KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Friday, April 29, 2011

Harusi ya kifalme Uingereza



Mwanamfalme wa Uingereza, William na mkewe Kate Middleton wameonekana hadharani kwa mara ya kwanza wakiwa kama wanandoa wapya. Baada ya kuhitimisha ibada ya misa katika Kanisa la Westminster Abbey mbele ya karibu wageni waalikwa 2,000 na watu wengine bilioni mbili waliokuwa wakiangalia harusi hiyo ya kifalme kwa njia ya televisheni, William na Kate pia walipigana busu la kwanza hadharani kama mume na mke, wakiwa kwenye kibaraza cha kasri la malkia la Buckingham.


Kabla ya harusi hiyo mapema leo, Malkia Elizabeth wa Pili, alimpa William cheo cha heshima cha kuwa mtawala wa jimbo la Cambridge. Baada ya harusi, Kate amekuwa rasmi mke wa mtawala wa jimbo la Cambridge. Wanandoa hao walijumuika pamoja na wageni 650 kwa chakula cha mchana na sasa wanasubiri sherehe itakayofanyika usiku ambayo itahudhuriwa na marafiki 300 na wanafamilia




Prince William has to ask Queen Elizabeth for her permission before proposing Kate








Prince William and Kate Middleton announced their engagement on Tuesday Nov. 16, 2010. The wedding date has not been announced yet, but it is expected to take place in the spring or summer of 2011. Prince William’s marriage brings a big cheer to the whole Britain in amid economic woes. The royal wedding will be held on the 30-year anniversary of his parents’ wedding. Below are five wedding traditions in British royal nuptials which will surely become hot topic for upcoming newspaper presses.



Asking the Queen\'s permission

It is the tradition that Prince William has to ask Queen Elizabeth for her permission before proposing Kate. The Royal Marriages Act of 1772 requires all descendants to access the sovereign ruler’s approval for the marriage. The British law prohibits royals from marrying Catholics. Hence, if Kate Middleton were Catholic, William would have to choose either the throne or his love










With Diana\'s ring, William and Kate are engaged







Royal rings are made with a piece of Welsh gold.










Diana\'s impressive wedding dress






Residence



There will be an apartment available for them in the royal residence. However, after the nuptial, William and Kate will return to their home in Wales near William\'s Royal Air Force base. An unusual fact is that William and Kate have lived together long before their marriage ceremony. Whenever William\'s service is over, William and Kate will move to a house in Herefordshire.






Royal wedding between Queen Elizabeth and Prince Phillip in 1947






The wedding location

The wedding location of Kate Middleton and Prince William has not been announced yet. Westmister Abbey is most likely the traditional place. Otherwise, St. Paul’s in London where Prince Charles married Princess Diana and St. Georges Chapel in Windsor would be another choice.

















Mahakama yampunguzia Mbatia ada ya kesi yake






MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imempunguzia Mwenyekiti wa Chama Cha NCCR-Mageuzi, James Mbatia na wanachama wawili wa chama hicho, ada ya kuendesha kesi yake dhidi ya Mbunge wa Jimbo la Kawe, Halima Mdee.

Katika kesi hiyo, Mbatia ambaye alikuwa mgombea wa kiti hicho, uchaguzi mkuu mwaka jana, alifungua kesi kupinga ushindi wa Mdee.Sheri ya Uchaguzi inamtaka mlalamikaji kuweka mahakamani dhamana ya Sh5 milioni kwa kila mlalamikiwa.

Kwa msingi huo, Mbatia kupitia kwa wakili wake, Mohamed Tibanyendela, aliwasilisha maombi mahakamani hapo akiomba mahakama kumpangia kiwango cha chini itakachoona kinafaa.

Hata hivyo, sheria hiyo pia inatoa nafasi kwa mlalamikaji kuomba kusamehewa au kupangiwa kiwango cha chini zaidi ya hicho kilichotajwa kwa kadri mahakama itakavyoona kulingana na mazingira ya kesi husika.

Lakini, Mbatia aliwasilisha maombi mahakamani hapo kupitia kwa wakili wake, Tibanyendela akiiomba mahakama kumpunguzia kiasi hicho, badala yake alipe Sh1 milioni kwa kila mlalamikiwa.

Katika maombi hayo, licha ya mambo mengine, Mbatia alidai hivi sasa hana uwezo wa kulipa kiasi hicho kwa sababu ametoka kwenye kampeni za uchaguzi huo.

Wanachama wengine wa chama hicho ambao waliomba kuunganishwa na Mbatia kwenye kesi hiyo, Hemed Kanoni na Solomon Lufunda, waliomba mahakama kuwasamehe kulipa kiasi chochote cha dhamana kwa madai kuwa, hawana uwezo huo kwa sababu ni wakulima.

Akitoa uamuzi huo jana, Jaji John Utamwa, alitupilia mbali maombi ya Mbatia kutaka alipe Sh1 milioni kwa kila mlalamikiwa, na walalamikaji wenzao kutokulipa kabisa kwa sababu zao hazina msingi.Jaji Utamwa aliwapunguzia kiwango hicho na kuwataka kulipa Sh3 milioni kwa kila mlalamikiwa wote kwa pamoja.

Kwa uamuzi huo, Mbatia na wenzake wanapaswa kulipa Sh9 milioni kama dhamana ya kesi yao, badala ya Sh15 milioni, ndani ya siku kumi 14 tangu kutolewa kwa uamuzi huo ili kesi iweze kupangiwa siku ya kusikiliza.

Katika kesi hiyo, Mbatia anapinga ushindi wa Mdee, anachodai kuwa Mdee wakati wa kampeni alitoa tuhuma za uongo kwamba Mbatia alikuwa akipewa Sh80 milioni na CCM, mambo ambayo anadai yalimwathiri katika upigaji kura





Burundi kuadhimisha mauaji ya Wahutu




Raia wa Burundi
Nchini Burundi leo April 29 ni kumbukumbu ya mauaji ya maelfu ya raia wa kabila la wahutu waliouliwa na jeshi mwaka 1972.

Mauaji hayo yalifunikwa funikwa na tawala zilizopishana na hivi sasa baada ya mageuzi ya kidemokrasia shirika moja linakutetea haki za jamii limetaka yaliotendeka yote yawekwe wazi na haki itendeke.

Hata hivyo baadhi ya raia wa nchi hiyo wanaunga mkono juhudi za serikali ya kutenga siku ya kumbukumbu ya maujai hayo ili kuna wale wanaopinga wakisema, huenda ikasababisha uhasama kati ya jamii mbali mbali nchini humo








Mchango kwa Ukarabati wa Chernobyl




Rais Viktor Yanukovych wa Ukraine (kushoto) na Rais wa Halmashauri ya Umoja wa Ulaya Jose Manuel Barroso.Leo mkutano maalum umefunguliwa Kiev mji mkuu wa Ukraine, ukiwa na azma ya kuchanga fedha za kusaidia kukabiliana na madhara ya ajali ya mtambo wa nyuklia wa Chernobyl uliotokea miaka 25 iliyopita.

Umoja wa Ulaya pekee umeahidi kutoa Euro milioni 110 kusaidia kuugubika mtambo huo kwa kuta za zege. Rais wa Ukraine Viktor Yanukovych katika hotuba ya kuufungua mkutano huo mjini Kiev alisema kuwa Chernobyl ni maafa kwa dunia mzima kwa hivyo ulimwengu mzima unapaswa kushirikiana kupambana na janga hilo. Ajali ya kiwango kikubwa kama hicho haiwezi kuachiliwa Ukraine peke yake. Amesema ajali ya hivi karibuni nchini Japan pia imethibitisha kuwa matukio kama hayo ni changamoto kwa binadamu wote.

Kinu cha Chernobyl kilichomiminiwa zege hiyo miaka 25 iliyopita, sasa kina nyufa na matundu na hivyo mionzi ya sumu ya nyuklia inapenya. Ukarabati uliofanywa kati ya mwaka 2004 na 2008 umetumia vyuma kuimarisha baadhi ya kuta zilizogubika kinu hicho. Julia Marositsch anaefanya kazi katika kitengo cha ushirikiano wa kimataifa cha mtambo wa nyuklia wa Chernobyl anasema:

"Vyuma hivyo vitasaidia kuimarisha jengo hilo la zege kwa takriban miaka 15. Kwa hivyo kuna muda wa kufanya ukarabati na kumimina zege jipya ili kuwa na kuta imara zaidi."


Mtambo wa nyuklia wa Chernobyl ulioripuka 26 Aprili, 1986Kazi hiyo ya ukarabati inahitaji muda huo, kwani kazi ya mradi huo mkubwa ni ngumu kuliko vile ilivyotazamiwa kama anavyoeleza Heinz Smital, mtaalamu wa kinga ya mionzi ya nyuklia wa shirika la ulinzi wa mazingira Greenpeace.

"Haiwezekani kufanya kazi juu ya jengo hilo kwani katika sehemu hiyo viwango vya mionzi ya nyuklia ni vikubwa mno."


Gharama za ukarabati zinaongezeka kila mwaka. Kwa hivi sasa, inatathminiwa kuwa kutahitajiwa kiasi cha Euro bilioni 1 nukta 6 - na jumuiya ya kimataifa inatoa msaada - mfadhili mkubwa ni Umoja wa Ulaya. Na msaada huo unahitajiwa, kwani bado kuna hatari kubwa. Inatathminiwa kuwa asilimia 5 tu ya mionzi ya nyuklia ndio iliyotawanyika wakati wa mripuko. Hiyo humaanisha asilimia 95 bado zimo ndani ya mtambo huo. Na taka hizo za nyuklia lazima zizuiliwe ndani kwa njia yo yote ile anasema Heinz Smital wa Greenpeace.







Foleni baada benki kufunguliwa I Coast




Benki Ivory Coast


Maelfu ya raia wa Ivory Coast wamepanga foleni kutoa pesa na kupokea mishahara iliyocheleweshwa kufuatia benki nchini humo kufunguliwa tena baada ya kufungwa kwa wiki 10.

Kufungwa kwa benki hizo kulitokana na jaribio la aliyekuwa Rais Laurent Gbagbo kung'ang'ania madarakani baada ya uchaguzi wenye utata.

Kufunguliwa tena kwa mfumo wa benki ni hatua ya kufufua uchumi wa nchi inayoongoza kwa uzalishaji wa kakao duniani.

Serikali ya rais mpya Alassane Ouattara imeahidi kulipa mishahara ya miezi miwili kwa sekta za umma.

Raia wa nchi hiyo walitaarifiwa kwa kipindi kifupi juu ya kufungwa kwa benki hizo mwezi Februari, wakiacha maelfu wakihangaika kumudu maisha yao bila mishahara, mafao ya uzeeni na akiba.

Mteja mmoja aliyekuwa kwenye foleni nje ya benki iliyokuwa kwenye mji mkuu Abidjan, alisema alikuwa akisubiri tangu mapema asubuhi kutoa pesa za kutosha kwa ajili ya kulisha familia yake.

Alisema, "Ntaitunza familia yangu iliyoteseka kwa takriban miezi miwili bila ya kuwa na chakula cha kutosha. Ntawatunza watoto na kuhakikisha wanarudi shuleni. "

Sekta ya biashara nayo imekwama kufanya kazi kwa ufanisi na biashara kuu ya kakao, inabaki ikisuasua.

Mwandishi wa BBC John James aliyopo mjini humo, japo vikwazo vimeondolewa, wafanyabiashara wanahitaji akaunti zao za benki kabla ya kulipa ushuru wa forodha





Mapigano yaendelea Misrata





Mji wa Misrata bado umekuwa ukigubikwa na mapigano makali kati ya vikosi vinavyomtii kiongozi wa Libya, Kanali Muammar Gaddafi na waasi wanaoudhibiti mji huo.

Miripuko mikubwa na milio ya bunduki imesikika katika uwanja wa ndege. Misrata ni mji wa tatu kwa ukubwa nchini Libya na ndio mji wa magharibi ambao waasi wanajaribu kuutumia kuingia kwenye mji mkuu wa Tripoli.


Wakati huo huo, katika mpaka na Tunisia wanajeshi wanaomuunga mkono Kanali Gaddafi wamerusha makombora na kupambana na vikosi vya Tunisia katika jaribio la kuwaondoa waasi ambao wamekimbilia kwenye eneo la Dehiba.












Waandamanaji Syria wadai uhuru zaidi








Vyombo vya habari vya Syria vimeripoti kuwa wanajeshi wanne wameuawa na wengine wawili wametekwa na watu wanaojiita magaidi wenye silaha. Shambulio hilo limetokea kwenye mji wa kusini wa Daraa, ambako maelfu ya wananchi


wamekusanyika kudai uhuru zaidi wa kisiasa na kupuuzia umwagaji damu na ukandamizaji unaofanywa na serikali dhidi ya maandamano ya kuupinga utawala wa Rais Bashar al-Assad.


Wanaharakati na kundi la Udugu wa Kiislamu, Muslim Brotherhood, lililopigwa marufuku nchini Syria, waliwataka raia wa nchi hiyo kuingia mitaani katika siku ya ghadhabu baada ya sala ya Ijumaa,

lakini wizara ya mambo ya ndani imesema raia hawatakiwi kuandamana bila kibali. Kundi la kutetea haki za binaadamu limesema matumizi ya nguvu yaliyofanywa na serikali ya Syria yamesababisha mauaji ya watu 500 tangu maandamano yaanze katikati ya mwezi Machi.

Baadae leo wanadiplomasia kutoka serikali za Umoja wa Ulaya watakutana mjini Brussels kujadili uwezekano wa kuiwekea Syria vikwazo. Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Ujerumani, Guido Westerwelle, anashinikiza vikwazo dhidi ya Syria na kutaka hatua ngumu za kidiplomasia zichukuliwe.

'Mtume' Kupigwa Faini Kwa Kutabiri Tetemeko la Ardhi


Mwanaume mmoja wa nchini Taiwan ambaye alijitangaza kuwa yeye ni mtume amesababisha mtafaruku nchini humo baada ya kutabiri litatokea tetemeko kubwa la ardhi nchini humo mwezi mei na kusababisha watu waanze kuzikimbia nyumba zao.
Serikali ya Taiwan imetishia kumpiga faini mwanaume mmoja wa nchini humo anayejiita yeye ni mtume kwa kusababisha mtafaruku nchini humo.

Mamlaka za Taiwan zimesema kuwa Mtume huyo anayejulikana pia kwa jina la “Teacher Wang” aliandika kwenye blogu yake utabiri wa kutokea tetemeko kubwa la ardhi litakaloambatana na Tsunami.

Mtume huyo feki pia aliwataka watu wazikimbie nyumba zao kwani hazitaweza kuhimili tetemeko hilo la ardhi na kuwashauri waishi kwenye nyumba zilizotengenezwa kwa makontena ya mizigo.

Wataiwan wengi wamekuwa wakizikimbia nyumba zao na kuuhama mji na kwenda kuishi kwenye nyumba zilizotengenezwa kwa makontena kwenye miji ya ukanda wa kati wa Taiwan.

Jumla ya makontena 170 ya mizigo yameishageuzwa nyumba huku watu wengi zaidi wakitarajiwa kufuata utabiri huo wa Mtume Wang.

Serikali ya Taiwan imemtaka Wang aondoe utabiri wake kwenye blogu yake au la atapigwa faini ya dola milioni moja za Taiwan ambazo ni sawa na takribani Tsh. Milioni 50








Wanaotuhumiwa kutaka kumuua Chageni wapewa dhamana



HAKIMU Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Mkoa wa Mwanza, Agelous Rumisha, jana amewaachia kwa dhamana, watu wanne wanaotuhumiwa kula njama za kutaka kumuua alikuwa mbunge wa Busega, Dk Raphael Chegeni.

Washtakiwa katika kesi hiyo namba 113 ya mwaka 2011,ni Dismas Zacharia (47), Erasto Kazimiri (48), Queen Bogohe (37) na mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM ya Mkoa wa Mwanza, Ellen Bogohe (54).

Akitoa maamuzi kuhusu hoja kama kesi inapaswa kusikilizwa ama katika Mahakama ya Mkoa au Mahakama Kuu, hakimu huyo alisema kulingana na sheria za jinai kesi hiyo inapaswa kusikilizwa Mahakama na Kuu.

Msimamo huo ulisababisha mjadala wa kisheria baina ya mawakili wa utetezi na wa serikali.

Katika maelezp yake, hakimu huyo alisema dhamana kwa watuhumiwa ni haki yao na kwamba hilo limo katika katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

"Hivi karibuni kumekuwa na mjadala mkali kuhusu katiba ya nchi, wapo wanaosema kuwa katiba iliyopo haifai kwa sababu ina viraka vingi, lakini Ibara ya 13 Kifungu kidogo cha (b) fasihi ya 6 ya mwaka 1979 inatoa haki ya mtu ambaye hajathibitika kuwa na hatia kupewa dhamana," alieleza hakimu huyo.

Alisisita kuwa katika ibara hiyo mshtakiwa yeyote anayo haki ya kupewa dhamana isipokuwa pale Jamhuri itakapothibitisha vinginevyo.

"Huo ndiyo uzuri wa katiba hii kwa upande mwingine, hivyo natoa dhamana kwa watuhumiwa hawa lakini, kwa masharti yafuatayo," alisema.

Alitaja masharti hayo kuwa ni kila mshtakiwa kuwa na wadhamini kwa hati ya dhamana ya Sh3 milioni kila mmoja.

Alisema ingawa juzi kuliwasilishwa ombi la kutotolewa ka dhamana kwa watuhumiwa, lakini wakili wa serikali hakuwasilisha mahakamani, hati ya kupinga dhamana.

Ingawa dhamana sasa iko wazi kwa washtakiwa, lakini mshtakiwa wa kwanza Dismas Zacharia alishindwa kuachia baada ya mmoja wa wadhamini wake, kushindwa kutoa uthibitisho wa barua.

Watuhumiwa wengine walidhaminiwa na kuachiwa kwa dhamana.

Kesi hiyo itatajwa tena Mei 5 mwaka huu.

Wakati huo huo,kesi inayomkabili aliyekuwa Meya wa Jiji la Mwanza, Leonard Bihondo na wenzake watatu, pia imeahirishwa hadi Mei 6 mwaka huu.

Awali akizungumzia kesi hiyo wakili wa serikali Paschal Marungu, alisema waliiomba mahakama isigoze mbele shauri hilo ili waweze kukamilisha upelelezi ambao alidai uko katika hatua za






Amuua Bibi Yake Kwasababu ya Dola 1




Mwanaume mmoja wa nchini Marekani anashikiliwa na polisi baada ya kumuua bibi yake kwakuwa alimpa dola 1 badala ya dola 175 alizokuwa akizihitaji, aliificha maiti ya bibi yake kwenye kabati na kula uroda na kahaba kwa siku mbili kwenye kitanda cha bibi yake.
Larry Davis mwenye umri wa miaka 22 amekiri mbele ya polisi kuwa alimuua bibi yake mwenye umri wa miaka 76 Cora Davis.

Larry amewaambia polisi wa mjini Manhattan kuwa alimuomba bibi yake dola 175 lakini badala yake bibi yake huyo alimpa dola moja tu hali iliyomfanya akasirike na kuamua kumshushia kipigo cha nguvu bibi yake.

Bibi Cora alidondoka chini kwenye sakafu na kuvunjika shingo yake na baadae kupoteza maisha yake.

Ili kuficha mauaji aliyoyafanya, Larry aliificha maiti ya bibi yake kwenye kabati.

Kesi ya Larry ilichukua nafasi kubwa sana kwenye vyombo vya habari mwezi uliopita baada ya kugundulika kuwa Larry kwa kutumia pesa za bibi yake alikula uroda kwa siku mbili mfululizo na kahaba kwenye kitanda cha bibi yake huku maiti ya bibi yake akiwa ameificha kwenye kabati la nguo.

Larry bado anaendelea kushikiliwa na polisi ambapo kesi yake imepangwa kusikilizwa juni 1.

Larry amenyimwa dhamana na ataendelea kunyea debe jela mpaka hukumu ya kesi yake itakapotolewa







Mbunge ataka kuwalipia faini wafungwa 50

MBUNGE wa Morogoro Mjini, Azizi Abood, ameahidi kuwalipia faini wafungwa 50 wanaotumikia vifungo vya kati ya mwezi na mwaka mmoja, baada ya kushindwa kulipa faini.

Abood alitoa ahadi hiyo juzi baada ya kutembelea Gereza Kuu la Mkoa wa Morogoro na kuzungumza na mahabusi na wafungwa wanaotumikia adhabu za vifungo vya muda tofauti, katika gereza hilo.

Katika mazungumzo hayo, Abood alielezeav kushangazwa kwake na hatua ya msichana aliyejitambulisha kuwa Nasra Ramadhan (13), kutumikia adhabu ya kifungo cha mwaka mmoja, baada ya kushindwa kulipa faini ya Sh70,000, kwa kosa la kutoa lugha chafu.

Kufuatia maelezo ya Nasra, mbunge huyo aliomba orodheshewe idadi ya wafungwa waliohukumiwa kutumia adhabu za vifungo vya kati ya mwezi na mwaka mmoja, ambao walitakiwa kulipa faini, lakini na wakashindwa kuzilipa.

"Nimemwomba mkuu wa gereza aniorodheshe majina ya wafungwa 50 walioshindwa kulipa faini kwa makosa waliyokutwa nayo na hivyo kusababisha watumikie vifungo. Nataka kuwalipia, wameniomba na wameahadi kujirekebisha," alisema Abood.

Alisema wafungwa hao ni wale waliopaswa kulipa faini ya kati ya Sh10, 000 na Sh120,000 na kwamba lengo ni kuwafanya watoke jela na kuungana na familia zao katika katika ujenzi wa taifa.

Katika hatua nyingine, mbunge huyo ameahidi kutoa vifaa vya kupikia vyakula vya wafungwa wa gereza hilo.

Kwa mujibu wa Aboodi ahadi hiyo inatokana na kuharibika kwa baadhi ya vifaa zikiwemo sufuria zinazotumika katika kupikia vyakula.

Mbunge huyo pia alielezea kusikitizwa kwake kuhusu msongamano wa mahabusi na wafungwa katika gereza hilo na kwamba hali hiyo ni tishio kwa afya za watu hao.

Alisema kwa sasa gereza hilo lina wafungwa na mahabusi 565 wakati uwezo wake ni kuhifadhi watu 144 tu.

Alisema msongamano huo unachangiwa na ucheleweshaji wa kesi mahakamani








Rumande kwa mauaj






MKAZI wa Keko Dar es Salaam, Noel Mwapula (24), anayedaiwa kuwa mlinzi, amefikishwa Mahakama ya Wilaya ya Ilala, akikabiliwa na mashiatka yapatayo matano likiwemo la mauaji ya watu wawili katika maeneo tofauti.
Amesomekwa mashitaka yake na mahakimu wanne tofauti na awali alisomewa mashitaka Mbele ya Hakimu Karim Mushi, na Wakili wa Serikali , Alice Mtulo na kudaiwa kuwa, Agosti 21 mwaka jana, majira ya saa 3 usiku, katika eneo la Mchikichini, Dar es Salaam, mshitakiwa alimuua Omary Juma kwa makusudi


Pia imedaiwa kumuua Yassini Ramadhan Februari 23 mwaka huu, majira ya saa 2 asubuhi, katika eneo la Sharrif Shamba,jijini Dar es Salaam.

Pia Mbele Hakimu Janeth Kaluyenda imedaiwa kuwa, Machi 13 mwaka huu saa 12 jioni, katika eneo la Mchikichini, mshitakiwa alipanga njama ya kuiba kiasi cha shilingi 300,000na kabla ya alitumia vitisho ili apewe fedha hizo.

Ilidai kuwa kabla ya kuiba fedha hizo, mshitakiwa ambaye alirudishwa rumande alitumia kisu kumtishia Bena Kimaro ili ampe fedha hizo.

Kutokana dna sheria za Jamuhuri waMuungano wa Tanzania mshitakiwa hakutakiwa kujibu chochote mahakamani hapo kwa kuwa mahakama hiyo haina mamlaka ya kuendesha kesi za mauaji na mshitakiwa alirudishwa rumande hadi Mei12







Wahabeshi,Wasomali 56 wafungwa jela






MAHAKAMA ya Wilaya ya Handeni, imewahukumu kifungo cha miaka miwili jela, wahamiaji haramu 56 kutoka za Ethiopia na Somalia, baada ya kupatikana na hatia ya kuingia na kuishi nchini isivyo halali.

Mapema, Mwanasheria wa Idara ya Uhamiaji wilayani Handeni, Charles Kasambula, alisema watu hao walikamatwa Aprili 13 mwaka huu katika shamba la katani la Kwaraguru, lililoko katika Kata ya Kwedizinga.

Alisema hatuan hiyo ilikuja baada ya taarifa zilizotolewa na raia wema kuhusu kuwapo kwa kundi la watu, lililokuwa limejificha katika shamba hilo.


"Baada ya kupata taarifa hizo, tulikwenda katika eneo hilo na kukuta kundi la Wahabeshi na Wasomali wakiwa wamejificha. Walikuwa wanasubiri usiku uingie ili waendelee na safari yao," alisema Kasambula.

Kwa mujibu wa ofisa huyo, wahamiaji haramu sita miongoni mwa waliokamatwa ni wanawake na 50 wengine ni wanaume.

Alisema wapowahoji, walidai kuwa walikuwa walikuwa wanatoka Kenya na kwenda Afrika Kusini.



"Wahamiaji hao haramu walidai kuwa wamekimbia kutoka nchini mwo ili kusalimisha maisha yao kutokana na vita vya wenyewe kwa wenyewe," alisema ofisa huyo.

Kufuatia kitendo cha wahamiaji hao kukiri hilo la kuingia na kuishi nchini isivyo halali, hakimu aliyekuwa akisikiliza kesi hiyo, Jonathan Mgongolo, alisema kuwa ameridhika na maelezo ya pande zote mbili.

"Hivyo kutokana na kifungu cha sheria za uhamiaji namba 31 (1)(i) mahakama inawahukumu kutumikia kifungo cha miaka miwili jela au kulipa faini ya Sh20,000 kwa kila mmoja kwa kosa la kuvunja sheria hiyo," alisema.

Hata hivyo, wahamiaji hao walishindwa kulipa faini, jambo lililosababishwa kupelekwa jela kutumikia adhabu ya kifungo.

Wimbi la wahamiaji haramu kuingia wilayani Handeni linazidi kuwa kubwa kwa kadri siku zinavyodi kwenda mbele.

Machi mwaka huu,wahamiaji haramu 11 kutoka Somalia, waliongia Handeni na baadaye, walikamatwa










Babu amaliza mazishi ya mwanae arudi Samunge









MCHUNGAJI Mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Ambilikile Mwasapila, amerejea kijijini Samunge jana baada ya kwenda safari ya kwenda kumzika mtoto wake Jackson Masapile [43] huko mkoani Manyara.
Mchungaji MWasapile aliondoka kijijini Samunge Jumatatu ya wiki hii, majira ya saa 12 jioni na gari la Halmashauri ya wilaya ya Ngorongoro akielekea Wilayani Babati mkoani Manyara kwa ajili ya mazishi ya mwanae huyo na aliondoka kijijini Samunge na maofisa usalama kwa ajili ya ulinzi kuelekea huko.

Hivyo leo anatarajiwa kuanza kutoa dawa baada kurudi safari yake hiyo ya kumalizia mazishi ya mwanae.

Kijijini hapo wagonjwa waliweza kumsubiria mchungajihuyo kwa takribani siku atatu wakingojea arudikutoka Manyaaraili waweze kupata kikombe cha tiba











Jamhuri yagoma kujibu rufaa





JAMHURI imegoma kujibu hoja za rufaa za muomba rufaa, Danford Anthorny katika kesi ya maombi ya rufaa namba 94/2010 kwa kile ilichoelezwa kuwa mahakama iliyosikiliza kesi ya msingi haikuwa na uwezo wa kisheria.
Mrufani huyo alitiwa hatiani na Mahakama ya Wilaya ya Kilosa na kuhukumiwa adhabu ya kifungo mwaka 2009 baada ya kupatikana na hatia ya kukutwa na nyara za serikali.

Hata hivyo hakukubaliana na hukumu hiyo, hivyo akakata rufaa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam akitoa sababu nane za kupinga hukumu na adhabu hiyo.

Lakini wakati wa usikilizwaji wa rufaa hiyo, mwishoni mwa wiki serikali ambayo ni mjibu rufaa hiyo ilikataa kujibu sababu hizo za rufani ikidai kuwa mahakama iliyosikiliza kesi ya msingi haikuwa halali.

Wakili wa serikali aliyejitambulisha kwa jina moja la Katuga alidai kuwa kwa kuwa haina uwezo wa kisheria kusikiliza kesi ya namna hiyo na kwamba kwa hali hiyo shauri hilo halikuwa halali kisheria.

“Mheshimiwa Jaji, mrufani alishitakiwa kwa kosa la kukutwa na nyara za serikali kinyume cha kifungu cha 70(1) (2) cha Sheria ya Hifadhi ya Wanyama sura ya 283 kama kilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002, ambalo limo katika makosa ya uhujumu uchumi,” alisema wakili Katuga.

Alisema mahakama za chini ya Mahakama Kuu, hazina uwezo wa kisheria wa kusikiliza shauri la uhujumu uchumi isipokuwa tu kama zimepata kibali kutoka kwa Mkurugenzi wa Mashtaka(DPP) kwa mujibu wa kifungu cha 12(3).

“Lakini mahakama ya Wilaya ya Kilosa ilisikiliza kesi hii bila kuwa na kibali hicho.Kwa hiyo ilisikiliza kesi ambayo haikuwa na mamlaka nayo, hivyo shauri halikuwa halali kisheria. Kwa sababu hizo Jamhuri haina sababu ya kujibu hoja za mrufani kwa sababu si halali mbele ya sheria,” alidai Wakili Katuga.

Baada ya kusikiliza hoja za upande wa mjibu rufaa (Jamhuri) Jaji Fatuma Masengi alimuuliza mrufani iwapo alikuwa na jambo lolote la nyongeza, lakini mrufani huyo akajibu kuwa hana hivyo Jaji Masengi aliahirisha kesi hiyo hadi Mei 4 kwa ajili ya uamuzi.

Akitoa maoni yake juu ya msimamo huo wa Jamhuri nje ya mahakama, Wakili wa kujitegemea Makaki Masatu baada ya Wakili wa serikali kubainisha kasoro hizo za kisheria zilizofanywa na mahakama ya chini, alisema jaji alipaswa kumwachilia palepale muomba rufaa.

“Wakili wa serikali anapokwenda kwenye kesi haendi kutetea tu upande wa serikali hata kama kuna makosa ya kisheria bali ni lazima asimame katika sheria;

Hivyo baada ya wakili wa serikali kubainisha kasoro hizo mahakama ingeweza kumwachilia mpaka pale serikali kama ingetaka ingeweza kujipanga tena na kumshtaki upya ”, alisema. Wakili Masatu.









Matokeo kidato cha sita shule za serikali zang’ara




MATOKEO ya Kidato cha sita yaliyotangazwa yameonyesha shule za serikali kushika nafasi za juu kufaulisha wanafunzi huku wavulana waking’ara katika matokeo hayo kwa kushika 10 bora .
Matokeo ya kidato cha sita ya mwaka huu yalitangazwa jijini Dar es Salaam jana na Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la
Tanzania (NECTA), Dk. Joyce Ndalichako.

Ndalichako amesema, unaonesha kuwa daraja la kwanza waliofaulu ni asilimia 7.25, daraja la pili ni asilimia 20.23 , daraja la tatu 51 , daraja la nne 13.51 na waliopata sifuri ni asilimia 7.97 ya wanafunzi wote.

Amesema shule 10 bora zilizofaulisha wanafunzi ni za serikali zikifuatiwa na za seminari.

Pia Somo lililoongoza kwa kufaulisha wanafunzi wengi ni Uchumi ambalo limeweza kufaulisha asilimia 93 ya watahiniwa na kufuatiwa na Biashara klimefaulisha asilimia 88.7, Advanced Mathematics limefaulisha aslimia 81.5, Kemia limefaulisha asilimia 80.3, Fizikia 67.03, Basic Applied Mathematics limefaulisha asilimia 50.69 na Jiografia limefaulisha asilimia 9.65.

Baraza limefuta mitihani ya watahiniwa 12 kutokana na udanganyifu kati yao watano ni wa shule na saba wa kujitegemea ambapo pia watahiniwa 218 matokeo yao yamesitishwa hadi watakapolipa ada ya mitihani








Viongozi wa ushirika kortini wa uhujumu uchumi



TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), mkoani Kilimanjaro, imemburuta
mahakamani, Diwani wa Machame, wilayani Hai Rajabu Nkya (CCM) na watu wengine wawili kwa tuhuma za
uhujumu uchumi.

Desemba 6 mwaka jana, Mwananchi lilifichua tuhuma za kuwapo kwa vitendo vya ufisadi wa Sh52 milioni, katika Chama cha Msingi cha Ushirika cha Nkuu-Machame, ukimhusisha Nkya ambaye ni Mwenyekiti wa
chama hicho.

Hata hivyo Mwenyekiti huyo alikanusha vikali tuhuma hizo na kwamba ni chokochoko zinazochochewa na baadhi ya waliokuwa viongozi wa chama hicho walioondolewa madarakani.

Lakini jana Takukuru ilimfikisha Nkya mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Wilaya ya Hai,Denis Mpelembwa na kumsomea mashtaka mawili likiwamo la uhujumu uchumi na kushindwa kutimiza masharti ya
dhamana.

Washtakiwa wengine katika waliosomewa mashtaka hayo na Mwendesha Mashtaka wa Takukuru, Maghela Ndimbo, ni Katibu wa chama hicho, Esther Shoo na mfanyabiashara Awadhi Lema.

Katika shtaka la kwanza linalowahusu Nkya na Shoo, mwendesha mashtaka alidai kuwa kati ya Machi na Oktoba mwakan 2007, washtakiwa walikisababishia chama hicho hasara ya Sh38 milioni, kwa kununua trekta kuukuu (mtumba).Ilidaiwa kuwa trekta hilo lilinunuliwa kutoka kwa mshtakiwa Lema.

Ilidaiwa kuwa kitendo kilichofanywa na washtakiwa hao ni matumizi mabaya ya ofisi ya chama hicho, kosa ambalo ni kinyume cha kifungu namba 31 cha sheria namba 11 ya kuzuia na kupambana na Rushwa ya mwaka 2007.

Katika shtaka la pili, ilidaiwa kuwa katika kipindi hicho hicho, washtakiwa wote watatu kwa makusudi wanadaiwa kukisababishia chama hicho hasara ya Sh21,176,725 kosa linaloangukia kwenye uhujumu uchumi.

Washtakiwa Nkya na Lema walikanusha mashtaka yanayowakabili lakini mshtakiwa Shoo, akakiri kutenda kosa la matumizi mabaya ya ofisi.

Aprili 28 upande wa mashtaka utamsomea maelezo ya kosa.

Kwa kuwa kosa linaloangukia chini ya sheria ya uhujumu uchumi linamtaka mshtakiwa kuweka mahakamani fedha taslimu ambayo ni nusu ya kiasi alichosababisha hasara au hati za mali isiyohamishika yenye thamani hiyo.

Kutokana na sharti hilo, ni mshtakiwa Nkya aliwasilisha hati ya nyumba ambayo ilikataliwa na mahakama kwa kuwa ilikuwa haijaambatanishwa na ripoti ya mthamini na washitakiwa wengine waliobaki kushindwa
kutimiza sharti hilo.









Wanafunzi 1000 UDOM wafukuzwa



KUFUATIA MGOMO unaoendelea kati ya wanafunzi na uongozi wa chuo kikuu cha Dodoma imepelekea wanafunzi wapatao 1000 kusimamishwa masomo na kutakiwa kuondoka chuoni hapo.
Wanafunzi hao ni wale wa Sayansi ya Habari (Informatics) kutoka chuoni hapo wamesimamsishwa kwa muda usiojulikana kufuatia mgogoro yao na Menejimenti toka wiki iliyopita.

Naibu Makamu Mkuu wa chuo hicho anayehusika na masuala ya Taaluma, Utafiti na Ushauri, Profesa Ludovick Kinabo, amesema hatua hiyo imechukuliwa kutokana na hali ya usalama kutokuwa shwari chuoni hapo.

“Chuo kinafungwa kwa muda usiojulikana, Kamati ya Baraza la Chuo itakaa Jumatatu ndipo itaamriwa hatima ya wanafunzi hao na hatua zitakazochukuliwa baada ya kuondoka chuoni.” Alisema

Amesema vurugu hizo zimesababisha msongo wa mawazo kwa wanafunzi wengine wasiohusika chuoni hapo

Tangu wiki iliyopita chuoni hapo hali ilikuwa tete kutokana na badhi ya wanafunzi kuchochea migomona maandamano yaliyopelekea kusababisha usumbufu chuoni hapo








KUFUATIA MGOMO unaoendelea kati ya wanafunzi na uongozi wa chuo kikuu cha Dodoma imepelekea wanafunzi wapatao 1000 kusimamishwa masomo na kutakiwa kuondoka chuoni hapo.
Wanafunzi hao ni wale wa Sayansi ya Habari (Informatics) kutoka chuoni hapo wamesimamsishwa kwa muda usiojulikana kufuatia mgogoro yao na Menejimenti toka wiki iliyopita.

Naibu Makamu Mkuu wa chuo hicho anayehusika na masuala ya Taaluma, Utafiti na Ushauri, Profesa Ludovick Kinabo, amesema hatua hiyo imechukuliwa kutokana na hali ya usalama kutokuwa shwari chuoni hapo.

“Chuo kinafungwa kwa muda usiojulikana, Kamati ya Baraza la Chuo itakaa Jumatatu ndipo itaamriwa hatima ya wanafunzi hao na hatua zitakazochukuliwa baada ya kuondoka chuoni.” Alisema

Amesema vurugu hizo zimesababisha msongo wa mawazo kwa wanafunzi wengine wasiohusika chuoni hapo

Tangu wiki iliyopita chuoni hapo hali ilikuwa tete kutokana na badhi ya wanafunzi kuchochea migomona maandamano yaliyopelekea kusababisha usumbufu chuoni hapo









Wakimbizi 700,000 warudishwa Rwanda, DRC


ZAIDI ya wakimbizi 700,000 kutoka Burundi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Kongo (DRC) wamerudishwa kwao kuanzia mwaka 2000, huku wengine takriban 100,000 wakitafutiwa makazi ya kudumu nchini.

Wakimbizi hao ni wale ambao walikuwa wamepewa hifadhi nchini kwenye kambi za Nyarugusi na Ntaboba, Wilaya ya Kasulu, mkoani Kigoma. Takwimu hizo ni kuanzia mwaka 2000 hadi sasa.


Akizungumza kwenye warsha ya waandishi wa habari, Ofisa Msaidizi wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa (UNHCR) nchini, William Ngeze, alisema wakimbizi hao waliorudishwa wengi wao walikuwa mikoa ya Tabora, Kigoma na Tanga.
“Wakimbizi wengi waliorudishwa ni waimbaji wanakwaya wa Bulyanhulu na wengine kutoka kwenye kambi za Nyarugusi na Ntaboba,” alisema Ngeze.

Ngeze alisema idadi ya wakimbizi hao waliorudishwa inaonyesha jitihada kubwa zilizofanywa na UNHCR na kwamba, waliosalia ambao ni chini ya 100,000 wanatafutiwa eneo la makazi ya kudumu.
Alisema suala la kuwahamisha wakimbizi hao kutoka kwenye kambi hizo na kuwapeleka nyingine, limekuwa gumu kutokana na kukosekana kwa fedha na nchi ambayo iko tayari kuwapokea.


“Ili mtu aweze kuitwa mkimbizi lazima awe na sababu ya msingi iliyomuondoa nchini kwake, ambayo inaweza ikampelekea kukosekana kwa usalama wa maisha yake,” alisema.

Ofisa Mipango Mwandamizi wa UNHCR, Mbogozi Andrew, alisema shirika hilo linatumia dola 22 bilioni za Marekani kila mwaka kuhudumia wakimbizi hao nchini.
Pia, Andrew alisema miongoni mwa huduma wanazozitoa kwa wakimbizi, ni zile za jamii ikiwamo elimu, matibabu, chakula, makazi na malazi.

Alisema wakimbizi wanapokuwa nchini wanatakiwa kufuata sheria kama wananchi wengine na kwamba, iwapo atavunja sheria anahukumiwa kama raia mwingine.







Anywa sumu baada ya dada yake kumtamkia kuwa ana mimba ya mumewe







MWANAMKE anayetambulika kwa jina moja la Fatuma amelazimika kunywa sumu kwa aibu baada ya dada yake kumtamkia kuwa anaujauzito aliopewa na mume wake.
Mwanamke huyo ni ili habari iliyochapishwa wiki mbili zilizopita katika mtandao huu aliyeweza kumfumania mume wake na dada yake chumbani kwake.

Nifahamishe ilipata habari y a kunywa sumu kwa mwanamke huyo jana majira ya usiku na asubuhi hii ilifika nyumbani kwa mwanamke huyo na kukuta tayari alishakimbizwa zahanati kwa msaada zaidi

Imedaiwa kuwa mwanamke huyo juzi katika sikukuu ya Muungano dada yake ambaye alimfumania na mume wake wakati alipokwenda safari ya kumsalimia mama yake alimfata mdogo wake na kumuambia kuwa amsaidie kutafuta daktari ili aweze kutoa ujauzito aliokuwa nao

Imedaiwa kuwa mdogo wake huyo alijaribu kumuuliza ni kwanini autoa ndipo dada huyo alipoanza kulia na kumuomba radhi kwa mara nyingine na kumueleza alipewa na shemeji yake ambaye ni mume wa mwanamke huyo

Ndipo mwanamke huyo alianza kilio kwa mara nyingine na kwenda kwa shangazi yake aishio karibu naye kumueleza tukio hilo na kudaiwa majira ya saa moja usiku Aprili 26 alitafuta sumu ya kuulia panya bila wana familia kujua na alikoroga na kunywa
Hata hivyo imedaiwa kuwa dakika chache baadae alikutwa kitandani akiwa hoi na hatua za awali za kutoa povu zilianza kujitokeza na kudaiwa kukimbizwa hospitali

Hadi leo asubuhi mwanamke huyo anaendelea na matibabu katika zahanati moja ya karibu na maeneno hayo
Awali mwanamke huyo alimfumani mume wake na dada yake na aliweza kuacha nyumba hiyo na kwenda kwa shangazi yake lakini baadae maongezi ya kifamilia yalifanyika na kumalizika na kusameheana kwa pande zote mbili ana alirudi nyumban I kwake bila wanafamilia kutotambua kwamba alipewa ujauzito na yeye mwenye alikuwa hafahamu

Ndipo juzi jambo hilo lilijitokeza baada ya dada yake kujigundua kuwa mjamzito na kumfata mdogo wake wasaidiane kutoa ujauzito huo bila wanandugu kujua

Nifahamishe itaendelea kuwajuza kitakachoendelea kuhusiana na mtafaruku huu wa kifamilia








Ban Ki Moon ampongeza JK, wananchi





WAKATI Watanzania leo wakiadhimisha miaka 47 ya Muungano, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon, amemtumia salamu za pongezi, Rais Jakaya Kikwete, serikali na wananchi wote.


Katika salamu zake ambazo nakala yake ilitumwa katika Ubalozi wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon, alisema, kuliko ilivyokuwa wakati mwingine wowote, dunia sasa inakabiliwa na changamoto nyingi.

Alisema changamoto hizo zilizovaa sura na uzito tofauti, zinavuka mipaka kutoka katika taifa moja hadi lingine na kwamba ufumbuzi wake unahitaji utulivu, umakini, mshikamano na ushirikiano wa kimataifa.


Katibu Mkuu huyo wa Umoja wa Mataifa, alimweleza Rais Kikwete kuwa yeye binafsi, amedhamiria kuhakikisha kuwa Umoja wa Mataifa, unakwenda sambamba na kasi ya mabadiliko yanayotokea sasa duniani.

"Nakuhakikisha (Kikwete) kwamba Umoja wa Mataifa, unasimamia na kutoa matarajio yenye kuridhisha na halisi katika kazi zake tatu kuu za msingi ambazo ni maendeleo, amani na usalama na haki za binadamu," alisema Mkuu huyo wa Umoja wa Mataifa.

Pia alielezea kufarijika kwake na kupata moyo kuhusu namna uongozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, unavyojituma.


Alisema anaihesabu Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kama mshirika mkubwa katika kuifanya dunia, kuwa endelevu na salama kwa watu wote

Thursday, April 28, 2011

Wafungwa 480 Watoroka Kupitia Kwenye Kishimo Hiki




Wafungwa 480 wa Taliban nchini Afghanistan wametoroka kupitia kwenye kishimo hichi kilichochimbwa na wanamgambo wa Taliban kwaajili ya kuwatorosha wanamgambo wao waliotupwa jela na serikali ya Afghanistan.
Wafungwa hao wa jela ya mji wa Kandahar walitoroka kupitia shimo lilichimbwa kwenye sakafu ya jela hiyo na kutokezea kwenye eneo jingine lililopo umbali wa kilomita moja.

Wanamgambo wa Taliban ndio waliochimba shimo hilo ambapo walidai iliwachukua miezi mitano kulichimba handaki hilo kwaajili ya kuwatorosha wanamgambo wao waliotupwa jela na serikali ya Afghanistan.

Wafungwa hao 480 walitoroshwa usiku wa siku ya jumapili na asubuhi yake maafisa wa gereza walishangaa kukuta jela ikiwa nyeupe wafungwa wametoroka.

Msako mkali umeanzishwa kuwasaka wafungwa hao ambapo Taliban walitamba kuwa miongoni mwa wafungwa waliotoroshwa kulikuwa na makomando wao 100






Mlokole apewa notisi kwa kukera wapangaji wenzake





MWANAMKE mmoja ambaye anadaiwa kuwa ni mkristo anayeabudu katika dhehebu la Makanisa ya Kilokole amelazimika kupewa notisi na mwenye nyumba wake baada ya kuonekana kuwa kero kwa wapangaji wenzake.
Mwanamke huyo [jina linahifadhiwa] amekutwa na kadhia hiyo, Aprili 25 mwaka huu, huko maeneo ya Uwanja wa Ndege alipokuwa amepanga nyumba hiyo

Chanzo cha habari hii kilidai kuwa, mwanamke huyo anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 25 hadi 28 amedaiwa kuwa kero kwa wapangaji wenzake kwa kusababisha kelele usiku wa manane wakati akiwa katika maombi ya kumuomba Mungu.

Imedaiwa kuwa, mwanamke huyo ambaye alipanga chumba kimoja imedaiwa chumba chake kilikuwa kikitumika na waumini wenzake kama kituo cha kufanyia maombezi mara kwa mara na siku za awali walijaribu kumvumilia lakini miezi mitatu baadae baadhi ya wapangaji walishindwa kuvumilia na kuripoti tukio hilo kwa mmiliki wa nyumba hiyo ili aweze kutatua tatizo hilo

Imedaiwa kuwa mwanamke huyo amefikisha muda wa miezi mitatu na wiki mbili katika nyumba hiyo toka alipie pango lake

Imedaiwa mwanamke huyo siku za mwishoni mwa juma huwa na kawaida ya kuja na waumini wenzake na kufanya maombi chumbani kwake na kusababisha kelele mithili ya kuwa na msiba jambo ambalo lilikuwa likileta usumbufu kwa baadhi ya majirani wa nyumba hiyo hata na baadhi ya majirani wa nyumba za karibu kwa kuwa mara kwa mara walikuwa wakidhani alikuwa amefiwa na kukimbilia chumbani humo hadi walipozoea kuwa huwa anasali

Mbali na kusali na waumini wenzake majira ya mchana ama jioni, pia maombi ambayo yalikuwa yakikera watu zaidi ni yale ya usiku wa manane na kusababisha usumbufu kwa watoto na hata watu wazima kwa kuwa husababisha kelele za hali ya juu.

Kufuatia hali hiyo wapangaji waliitisha vikao na kukubaliana kuwa wafikishe ripoti hiyo kwa mwenye nyumba na hatimaye mmiliki huyo alifika hapo na kumsihi kuwa awe anafanya maombi hayo bila kusababisha usumbufu kwa wenzie

Kwa kuwa alishazoea hali hiyo ilimuia vigumu kuacha maombi hayo na baadae mmiliki huyo kuchukua uamuzi wa kumpa taarifa ya kumsimamisha mkataba ama aweze kumrudishia kodi yake iliyobaki aweze akapange nyumba nyingine

Hata hivyo mwanamke huyo hajaafiki hayo na kumtaka radhi mmiliki wa nyumba hiyo na kumwambia alikuwa ameipenda nyumba hiyo hata hivyo mwenye nyumba alimtaka amalizie mkataba ahame








Wafungwa zaidi ya 3000 wasamehewa




RAIS wa Jamuhuri wa Muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete ametoa msamaha kwa wafungwa zaidi ya 3000 katika maadhimisho ya miaka 47 ya Muungano yaliyofanyika juzi visiwani Zanzibar
Rais Kikwete ametoa msamaha huo ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha sikukuu hizo ambazo huadhimishwa kila mwaka nchini

Msahamaha alioutoa uliwahusu wafungwa waliokuwa waneakaribia kumaliza vigungo vyao, na haukuwahusu wale waliokuwa wamehukumiwa vifungo vya maisha.

Wengine waliohusika katika msamaha huo ni wafungwa wazee wenye umri wa miaka 70 au zaidi ambao umri wao utathibitishwa na jopo la waganga chini ya uenyekiti wa Mganga Mkuu wa Mkoa au wilaya.

Pia wafungwa wanawake waliofungwa gerezani wakiwa na mimba, pamoja na wale walioingia na watoto wachanga wanaonyonyesha na wasionyonya.

Waliobahatika pia ni wafungwa wenye ulemavu wa mwili na akili








Anywa sumu baada ya dada yake kumtamkia kuwa ana mimba ya mumewe






MWANAMKE anayetambulika kwa jina moja la Fatuma amelazimika kunywa sumu kwa aibu baada ya dada yake kumtamkia kuwa anaujauzito aliopewa na mume wake.
Mwanamke huyo ni ili habari iliyochapishwa wiki mbili zilizopita katika mtandao huu aliyeweza kumfumania mume wake na dada yake chumbani kwake.

Nifahamishe ilipata habari y a kunywa sumu kwa mwanamke huyo jana majira ya usiku na asubuhi hii ilifika nyumbani kwa mwanamke huyo na kukuta tayari alishakimbizwa zahanati kwa msaada zaidi

Imedaiwa kuwa mwanamke huyo juzi katika sikukuu ya Muungano dada yake ambaye alimfumania na mume wake wakati alipokwenda safari ya kumsalimia mama yake alimfata mdogo wake na kumuambia kuwa amsaidie kutafuta daktari ili aweze kutoa ujauzito aliokuwa nao

Imedaiwa kuwa mdogo wake huyo alijaribu kumuuliza ni kwanini autoa ndipo dada huyo alipoanza kulia na kumuomba radhi kwa mara nyingine na kumueleza alipewa na shemeji yake ambaye ni mume wa mwanamke huyo

Ndipo mwanamke huyo alianza kilio kwa mara nyingine na kwenda kwa shangazi yake aishio karibu naye kumueleza tukio hilo na kudaiwa majira ya saa moja usiku Aprili 26 alitafuta sumu ya kuulia panya bila wana familia kujua na alikoroga na kunywa
Hata hivyo imedaiwa kuwa dakika chache baadae alikutwa kitandani akiwa hoi na hatua za awali za kutoa povu zilianza kujitokeza na kudaiwa kukimbizwa hospitali

Hadi leo asubuhi mwanamke huyo anaendelea na matibabu katika zahanati moja ya karibu na maeneno hayo
Awali mwanamke huyo alimfumani mume wake na dada yake na aliweza kuacha nyumba hiyo na kwenda kwa shangazi yake lakini baadae maongezi ya kifamilia yalifanyika na kumalizika na kusameheana kwa pande zote mbili ana alirudi nyumban I kwake bila wanafamilia kutotambua kwamba alipewa ujauzito na yeye mwenye alikuwa hafahamu

Ndipo juzi jambo hilo lilijitokeza baada ya dada yake kujigundua kuwa mjamzito na kumfata mdogo wake wasaidiane kutoa ujauzito huo bila wanandugu kujua

Nifahamishe itaendelea kuwajuza kitakachoendelea kuhusiana na mtafaruku huu wa kifamilia








Konda Nae Kaoteshwa na Mungu -Mbagala


MKAZI wa Mbagala jijini Dar es Salaam, ameibuka na kusema kuwa ameoteshwa na Mungu kutoa dawa kwa njia ya kikombe kutibia wagonjwa wenye maradhi sugu.
Dawa hiyo amedai Mungu amemuotesha kutoa dawa ambayo ni maji ya kisima, bomba na haichanganywi na chochote zaidi ya maji hayo.

Awali kijana huyo aliyekuwa akiabudu dini ya Ukristo na baadae kubadili dini na kuwa Muislam na ndipo ameoteshwa.

Awali imedaiwa kijana huyo alikuwa akifanya kazi ya ukonda katika daladala na hivi karibuni ameibuka na kudai kuwa ameoteshwa.

Kufuatia taarifa hiyo watu wameanza kujitokeza nyumbani kwa kijana huyo kupata kikombe cha dawa hiyo huku akiwa ameshika msaahafu mkononi.

Hata hivyo Kamanda wa Polisi Temeke, wanafanya jitihada za kufanya mahojiano maalum na kijana huyo na taarifa itatolewa kwenye vyombo vya habari.

Kijana huyu ni wa saba kujitokeza na kudai wameoteshwa na Mungu na wengine wamejitokeza katika mkoa wa Mbeya, Moshi, Mbeya, Iringa, Tabora na Morogoro, Pwani wote wakidai kuoteshwa na Mungu kutoa tiba kwa njia ya kikombe






Muhogo mbichi wapoteza maisha ya mtoto



MTOTO Lawrence Gervas [4] amefariki dunia baada ya kumaliza kutafuna muhugo mbichi unaosadikiwa kuwa na sumu na watu wengine wawili kuugua kutokana na kutafuna mihogo hiyo.
Akitoa taarifa hiyo mwishoni mwa wiki, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Nonosius Komba, alisema kuwa, tukio hilo lilitokea Aprili 19, mwaka huu, majira ya saa 12 jioni huko Kata ya Igoma, Wilayani Nyamagana.

Kamanda huyo amesema kuwa mtoto huyo alifariki, baada ya kutafuna mihogo mibichi waliyokuwa wakitafuta na wenzake.

Katika tukio hilo wengine wamenusurika na kifo hicho na wanaendelea na matibabu hospitali ya Bugando kutokana na kutafuna mihogo hiyo.

Gervas alifariki dunia wakati akikimbizwa katika hospitali ya Bugando.

Taarifa hiyo imendelea kusema kuwa, “Tayari mihogo hiyo tumeipeleka kwa Mkemia Mkuu wa Serikali Kanda ya Mwanza kwa ajili ya uchunguzi wa kina ili pia kujua kiasi cha sumu iliyomo katika chakula hicho,” alisema Kamanda Komba







Maadhimisho miaka 47 Muungano








MAADHIMISHO miaka 47 ya Sikukuu ya Muungano wa Tanzania yanatarajiwa kufanyika kesho huko visiwani Zanzibar
Katika taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Waziri Mkuu imesema kuwa, maadhimisho hayo kitaifa yanatarajiwa kufanyika katika Uwanja wa Amani kisiwani Zanzibar

Maadhimisho hayo ni kumbukumbu ya kukumbuka kuungana kwa nchi mbili ambazo ni Tanganyika na Zanzibar na kupatikana Tanzania nchi zilizoungana April 26, mwaka 1964 kwa kuchanganya udongo wa pande zote mbili na waasisi wa nchi hizo.

Hivyo kila mwaka ifikapo Aprili 26 ni siku ya mapumnziko kupisha sikukuu ya kumbukumbu hizo.

Hivyo watanzania wametakiwa kujitokeza kwa wingi uwanjani hapo kusherehekea kwa pamoja sikukuu hizo na milango ya uwanja huo ityafunguliwa kuanzia majira ya 12 asubuhi kuruhusu wananchi kujumuika katika sherehe hizo









Shule ya awali Nia yafungwa





KAIMU Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Meck Sadick ametoa agizo kufungwa kwa shule ya Awali Nia iliyopoteza maisha ya watoto wanne walioangukiwa na ukuta iliyopo Kimara Matosa jijini Dar es Salaam
Hatua hiyo imekuja baada ya kugunduklika kuwa shule hiyo ilikuwa ikiendeshwa isivyo halali na mmiliki kuendesha shule hiyo bila kibali na Jacqueline Sarungi [42]

Sadick amesema kufuatia hatua hiyo shule hiyo ifungwe na kutoa onyo kali kwa shule zote zinazoendeshwa isivyo halali zigungwe haraka iwezekanavyo

“Shule zote za awali ambazo hazina usajili wala kibali za kuendesha shule hizo zifungwe, na ikigundulika sheria itafata mkondo wake

Watoto wanne walipoteza maisha katika shule wakati wakiwa wanabembea ndani ya shule hiyo na ukuta wa jirani wa nyumba iliyokuwa karibu na shule hiyo ukaanguka na kuwafikia watoto hao na kupoteza maisha papohapo

Watoto waliopoteza maisha ni Isaack Ndosi [5], Gladness Shimwela (5), Devotha Living (5)na Ludacris Lawrence (3) wote walikuwa wakazi wa Kimara B Matosa






Siogopi vitisho, mapambano yapo palepale- Nape






KATIBU wa Halmashuri Kuu, Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye, amesema atapambana vilivyo kuwang’oa mafisadi waliopo ndani ya chama hicho na kudai katika hilo haogopi mtu na kutotishika na vitisho vinavyoendelea dhidi yake.
Nape alitoa siku 90 kutaka mafisadi kujiondoa wenyewe ndani ya chama hicho na kinyume na hapo watatajwa hadhrani kwani kuwepo kwao wanakiharibu chama hicho na kukiondolea sifa.

Hata hivyo alisema hayo si maamuzi yake binafsi na kudai kuwa ni maazimi ya Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) na Kamati Kuu ya CCM yaliyoazimiwa katika vikao vyake.

Hivyo kufuatia vitisho kwa mafisadi hao amesema katika maisha yake hamwogopi mtu anapotekeleza majukumu yake ya kikazi na kuwataka wafanye wanayoyataka na kusisitiza kuwa amezaliwa katika jiji la Dar es Salaam, hivyo mapambano kwake ni mambo ya kawaida na kamwe hawezi kuogopa watu wanaomtisha.

“Mimi natimiza majukumu yangu nashangaa wanaosema kwamba nafanya mashambulizi yangu kwa ajili ya kuwalenga wanachama fulani”.

“Kwanza mimi namuamini sana Mungu na si kawaida yangu kumuogopa mtu, kwani Mungu akiamua kuniita sitaweza kupinga najua siku yangu ndio imefika’ sitaweza kukwepa” alisema Nnauye

“Sitavunjika moyo, sitakata tamaa na chochote wanachofanya mafisadi ni sawa na kumwagia petroli kwenye moto, matokeo yake ni kuendelea kuulipua na kukoleza mapambano ya vita dhidi yao,”

Hayo yamekuja baada ya kudaiwa kuna baadhi ya wanachama hawataki kujiondoa ndani ya chama hicho na kuleta vikwazo kutokana na hivi karibuni, CCM kuweka mikakati mipya ya kukijenga Chama na kuwataka watuhumiwa wa ufisadi walioko ndani ya CCM kutafakari na kuachia madaraka ndani ya siku 90, vinginevyo watalazimishwa.

Tangu kutangazwa kwa mkakati huo, kuna taarifa kuwa baadhi yao hawataki kuondoka na wamepanga kuanza kutekeleza njama za kuwachafua viongozi waandamizi wa CCM akiwemo Mwenyekiti wa Taifa wa CCM , Rais Jakaya Kikwete na familia yake.








Mfanyabiashara Rumande kwa Kuvunja Nyumba ya Mwandishi




Mfanyabiashara mmoja maarufu wa mjini Kasulu mkoani Kigoma amefikishwa katika mahakama ya wilaya hiyo akituhumiwa kuvunja na kubomoa nyumba ya mwenyekiti wa klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Kigoma ndugu Prosper Kwigize iliyopo mjini Kasulu.
Katika mahakama hiyo mwendesha mashtaka wa polisi Baraka Hongoli ameieleza mahakama hiyo juzi kuwa, Bw. Jared Bugeraha maarufu kama Bwato aliivunja nyumba hiyo yenye thamani ya shilingi milioni kumi na mbili siku ya jumanne asubuhi akishirikiana na vijana watano walioajiliwa kwa kazi hiyo.

Imeelezwa mahakamani hapo kuwa, mfanyabiashara huyo alifanya kitendo hicho baada ya kufanikiwa kuwafukuza mafundi na familia ya mwanahabari huyo akitishia kuwaua endapo wangezuia kutekelezwa kwa uharibifu huo.

Aidha imetajwa kuwa, Bw. Bwato alifanya hivyo kama sehemu ya kutekeleza azima yake ya kujichukulia sheria mkoanoni kwa kile alichotaja katika maelezo yake kwa jeshi la polisi kuwa Bw. Kwigize na wengine watatu walikuwa wamejenga nyumba zao katika viwanja vyake vilivyoko mtaa wa mwilamvya kitalu T.

Katika mahakama hiyo mshtakiwa alisomewa mashtaka mawili moja la kuvunja nyumba na kosa la pili likitajwa kuwa alitishia kumuua Bw. Masoud Kitowe mkazi wa mjini Kasulu ambaye naye amejenga nyumba yake katika eneo hilo.

Imeelezwa mahakamani hapo kuwa, mshtakiwa alikusudia kuvunja nyumba tatu ikiwemo ya Bw. Japhet Jonas ambapo kabla ya kutimiza azima yake jeshi la polisi lilipokea taarifa kutoka kwa mamlaka ya idara ya ardhi, maliasili na mazingira na kufanikisha kuzuia uharifu huo.

Hata hivyo polisi waliokwenda eneo la tukio walikuta nyumba ya Bw. Kwigize ikiwa chini na kufanikisha kuzua kipande kimoja tu cha ukuta wa nyumba hiyo yenye ukumbwa wa mita 13.5 urefu na upana mita 8 ikiwa na vyumba vinne self container, sebule moja pamoja na jiko la kupikia.

Pamoja na mhakama ya wilaya ya Kasulu kutoa mwanya wa dhamana kwa mshatakiwa ndugu zake hawakukidhi masharti na hivyo mshtakiwa akapelewa rumande hadi Mei 5, kesi yake itakapotajwa tena katika mahakama hiyo.

Hii ni mara ya nne kwa mfanya biashara huyo kuvunja nyumba za wananchi wenzake kwa visingizio mbalimbali kwa madai ya kuwepo kwa migogoro ya ardhi na amekuwa hana desturi ya kufuata sheria akitamba kuwa pesa anazomiliki zinaweza kumaliza tatizo au kesi yoyote katika maisha yake, aidha amekuwa akiwanyima mishahara watumishi wake na kuwazushia kesi za wizi ili kuwahujumu na kuwatishia kutodai madai ya posho zao







Masikini watoto hawa!




SIMANZI imetawala kwa wazazi na uongozi wa Shule ya Awali iitwayo Nia baada ya kupoteza watoto wanne kufa papohapo baada ya kuangukiwa na ukuta wakati wakiwa michezoni
Shule hiyo ya awali ‘chekechea’ ipo Kimara Matosa jijini Dar es salaam wilayani Kinondoni inamilikiwa na Jacqueline Sarungi [42] mkazi wa Kimara Matosa.

Juzi majira ya saa 6:30 mchana katika shule hiyo watoto wane walipoteza maisha papohapo na wengine watatu walijeruhiwa baada ya kuangukiwa na ukuta wa nyumba uliokuwa karibu na shule hiyo.


Watoto hao walipoteza maisha wakati walipokuwa wakibembea na ghafla waliangukiwa na ukuta wa nyumba iliyo karibu na shule hiyo

Watoto waliopoteza maisha ni Isaack Ndosi [5], Gladness Shimwela (5), Devotha Living (5)na Ludacris Lawrence (3) wote walikuwa wakazi wa Kimara B







Waislamu waliombea Taifa




WAUMINI WA KIISLAMU wamefanya maombi maalumu ya amani kuliombea Taifa la Tanzania liendelee kuwa katika amani.
Maombi hayo yaliandaliwa na Taasisi ya Waislamu ya Taibah Tanzania kwa lengo la kuliombea Taifa lisiende pabaya kwa kugawa watanzania kwa matabaka.

Mwenyekiti wa Taasisi hiyo Shehe Hassani Kiburwa, alisema wameamua kufanya Maulid hayo ya kuombea amani ya nchi, baada ya kuona kuna dalili za kutoweka kwa utulivu na amani nchini.

Katika maombi hayo waislamu walitoa wito kwa serikali kuwashughulikia wale wote wanaoonekana kutaka kulipeleka taifa pabaya

Waliitaka serikali kuwashughulikia watu hao wanaoonekana kutaka kuligawa taifa hili kwa ukabila, udini na hata wanaotaka kulifanya taifa hilo kama lao binafsi na kusahau wananchi

“Nchi hii ni ya wote na waliomo pia wanatoka kumoja, Watanzania sote tunasafiri katika jahazi moja, hivyo kama kuna mmoja






Mahakama yaamuru kufungwa kwa ukumbi



MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Mwanza, imeamuru kufungwa kwa ukumbi wa Palm Inn ulioko Kata ya Nyakato kwa kuwa ulikuwa ukisabasisha usumbufu kwa wakazi eneo hilo
Amri hiyo imetolewa na Mahakama hiyo kumtaka mmiliki wa ukumbi huo kusimamisha shughuli zake kwa kuwa ukumbi huo una shitaka mahakamani.

Mmiliki wa ukumbi huo Bw. Paulo Mushi anashitakiwa na watu wawili waliotambulika kwa majina ya Kapeji Donald na Gbral N. Mong’osyson kwa kuathirika na kelele za usiku kutoka ukumbini humo na kuwanyima usingizi nyakati za usiku.

Hivyo Mahakama hiyo imeamuru kufungwa kwa NightPub hiyo ili kupisha kumalizika kwa kesi hiyo ya madai hadi itakapomalizika

Walalamikaji hao wamefungua kesi hiyo ya madai kutaka walipwe kiasi cha shilingi million 85 kama fidia ya usumbufu huo








Askari auawa wakati akisaka walima bangi-Tabora


ASKARI Polisi Joseph mwenye namba E 9530, PC wa Kituo Kidogo cha Puge Wilayani Nzega mkoani Tabora, ameuawa kwa kupigwa mawe na kukatwa mapanga na wananchi wakati akiwa katika msako wa kukamata watu wanaolima zao aina ya bangi wilayani humo.
Akitoa taarifa hiyo jana kupitia Televisheni ya Taifa, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Bw. Liberatus Barlaw aliseman kuwa, tukio hilo lilitokea jana saa 4 asubuhi katika kata hiyo.

Wananchi hao pia waliweza kumjeruhi askari mwingine na wengine wawili walifanikiwa kukimbia.

Tarifa ya awali kutoka wilayani humo imedai kwua askari hao hawakuwa na silaha na ndo mana wananchi walipata nguvu ya kuwadhibiri kirahisi na kusababisha kifo hicho














Mwanamke mbaroni kwa kutupa mtoto chooni






HAPPY Freddy (28), mkazi wa Mikocheni, anashikiliwa na Polisi kwa kosa la kusababisha kifo cha mtoto wa kiume wa siku moja kwa kumtupa chooni.
Kamanda wa mkoa wa Kinondoni Bw. Charles Kenyela amesema kuwa, tukio hilo lilitokea juzi majira ya saa 8 mchana huko maeneo ya Mikocheni 'A'.

Kenyela amesema kuwa, taarifa hiyo iliifikia polisi baada ya wifi wa mtuhumiwa aitwae Shadya Ally (18) kupeleka taarifa kituo cha polisi Osterbay.

Amesema mtuhumiwa akiwa nyumbani kwake Mikocheni alianza kusikia uchungu wa kuashiria kutaka kujifungua na alimuomba wifi yake huyo amsindikize hospitali .

Kamanda akiendelea kutoa taarifa hiyo alisema kuwa, walianza safari ya kumpeleka hospitali lakini wakiwa njiani ghafla mtuhumiwa ambae ni ‘Happy’ alimwambia wifi yake huyo kuwa anajisikia haja na alishuka eneo hilo kwenda chooni kujisaidia na Shadya alimsubiri nje.

Amesema ghafla Shadya akiwa nje alisikia sauti ya mtoto ikilia kutoka chooni humo na aliamua kuingia na kukuta kichanga cha jinsia ya kiume kikiwa kimeegeshwa pembezoni mwa tundu la choo na kutoelewa ilikuwaje.

Kenyela alisema” wifi mtu aliamua kuwasha tochi ya simu yake ya mkononi na alimwona vizuri mtoto huyo na ghafla mtuhumiwa alikisukumiza kichanga hicho ndani ya tundu la choo kwa mguu wake na kwa madai kuwa alikuwa ameharibika.

Hivyo kufuatia tukio hilo Shadya aliomba msaada kwa majirani na kutoa taarifa kituo cha polisi kuomba kuopolewa kwa kichanga hicho na walifanikiwa kuokoa mwili huo kwa kushirikiana na polisi ukiwa tayari mfu.

Mtuhumiwa anaendelea kuhojiwa na polisi kufuatiwa tukio hilo







Daladala yauwa wawili asubuhi hii




DALADALA

WATU wawili wamefariki dunia na wengine zaidi ya 21 kujeruhiwa katika ajali iliyotokea eneo la Kigogo jijini Dar es Salaam.
Basi aina ya Toyota DCM linalofanya safari zake kati ya Kigogo Mburahati na Kivukoni limepinduka lilipofika eneo la Kigogo Festini na kusababisha ajali hiyo.

Kufuatia ajali hiyo watu wawili wameweza kupoteza maisha papohapo na kupatikana majeruhi hao










Hausigeli Jela miaka 7 Kwa Kumuiba Mtoto wa Muajiri Wake





MSICHANA wa kazi za ndani, Khadija Athumani (27), mkazi wa Kimara amehukumiwa kifungo cha miaka saba jela kwa kosa la kuiba mtoto wa mwajiri wake Victory Charles (4).
Hukumu hiyo ilitolewa jana katika Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni mbele ya Hakimu Athumani Nyamlani na huku upande wa mashitaka ulikuwa ukiongozwa na Mwendesha Mashitaka Mtani Magoma.

Mtani alidai kuwa, Februari 18, mwaka 2009 mshitakiwa alimuiba mtoto wa mwajiri wake aitwae Charles Aloyce.

Alidai kuwa aliiba mtoto huyo wakati alipokwenda kumfata mtoto huyo kumrudisha nyumbani kutoka shuleni.

Mshitakiwa huyo wakati wa ushahidi alidai kuwa alipokuwa kituoni akisubiri basi la mwanafunzi kufika kituoni hapo walitokea vijana wawili ambao alidai hawaelewi na kukaa hapo

Aliendelea kusema kuwa wakati basi hilo lilipofika kituoni hapo mtoto huyo alishuka garini na alimchukua na vijana hao walimueleza kuwa wampe hela na awape mtoto huyo na kudai alikataa

Wakati vijana hao wakiendelea kumsemesha mtoto huyo alimwambia dada huyo kuwa anahitaji kujisaidia na alimruhusu akajisaidie pembezoni na vijana hao walitoweka na mtoto huyo hakurudi.

Hata hivyo shahidi wa pili wa kesi hiyo ambae ni dereva wa basi la wanafunzi hao aliileza mahakama kuwa wakati alipofika katika kituo hicho walimkuta msichana huyo akiwa na vijana hao na walimshusha mwanafunzi huyo na basi lilisubiri kwa muda kidogo kumsubiri mzazi mwingine afike kituoni hapo kumchukua mtoto wake

Hakimu aliposikiliza ushahidi huo alitoa adhabu hiyo kali ili iwe fundisho kwa wengine na baada ya Mwendesha Mashitaka kumwambia hakimu huyo hakuwa na shtaka lingine zaidi ya hilo

Hata hivyo ndugu wa mtoto huyo hawakuridhika na hukumu hiyo kwa kuwa mtoto huyo hafahamiki yuko wapi mpaka sasa na kama yu hai ama la.








Wataka Hoteli ifungwe kwa kusababisha mauaji



WAKAZI wa Kigamboni jijini Dar es Salaam Wilayani Temeke wameipa Serikali siku zipatazo saba Hoteli ya Kitalii ya South Beach iwe imefungwa vinginevyo wataitisha maandamano kuichoma hoteli hiyo.
Pia wametaka kuondolewa kwa mwekezaji huyo nchini kwa kusababisha kifo cha Lila Hussein (34) kwa kumhisi mwizi alipoingia hotelini humo.

Imedaiwa kuwa, mwekezaji huyo amekuwa na vitendo vya kikatili vinavyoenda kinyume na haki za binadamu kwa kuwa mara kwa mara wamekuwa wakiokota maiti jirani na hoteli hiyo.

Jana kiliitishwa kikao kilichohudhuriwa na wananchi na kushirikisha maofisa wa Kituo Cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) cha jijini Dra es Salaam.

Katika kikao hicho wananchi hao wametoa mapendekezo ya kufungwa kwa hoteli hiyo na kuona ni suluhisho la kukomesha vitendo hivyo.

Pia walitaka hoteli hiyo itaifishwe na kupewa mtu mwingine ambaye atakuwa na moyo wa kibinadamu anayeweza kushirikiana na wananchi wanaolizunguka eneo hilo.

Mkazi mwingine wa eneo hilo, Mohamed Athumani (75), akizungumza katika kikao hicho alisema lazima walipize kisasi kwa kuwa ndugu yao ameuawa kikatili kwa kuchomwa moto na mwekezaji huyo bila hatia.

Hivyo waliitaka serikali kufuata maagizo hayo vinginevyo wananchi watashirikiana kwa pamoja na kuichoma moto hoteli hiyo.

Hivi sasa hoteli hiyo inalindwa na askari polisi wenye silaha baada ya mmiliki wake kushikiliwa na vyombo vya dola kwa tuhuma za kusababisha kifo hicho










Mvua zazua tafrani-Dar



MVUA zinazoendelea kunyesha jijini Dar es Salaam zimeonekana kuwa kero kwa wakazi wa jiji hilo.
Kufuatia mvua hizo imesababisha uharibifu wa miundombinu na kubwa imeweza kuvunja daraja linalounganisha barabara ya Bahama Mama ya Ubungo na Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam.

Kufuatia hali hiyo mawasiliano kwa wakazi watumiao barabara hiyo.

Manispaa ya Kinondoni imesema kuwa inafanya tathimini ili iweze kujenga daraja hilo na kurudisha mawasiliano.

Mvua kubwa zinazoendelea kunyesha jijini Dar es Salaam zimesabasisha mafuriko katika maeneo mbali mbali ya jiji la Dar es salaam.

Mvua hizo kubwa bado zinaendelea kunyesha na uharibifu zaidi unaotokana na mvua hizo unatarajiwa kutokea







Muuaji apatikana ashikiliwa na polisi







MWALIMU Kassim Bindo (25), anayedaiwa kuuwa watoto wawili wa kaka yake amepatikana na anashikliwa na polisi



Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Faustine Shilogile, amesema mtuhumiwa huyo yuko chini ya ulinzi wa polisi baada ya kukamatwa katika msako mkali uliofanywa na polisi.

Amesema mtuhumiwa huyo amekiri kuhusika na ukatili huo na uchunguzi wa kina zaidi unaendelea kuhusiana na tukio hilo.

Hivyo Kamanda huyo amesema muda wowote mtuhumiwa huyo anaweza kufikishwa mahakamani baada ya upelelezi kukamilika.

Mtuhumiwa huyo anatuhumiwa kuwaua watoto wawili ambao ni Mwanamkasi Shaban (4) na Asha Shabani mwenye umri wa siku 40 na kumjeruhi mama wa watoto hao Kuruthum Shabani [28] kwa kuwachoma na visu wakati walipokuwa wamelala nyumbani kwa babu yao huko maeneo ya Kipunguni.

Watoto hao wamezikwa jana

Awali mama wa watoto hao alikwenda nyumbani kwa wakwe zake akitokea nyumbani kwake maeneo ya Buguruni
kwa lengo la kwenda kupumzika akisubiriri kujifungua baada ya kutakiwa kwenda huko ili apate uangalizi wa karibu.

Alijifungua salama na alikuwa katika hatua za mwisho za kurudi nyumbani kwake Buguruni baada ya kukaa hapo takribani siku 40 na kabla hajarudi amekutwa na msiba huo wa kuuliwa mtoto wake mkubwa wa miaka minne na mtoto aliyejifungua akiwa hapo.

Hata hivyo imedaiwa kuwa mtuhumiwa ameonekana huenda alikuwa amechanganyikiwa na tukio hilo halikufikiriwa hata na familia.

Jana kijana huyo alikamatwa akiwa amerudi nyumbani hapo na hakutambua alichokuwa amefanya na kukuta watu wamekaa nyumbani hapo kwenye msiba na yeye kukaa na kujichanganya na watu waliofika katika msiba huo.

Ndipo alichukuliwa na kukamatwa na kufikishwa kituo cha polisi








Barcelona 2 Real Madrid 0



Nyota wa Barcelona Lionel Messi alifunga mabao mawili ya haraka haraka katika dakika za mwisho, na kuipa nafasi kubwa Barca kucheza fainali ya Klabu Bingwa Ulaya.


Messi


Kulikuwa na mvutano mkali kati ya timu hizo mbili, katika mchezo wa kwanza wa nusu fainali, hadi pale Pepe wa Real alipopewa kadi nyekundu katika dakika ya 61.

Baada ya kadi hiyo, Barca walianza kutawala, na kupata magoli hayo mawili.







Makundi hasimu ya Palestina yaafikiana





Israel inapinga muafaka huu kati ya Fatah na Hamas
Makundi mawili yanayozozana ya Fatah na Hamas yamesema yamekubaliana kuunda serikali ya mpito ya muungano huko Palestina.

Habari hii muhimu ilitangazwa nchini Misri, nchi ambayo imekuwa inajaribu kupatanisha makundi haya.

Mapigano ya makundi hayo mawili yalianza miaka minne iliopita yakiacha kundi la Fatah likidhibiti eneo la West Bank na Hamas eneo la Gaza.

Lakini hatua hii ya kuafikiana imepingwa na Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu ambaye anasema kundi la Fatah linaloongozwa na Rais Mahmoud Abbas haliwezi kufanya amani na Israel na Hamas.

Bw Netanyahu anasema lengo la Hamas ni kuangamiza Israel na kuwa hatua hii inaonyesha ulegevu wa utawala wa Rais Abbas.

Mgawanyiko kati ya Hamas na Fatah ni mkubwa na wakati mwengine kumekuwepo na maafa.

Vyombo vya usalama kutoka pande zote vimekuwa vikizozana na kuna hofu ikiwa vitaweza kuweka tofauti zao kando na kutii amri kwa utawala mmoja.

Kulingana na makubaliano hayo, Hamas watasimamia usalama wa Gaza na Fatah watadhibiti eneo la West Bank.

Ni wazi kuwa Rais Abbas amekerwa na kukwama kwa mazungumzo ya amani kati yao na Israel ndio maana ameamua kukubaliana na Hamas.

Serikali ya Marekani na Umoja wa nchi za Uropa wanalitambua kundi la Hamas kama magaidi, na haijulikani ikiwa wataendelea kufadhili utawala wa Rais Abbas baada ya muafaka huu.







Palestina yajibu kuhusu 'nyaraka za siri'




Wakimbizi wa Kipalestina, Lebanon
Maafisa wa Palestina wameishutumu al-Jazeera kwa kupotosha, baada ya kutoa taarifa za siri zilizokusudia kuonyesha nchi hiyo kuwa na maridhiano makubwa na Israel.

Rais Mahmoud Abbas alisema siri hizo zimechanganya kwa makusudi misimamo ya Palestina na Israel.

Nyaraka hizo zinasema kuwa Palestina iliikubalia Israel kubaki na eneo kubwa la mashariki mwa Israel wanalomiliki kinyume cha sheria- jambo ambalo Israel imelikataa.

BBC imeshindwa kuthibitisha binafsi nyaraka hizo.

Al-Jazeera ilisema ina rekodi 16,076 za siri za mikutano, barua pepe, na mawasiliano baina ya Palestina, Israeli na viongozi wa Marekani, baina ya mwaka 2000-2010.

Inaripotiwa Wapalestina wamependekeza kuundwa kwa kamati ya kimataifa ili kuhodhi maeneo matakatifu ya Kiislamu Jerusalem, na kupunguza idadi ya wakimbizi wanaotaka kurejea kufikia 100,000 kwa kipindi cha miaka 10.

Nyaraka hizo zinaaminiwa kutolewa kwa upande wa Palestina.

Bw Abbas, anayetarajiwa kufanya mazungumzo ya amani ya Mashariki ya kati siku ya Jumatatu na Rais wa Misri Hosni Mubarak, alisema mazungumzo ya amani yamefanyika kwa uwazi, na viongozi wenzake wa kiarabu walikuwa wakijua kila kilichoendelea.







Gaza
Akinukuliwa na shirika la habari la Reuters, alisema akiwa Cairo, " Kinachokusudiwa ni kutuchanganya. Nilishuhudia jana wakiwasilisha taarifa kama Palestina lakini walikuwa Israel...kwa maana hiyo hilo limefanywa kusudi."

Wakati huo huo, msemaji wa serikali ya Palestina, Yasser Abed Rabbo, alikataa kusema iwapo nyaraka hizo ni za kweli au la.

Alisema " Leo al-Jazeera imechapisha kwa kile kinachoita nyaraka zilizotolewa na wakurugenzi wa mapatano wa PLO."

" Hatutajadili uhalali au kutokuwa na uhalali wa nyaraka hizo."

Mhariri wa BBC wa Mashariki ya Kati Jeremy Bowen alisema kauli ya Palestina inaashiria mtikisiko mkubwa ambao nyaraka hizo za siri zinaweza kusababisha kwa Bw Abbas na wenzake.

Serikali ya Palestina kwa sasa itabidi kuwashawishi raia wa Palestina kwamba uamuzi huo ulifanyika kwa faida yao, hasa ambapo wengine wataona nyaraka hizo kama namna nyingine ya kuwadhalilisha.

Msemaji wa kundi la Hamas, ambalo linadhibiti ukanda wa Gaza na ni mpinzani wa chama cha Fatah cha Bw Abbas, alisema nyaraka hizo zilidhihirisha "ubaya wa serikali ya Palestina, na kiwango cha ushirikiano wao na umiliki wa Israel."









Vikosi vya Outtara vyauwa mshirika wake




Kiongozi wa kundi lijulikanalo kama ''Invisible Commandos'' Ibrahim Coulibaly, aliuawa katika shambulio la jumatano



Mmojapo wa viongozi maarufu wa makundi ya waasi nchini Ivory Coast ameuawa na vikosi vya Rais mpya wa nchi Alassane Ouattara.

Kiongozi wa kundi lijulikanalo kama ''Invisible Commandos'' Ibrahim Coulibaly, aliuawa katika shambulio la jumatano kwa mujibu wa msemaji wa Wizara ya Ulinzi.

Vikosi vya Bw.Coulibaly vilimsaidia Bw.Outtara katika juhudi za kudhibiti sehemu za mji mkuu Abidjan wakati wa mgogoro wa hivi karibuni.

Coulibaly ameshiriki majaribio kadhaa ya kuipindua serikali katika kipindi cha miaka kumi iliyopita. Mwaka 2002 alikuwa chachu katika mgogoro ulioigawa nchi mapande mawili hadi vikosi vya Bw.Outtara vilipompindua aliyekuwa Rais Laurent Gbagbo majuma mawili yaliyopita.

Akiwa mwenye umri wa miaka 47 na maarufu kama ''IB'' alikua mlinzi mkuu wa Bw.Outtara lakini hakutaka kusalimisha silaha zake akitaka kama wadadisi wengi walivyodhani akisubiri mchango wake katika vita vya kumuondoa Gbagbo ukubalike.

Mwandishi wa BBC mjini Abidjan, John James anasema kuwa kifo cha Bw.Coulibaly kitaondoa uwezekano wa kutokea kwa ghasia na kuikosesha utulivu serikali mpya.

Hata hivyo mwandishi wetu anasema kuwa mvutano wa ndani miongoni mwa washirika kutoka makundi ya wababe wa vita uliomuweka Rais Outtara madarakani bado unaleta wasiwasi.

Msemaji wa Wizara ya Ulinzi Capt Leon Alla Kouakou alielezea shirika la habari AFP kuwa aliiteka familia moja kufuatia hatua ya vikosi vya Bw.Outtara kumtaka asalimishe silaha zake.

Vikosi vya Ouattara vilipofyatua risasi za kumuonya alijibu kwa kutumia silaha nzito na walipojibizana kwa moto ndipo akauawa pamoja na wapambe wake.

Serikali ilipoteza askari wawili na Bw.Coulibaly kuuawa na wapiganaji wake sita katika mapigano yaliyofanyika katika kitongoji cha mji mkuu Abidjan kijulikanacho kama PK18 katika wilaya ya Abobo






Upinzani wapanga maandamano Uganda




Kisa Besigyge
Kundi la wanaharakati wa kisiasa nchini Uganda maarufu kama "Activists for Change" wanatarajiwa kurejelea tena maandamano ya kutembea hadi kazini kupinga kupanda kwa bei ya mafuta na chakula.

Naye Kiongozi wa upinzani Kizza Besigye ambaye aliachiwa huru jana baada ya wiki moja rumande ameapa kuunga mkono juhudi za kundi hilo.

Ikiwa hatashiriki, hii itakuwa mara ya kwanza yanafanyika bila viongozi wa ngazi ya juu kutoka upinzani ikizingatiwa pia kuwa mwenzake, Norbert Mao wa chama cha DP yupo chini ya ulinzi.








Maafisa wa polisi wapya wasajiliwa Kenya




Mkuu a Polisi nchini Kenya
Usajili wa makurutu watakao jiunga na kikosi polisi nchini Kenya umekamilika huku mabadiliko makubwa yakishuhudiwa ili kuhakikisha kuwepo na uwazi katika utekelezaji wa mchakato mzima.

Makurutu elfu saba walitarajiwa kusajiliwa kutoka wilaya 47 kote nchini na kujiunga na vikosi vya polisi tawala na polisi wa kawaida.

Ili kuhakisha kuwepo kwa uwazi na usawa katika usajili huo, wasajili waliweka mikakati kadhaa ili kupunguza visa vya ufisadi au ukiukaji wa sheria katika usajili wa makuruti.







Malawi na Uingereza 'zatunishiana misuli'


Uingereza imetoa amri kwa balozi wa Malawi kuondoka nchini humo kufuatia kufukuzwa "kusiko sawa" kwa balozi wa Uingereza nchini Malawi.



Rais Mutharika


Balozi wa Uingereza Fergus Cochrane-Dyet alitakiwa kuondoka Malawi baada wa kukaririwa katika waraka uliovuja akisema rais havumilii kukosolewa.

Mjumbe mmoja wa UIngereza ameonya kuwepo kwa "madhara makubwa", kwa mujibu wa waraka wa siri ambao BBC imeuona.

Asilimia 40 ya bajeti ya serikali ya Malawi inatoka nchi za nje. Uingereza ndio mhisani mkubwa zaidi.

Mualiko wa serikali ya Malawi katika haruzi ya Kifalme umefutwa pia.

Kwa mujibu wa waraka wa kibalozi uliochapishwa katika gazeti moja wiki iliyopita, Bw Cochrane-Dyet alimuelezea rais wa Malawi Bingu wa Mutharika kuwa anazidi kuwa "dikteta na kutovumilia kukosolewa".

Alisema wanaharakati wa vyama vya kiraia wamekuwa waoga baada ya kupata simu za vitisho na kusema serikali ilikuwa inazuia uhuru wa vyombo vya habari na watu wa makabila madogo.

Mwaka jana, kutokana na shinikizo kutoka kwa nchi wahisani, aliwapa msamaha wapenzi wawili wa jinsia moja waliofungwa gerezani kutokana na uhusiano wao wa kimapenzi, jambao ambalo ni kosa nchini Malawi








Kanisa latakiwa kuwashitaki makisisi wake


Nchini Rwanda kanisa katoliki bado linalaumiwa kwa kushindwa kuwafungulia mashtaka makasisi wanaotuhumiwa kuhusika katika mauaji ya kimbari ya mwaka 94.

kawadia kanisa katoliki linakuwa na mahakama zake zenye mamlaka ya kufuatilia na kuadhibu makasisi wanaofanya makosa mbali mbali.


rais Rais wa Rwanda
Lakini wakuu wa kanisa katoliki nchini Rwanda wanasema hakuna aliyefanya mauaji kwa niaba ya kanisa hilo. Na Makasisi binafsi waliohusika walitoweka kwa hivyo wasilaumiwe







Obama aonyesha cheti chake cha kuzaliwa


Ikulu ya White House huko Marekani imeonyesha cheti cha kuzaliwa cha Rais Barack Obama, kukabili uvumi wa muda mrefu kwamba kiongozi huyo hakuzaliwa Marekani.

Awali Bw Obama alikuwa ameonyesha tu cheti kinachothibitisha "alizaliwa akiwa hai" kikibainisha alizaliwa Hawaii.





Sehemu ya nakala ya cheti cha kuzaliwa Bw Obama.


Lakini wapinzani wake wamekuwa wakisisitiza kuwa Bw Obama alizaliwa Kenya, nchi alikozaliwa baba yake, na hivyo kumfanya asikidhi mojawapo ya vigezo vya kuchaguliwa kuwa rais.

Katika siku za karibuni Donald Trump anayedhaniwa kuwa na nia ya kugombea kupitia chama cha Republican alifufua uvumi huo. White House ikahisi kuna haja ya kulikabili swala hilo na kuumaliza uvumi.

Kuachana na upuuzi

Siku ya Jumatano, Bw Obama alielezea hatua hiyo isiyo ya kawaida inalenga kukomesha siasa zisizokuwa na maana, na kusema kwa miaka kadhaa amekuwa akitizama na kuchekeshwa na fitna za kuwa hakuzaliwa Marekani.

"Hatuna muda wa upuuzi wa aina hii," Bw Obama alisema. "Tuna mambo ya muhimu zaidi kufanya. Nina mambo ya maana zaidi kufanya. Tuna matatizo ya kutatua lakini tutayashughulikia, siyo swala hili."

Kutolewa kwa nakala hiyo ya cheti halisi cha Bw Obama, ambacho kilikuwa kimehifadhiwa kwenye chumba maalum chenye usalama huko Hawaii tangu kuzaliwa kwake Agosti 1961, kumetokea baada ya miaka mingi ya uzushi kutoka kwa watu wa Marekani wanaoegemea siasa za mrengo wa kulia







Dhulma nchini Libya kufanyiwa uchunguzi




Jopo hilo litachunguza dhulma zilizofanywa na majeshi ya serikali na waasi tangu Februari
Kundi la maafisa kutoka Umoja wa Mataifa limetumwa mjini Tripoli kuchunguza visa vya ukiukwaji wa haki za binadamu nchini Libya.

Jopo hilo liliteuliwa na baraza la haki za binadamu la umoja wa mataifa punde tu utawala wa Libya ulipoanza kushambulia waandamanaji wanaompinga kanali Muammar Gaddafi.

Serikali ya Libya imesema itashirikiana na jopo hilo la wachunguzi ambalo pia litachunguza madai ya dhulma zilizotekelezwa na waasi na majeshi ya Nato.

Kuna taarifa kuwa tangu maandamano ya kumpinga Kanali Gaddafi yaanze watu wametoweka, wengine wameteswa na hata kuuawa.

Kamishna wa tume ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa, Navi Pillay alisema kuwa huenda uhalifu dhidi ya binadamu unafanyika nchini Libya tangu mzozo huo uanze.

Makundi ya kutetea haki za binadamu yanasema zaidi ya watu elfu moja wameuawa na wengine wengi wamejeruhiwa katika mapigano hayo.

Meli zimekuwa zikiwasafirisha watu waliojeruhiwa hadi mjini Benghazi kupata huduma za matibabu.








Bunge kujadili ongezeko la bei ya chakula-Kenya




Raia wa Kenya wakiandamana kupinga bei ya Petroli
Nchini Kenya, Waziri mkuu Raila Odinga, leo anatarajiwa kufafanua bungeni hatua serikali inachukua kudhibiti hali.

Wiki iliopita shirika linalotetea haki za wanunuzi liliandaa maandamano katika sehemu kadhaa nchini, kulaani ongezeko hilo.

Chama cha wafanyikazi kimetisha kuongoza mgomo tarehe mosi mwezi Mei mwaka huu, ikiwa mishahara ya wafanyikazi haitaongezwa, suala linalozua wasi wasi serikalini na miongoni mwa wawekezaji.







Nigeria yachagua magavana




Upigaji kura Nigeria


Raia wa Nigeria wanapiga kura katika duru ya mwisho katika mchakato mrefu wa uchaguzi uliojaa vurugu.

Uchaguzi wa magavana 36 wenye ushawishi mkubwa umecheleweshwa katika majimbo mawili yaliyoathirika zaidi na ghasia.

Mabomu mengi zaidi yamelipuka kwenye mji wa Maiduguri kaskazini-mashariki mwa mji huo, ambapo takriban watu watatu waliuawa tangu siku ya Jumapili.

Shirika la kutetea haki za bindamu la Nigeria limesema zaidi ya watu 500 walikufa kufuatia ghasia ziliozibuka baada ya uchaguzi wa rais.

Ghasia ziliibuka upande wa kaskazini baada ya Bw Goodluck Jonathan, mkristo kutoka kusini, alipotangazwa kuwa mshindi wa uchaguzi wa Aprili 16.

Makanisa yalichomwa moto na Waislamu walilengwa katika mashambulio ya kulipiza kisasi.

Wakristo wengi walisherehekea sikukuu ya Pasaka kwenye kambi za jeshi ambapo walijihifadhi kutokana na vurugu hizo.

Licha ya kuwepo ghasia, waangalizi wengi walisema uchaguzi umekuwa bora zaidi tangu kurejeshwa kwa uongozi wa kiraia mwaka 1999.