocco ya kuimarisha sifa nzuri za nchi hiyo ili taifa hilo lionekana ulimwenguni kwamba linakwenda sambamba na maendeleo ya kisasa.

Kulingana na maafisa wa polisi, wanawake watano, wanaume wanne, na watoto wawili, ndio waliofariki kati hali hiyo ya mkanyagano.

Friday, May 22, 2009

Mheshimiwa Raisi na jitihada za maendeleo ya nchi yetu

Hizi ni baadhi ya harakati mbalimbali za Raisi wetu akiwa nje ya nchi yetu katika kututafutia maendeleo ya sekta mbalimbali za kijamii. Akiwa kama mpatanishi(katika migogoro kama Kenya, Komoro,rwanda na burundi, kongo darfur...nk) hili ni jambo la pongezi sana, raisi wa umoja wa afrika(mstaafu) ameweza kutuletea mabadiliko makubwa katika kuhakikisha nasi tunapata exposure kwa watu na taasisi mbalimbali za nje ya mipaka yetu. Na hivi karibuni alikuwa nchini Marekani akikutana na wataalamu wa maswala ya habari na teknolojia za kompyuta na kuwashawishi kuja kuwekeza katika nchi yetu, hili ni jambo la msingi tukizingatia ya kwamba maendeleo haya ni muhimu kwa kipindi hiki cha sasa cha sayansi na teknolojia! pia ameweza kwenda mashariki ya kati na asia ili kuweka mahusiano muhimu kwa maendeleo ya sekta mbalimbali.









































































Maendeleo haya ni kwetu sote kwani kwa kuwezeshwa kiteknolojia sote tutaweza pata huduma muhimu za mawasiliano kwa uhakika na ufanisi zaidi, na pia khali hii itatoa fursa za kazi kwa watanzania mbalimbali watakaokuwa waajiriwa wa miradi mbalimbali itakayoletwa na wawekezaji kutoka nje. Kwa haya tunampongeza sana raisi wetu na kumtakia kila la kheri katika harkati zake za kutuletea maendeleo katika nyanja mbalimbali za kimaisha!
Hongera Mheshimiwa raisi wetu na Mungu akujalie Kheri na Baraka Tele!Mungu ibariki Tanzania! Mungu ibariki Africa!