KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Saturday, August 20, 2011

Dhuluma maishani




Wanawake wengi hujikuta katika hali ambayo wamedhulumiwa; kihisia, nyumbani, na kijinsia. Usione haya ukijikuta katika hali hii kwa maana kuna watu wengi sana wanaopitia hali moja sawa na yako. Ukipata usaidizi mapema ni vizuri. Bonyeza kwenye vivukio vifuatavyo ili upate maelezo zaidi.
Dhuluma ya kujamiiana


Ni hali ya kujamiiana ambayo inatokea bila hiari ya mtu. Una haki ya kusema ‘hapana’. Wanaodhulumu ni pamoja na watu wasiowajua, marafiki au jamaa. Hali ambapo watu wa baadhi ya familia moja wanapofanya tendo la ndoa bila ya ndoa namaranyingine niharamu kikabila au kimila au kidini namaranyingine wanapokutana kimapenzi baadhi ya watu huwaita ‘najisi’.

Dhuluma hizi ni pamoja na kunajisi, kushikashika, kumtesa mtu kwa maneno makali, hata kumlazimisha kuona picha au filamu chafu chafu. Wakati mwingine unakubali tu kwa sababu umeogopa au unaona maisha yako yakiwa hatarini.


Unaweza kukubali na pia uwe na mhasiriwa na dhulumwa za kingono.

Hakuna mtu aliye na haki ya kukushika, kuongea nawe maneno yanayohusu ngono, kukufanya utazame filamu chafu chafu za ngono au picha; ama hata kushiriki ngono ya mdomoni, utuputupu wa nyuma au ya utupu wa mbele iwapo hautaki. Kuna makundi yanayoweza kukusaidia iwapo umenajisiwa yatahakikisha kuwa haki zako zimetunzwa.


Maishani: Dhuluma inaweza kutumika katika njia nyingi zisizokuwa za kihalali. Uhalali wajambo unatokana na uwezo, ubora au utendaji wa jambo husika. Kila maamuzi yana historia. Kutokana na njia ya Ukosefu, upungufu au mchujo wa uhalisia wa picha(kitendo, msemo au ishara) husika.kwamaana hii basi utakosa umakini wakutambua maana na uhalisia wakile au yule uishi nae au yule ndugu yako ama yule rafiki yako bila kumsahau jamaa zako. Jambo zuri lakuepusha dhuluma ni uadilifu na kuishi bila kusahau muongozo wa uvumilivu na kujifunza kusamehe maishani.




Unapaswa kufanya nini iwapo umenajisiwa au kudhulumiwa kimapenzi?
Ukidhulumiwa kimapenzi, mpigie simu polisi au mtu yeyote wa kifamilia unayeweza kumwamini. Askari hawatakulazimisha kuchukua hatua lakini watakusaidia.

Usioge ama kusugua meno. Andika chini maelezo ya kila namna uliyodhulumiwa na aliyekudhulumu. Inaweza kuwa vigumu lakini ni muhimu na inahitajika kwa ushahidi.


Hakikisha kuwa polisi wanakupeleka kwanza kwenye kliniki, hospitali au kwa daktari wa upasuaji; omba kifuko cha walionajisiwa na ukaguliwe iwapo umeambukizwa magonjwa ya zinaa au u mja mzito. Ni muhimu upewe dawa za kuzuia ugonjwa wa ukimwi kwa mda was masaa 72. Iwapo ulisumishwa ambia daktari achukue mkojo wako aupime.

Tafuta mahali pa faragha, mbali na aliyekudhulumu au aliyekushambulia. Muombe rafiki mwaminifu au jamaa akusaidie kwa kukuunga mkono hata akupatie mahali pa kuishi.

Kumbuka kuwa haupaswi kulaumiwa kwa yaliyokupata. Kupona kisaikologia na kimwili huhitaji muda. Nasaha bora itakufaa zaidi.


Watu waliodhulumiwa huonyesha dalili gani?

• Kuchanganyikiwa
• Kushindwa kulala vizuri
• Kuumwa na kichwa
• Uoga ama wasiwasi
• Kuchukilia kwa uzito zaidi jambo hata likiwa jepesi
• Majonzi na huzuni kuu
• Hasira
• Ndoto mbaya ama kukumbuka yaliyopita
• Kushindwa kabisa kuona roho au hata hisia za kimapenzi
Dhuluma za kinyumbani
Hizi ni dhuluma zinazoendelezwa na mme mtu au mke mtu wa kitambo, mpenzi wa kike au kiume na mtu mnayeishi naye. Mara nyingi wanawake na watoto ndio wanaotendewa dhuluma hizi. Hata hivyo pia wanaume wanaweza kutendewa dhuluma hizi.

Wanaodhulumu ni pamoja na mpenzi miliyetalikwana naye, wazazi wako, mlezi wako, mtoto wako au mtu yeyote ambaye mumewahi kuishi naye. (Hata kama mliyejumuika pamoja kwenye tafrija, mkajamiiana ama mmepata naye mtoto).

Dhuluma hizi hudhuru maisha ya anayedhulumiwa na watoto wake. Huweza kuishia kwa mtu kupelekwa hospitalini kutibiwa, kufungwa jela maisha, ama hata kusababisha kifo. Watoto ambao wamekua wakiona dhuluma hizi na watu ambao wamedhulumiwa wakiwa wazima, hata nao watawadhulumu wengine. Wanawake wanaovumilia dhuluma kwa muda mrefu mara nyingi huuawa na wapenzi (waume) wao kwa hivyo ni muhimu wapate usaidizi na wajiondoe katika mazingira haya.

Kuna msaada wakukusaidia kukabiliana na uhusiano wa kidhuluma unaotolewa bure.












Mbu waonyesha usugu vyandarua vyenye dawa




Mbu anayeambukiza malaria

Kuna taarifa kuwa mbu wameanza sugu haraka kwa vyandarua vilivyotiwa dawa, utafiti uliofanyika nchini Senegal umeonyesha.

Katika miaka ya karibuni matumizi ya vyandarua vyenye dawa yamekuwa ndio njia kuu ya kuzuia malaria hasa barani Afrika.

Kwa mujibu wa Jarida la Utafiti wa Kisayansi kwa magonjwa ya kuambukiza la Lancet, watafiti hao pia wanasema vyandarua hivyo vinapunguza uwezo wa kuhimili maradhi ya malaria kwa watoto wakubwa na watu wazima.

Lakini waatalam wengine wanasema utafiti huo ulikuwa mdogo kufikia maamuzi kuhusu uwezo wa vyandarua kwa muda mrefu.

Katika vita dhidi ya malaria silaha rahisi na yenye uwezo mkubwa moaka sasa imekuwa vyandarua vilivyotiwa dawa yamuda mrefu.

Katika miaka michache iliyopita vyandarua vimekuwa vikisambazwa barani Afrika na kwingineko –na Shirika la Afya Duniani –WHO linasema kama vikitumika vizuri vinaweza kupunguza nusu ya athari zinazotokana na malaria.

Iwapo huu ndio mwenendo tunaoushuhudia katika sehemu za Senegal basi ina umuhimu kwa siku zijazo katika mikakati ya kudhibiti na kuzuia malaria. Alisema Dr. Joseph Keating wa Chuo kikuu cha Tulane

Nchini Senegal, vyandarua vyenye dawa milioni sita vimesambazwa katika miaka mitano iliyopita. Katika utafiti huo uliofanyika katika kijiji kidogo nchini humo na kufuatilia matukio ya malaria kabla na baada ya kuanza kusambazwa kwa vyandarua hivyo mwaka 2008.

Katika kipindi cha wiki tatu tangu kuanza kutumika, wanasayansi walikuta kuwa maambukizi yalianza kushuka –matukio ya ugonjwa huo yalikuwa chini ya mara 13 kabla vyandarua havijaanza kutumiwa.

Watafiti pia walichukua sampuli za Anopheles gambiae, mbu mwenye kusambaza vilemelea vya malaria kwa watu Afrika. Kati ya mwaka 2007 na 2010 uwiano wa vijidudu vilivyokuwa sugu kwa aina moja ya dawa vilipanda kutoka 8% hadi 48%.









Viongozi wa Kiislamu waijadili Somalia





Viongozi na maafisa kutoka nchi 57 wanachama wa jumuia ya nchi za Kiislamu, wamekutana mjini Istanbul kuzungumzia njaa nchini Somalia. Mkutano huo umeitishwa na serikali ya Uturuki.

Waziri Mkuu wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan pamoja na mkewe wanakusudia kuzuru Somalia baadae wiki hii ili kuitanabahisha dunia juu ya hali halisi wanayokabiliana watu wa Somalia.

Kwa serikali ya Uturuki kutumia muda wake mwingi kwa maswala ya Somalia ni ushahidi wa azma ya nchi hiyo ya kutanua ushawishi wake barani Afrika na katika nchi za Kiislamu licha ya kukabiliwa na migogoro kadhaa kwingineko kama vile mzozo katika nchi jirani ya Syria na machafuko katika eneo la wakurdi la kusini Mashariki .

Lakini wananchi wa Uturuki wameitikia vilivyo wito wa kusaidia wanaokabiliwa na maafa nchini Somalia kwa kutoa zaidi ya dola millioni mia moja za kimarekani.

Waziri mkuu Recep Tayyip Erdogan ameahidi kwenda Somalia baadae wiki hii pamoja na waziri wa mambo ya nje na wake zao.

Ziara za viongozi wa serikali ni nadra sana nchini Somalia.

Mkutano huu wa nchi za kiislamu uliitishwa na Uturuki li kuhimiza nchi ziongeze misaada yao na kuonyesha uungaji mkono kwa nchi za kiislamu wakati wa mwezi mtukufu wa Ramadhani.

Pia unasadifiana na malengo ya Uturuki barani Afrika ambako imeongeza idadi ya balozi zake katika miaka mitatu iliyopita na pia biashara yake kuongezeka kwa zaidi ya dola billioni saba kila mwaka.





Waziri mkuu wa Uturuki ziarani Somalia




Waziri mkuu wa uturuki Recep Tayyip Erdogan anatarajiwa kuwasili nchini Somalia kuanzisha rasmi kampeni ya kukabiliana na baa la njaa nchini humo.
Rais Sharif na BwErdogan

Raia wa uturuki wamechangia dola milioni 150 kusaidia somalia

Waziri huyo mkuu ataandamana na waziri wake wa mashauri ya nchi za kigeni na wake zao. Viongozi hao wamesema wako nchini Somalia kuonyesha wanawaunga mkono raia wa Somalia.

Raia wa Uturuki wamechanga kiasi cha dola milioni 150 hadi kufikia sasa kuisaidia Somalia.

Bendera za uturuki zimekuwa zikipaa katika uwanja wa ndege na bandari kuu mjini Mogadishu ikiwa ni ishara kuwa mji huo upo tayari kumpokea waziri mkuu Erdogan.

Ziara yake hii huenda ikawa na malengo mawili.

Moja ni kushuhudia harakati za kusamabaza misaada iliochangwa na raia wa nchi yake.

Pia kiongozi huyo na msafara wake wa mawaziri na wake zao pia unahamu kujionea wenyewe matatizo yanayo wakabili raia wa somalia.

Kando na misaada ya vyakula na madawa, raia wa uturuki wamechanga kiasi cha dola 115 milioni kusaidia walioathirika na njaa nchini humo.

Serikali ya uturuki pia inalenga sana kuongeza ushawishi wake barani Afrika.

Kando na mchango wake kibiashara, utawala huo unathamini bara hili ambalo kwa kiasi kikubwa kura zake zilisaidia nchi hii kupata nafasi ilionayo kwenye baraza la usalama la umoja wa mataifa.

Ikiwa waziri mkuu Erdogan atafaulu kuchangia kwa kiasi kikubwa kwenye mikakati ya kutatua mzozo unaoendelea nchini Somalia basi hii itakuwa njia moja ya nchi yake kupewa heshima barani humu na kwenye ngazi za kimataifa.




Mutharika afuta kazi mawaziri




Rais wa Malawi, Bingu wa Mutharika, amelifuta kazi baraza lake lote la mawaziri baada ya majuma kadha ya maandamano ya ghasia, ambapo watu karibu 20 wamekufa.
Maandamano ya Malawi

Bwana Mutharika sasa ameshika wizara zote 42; na hakutoa sababu ya kufanya hivo.

Mataifa kadha ya magharibi, yamesimamisha msaada kwa Malawi baada ya waandamanaji kuuwawa mwezi uliopita, ambao wakilalamika juu ya kupanda kwa gharama za maisha na kama walivosema, serikali mbovu.










Wapiganaji wa Libya wanajizatiti Zawiya



Wapiganaji wa Libya wanaendelea kusonga mbele kuelekea mji mkuu, Tripoli.
Wapiganaji wa Libya, mjini Zawiya

Televisheni ya wapiganaji hao imewaambia watu wajitayarishe kuwapokea.

Baada ya kuteka eneo la kati ya mji wa Zawiya, magharibi ya Tripoli, wapiganaji sasa wanasema wameiteka bandari muhimu ya Brega, mashariki mwa nchi, yenye kinu cha kusafisha mafuta.

Hakuna taarifa ya kuthibitisha hayo yanayotokea Brega.

Mwandishi wa BBC mjini Zawiya anasema kwenye medani wanayoiita medani ya mashujaa, katikati ya Zawiya, aliona majengo yaliyopigwa mabomu, yanayowaka moto, na kuta zenye matobo ya risasi.

Jana eneo hilo lilidhibitiwa kabisa na jeshi la Kanali Gaddafi.

Kulikuwa na mapigano makali jana jioni hadi usiku.

Lakini wapiganaji sasa wanaudhibiti mtaa, wamewatimua wanajeshi wa Gaddafi ambao wameelekea barabara ya kwenda Tripoli.

Kati ya medani alikuta maiti kama watatu.

Ameona maiti wanaoonesha kama Waafrika, na wapiganaji wanadai kuwa wanajeshi wengi wa Gaddafi ni askari mamluki kutoka kusini ya Sahara.

Ukweli hasa haujulikani, lakini maiti nyingi huko zinaonekana ni za Waafrika.

Sasa wapiganaji wanajitayarisha kusonga mashariki zaidi mwa mji, kuwatimua wanajeshi wa Gaddafi waliobaki Zawiya, ili kufungua njia ya kuelekea Tripoli.

Wapiganaji wa Libya wanadai kuwa waziri mkuu wa zamani, Abdessalem Jalloud, amekimbia Tripioli na amejificha katika maeneo yanayodhibitiwa na wapiganaji.







Misri itaondoa balozi wake Israil



Misri inasema kuwa imeamua kumuondosha balozi wake nchini Israel kwa sababu ya kuuwawa kwa askari wake wa usalama.
Wapalestina wanaangalia uharibifu kutokana na shambulio al Israil Gaza

Askari hao watano waliuwawa wakati wanajeshi wa Israil walipowaandama wapiganaji wa Palestina, ambao waliishambulia Israil Alkhamisi.

Huku nyuma Wamisri wameandamana mbele ya ubalozi wa Israil na kuchoma moto bendera ya Israil.

Misri imeilaumu Israil na imetaka kufanywe uchunguzi.

Israil imesema wanajeshi wake hawakuwa na makosa na kwamba itachunguza tukio hilo.

Taarifa ya serikali ya Misri inasema balozi wa Misri ataondoshwa hadi Israil itapochunguza vifo vya askari watano wa usalama wa Misri.

Jeshi la Israel limeahidi kufanya uchunguzi.

Misri imesema yaliyotokea ni kinyume na mkataba wa amani baina ya Israil na Misri.

Balozi wa Israil mjini Cairo ameitwa Wizara ya Mashauri ya Nchi za Nje kwa majadiliano zaidi.

Huku nyuma, waandamanaji nje ya ubalozi wa Israil mjini Cairo, wameipuuza taarifa iliyotolewa, na walipiga kelele na kuchoma moto bendera ya Israil.

Baadhi ya waandamanaji walibeba picha ya Hayati Rais Gamal Abdel Nasser, ambaye akijulikana kuwa dhidi ya Israil, na akitaka umoja wa nchi za Kiarabu.

Tangu mashambulio ya Alkhamisi, ndege za Israil zimeshambulia eneo la Gaza mara kadha, huku wapiganaji wa Kipalestina wameirushia Israil makombora zaidi ya 20.







Mapambano ya kikabila Sudan Kusini




Wakuu wa Sudan Kusini wanasema watu zaidi ya 500 wameuwawa kwenye mapigano ya kikabila katika jimbo la Jonglei, mashariki mwa nchi.
Bendera ya Sudna Kusini ikipandishwa

Afisa wa eneo hilo (Gabriel Duot Lam) ameiambia BBC kwamba watu mia kadha wamejeruhiwa na zaidi ya 200, wengi wakiwa watoto, walitekwa nyara.

Mapigano hayo yalitokea Alkhamisi, wakati watu wa kabila la Murle inasemekana waliwashambulia Lou Nuer,


na kuwaibia ng'ombe kama elfu 40.

Sudan Kusini ilipata uhuru mwezi uliopita na inakabili matatizo makubwa kuhusu usalama.








Tanzania yapiga marufuku uuzaji wanyama





Twiga


Tanzania imetangaza kuwa inapiga marufuku biashara ya kukamata na kuwasafirisha wanyamapori kwenda nje ya nchi.

Hatua hiyo imetangazwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda wakati akijibu hoja bungeni kuhusu madai kwamba wanyama takriban 130 wakiwemo ndege 16 walitoroshwa kinyume cha sheria mwishoni mwa mwaka jana na kusafirishwa kwenda nchi moja ya Mashariki ya Kati.

Katika jibu lake Bw Pinda alisema: “Kwanza tunataka tukubaliane na mawazo ya wabunge kwa ujumla kwamba, inaonekana eneo hili bado utaratibu wake wa usimamizi na hata namna biashara yenyewe inavyofanyika, ni eneo ambalo kwa kweli linahitaji kutazamwa upya.

“Kwa hiyo, kama serikali tumeamua kwamba, tutasimamisha usafirishaji au biashara za wanyama zote na tuangalie tena upya jambo hili na ikitokea kwamba tunakubaliana tuendelee nalo, ni dhahiri na lazima masharti yabadilike.”

Wabunge wa chama tawala pamoja na upinzani wamekuwa wakiishutumu serikali kwa kuifumbia macho kashfa hiyo.

Lakini kwa uamuzi iliofanya, serikali imeonekana kujipunguzia shutuma na kupata kuungwa mkono na wabunge wa kambi zote mbili.
Shutuma

Hata hivyo hitimisho hilo halikufikiwa bila serikali kujeruhiwa vibaya na wabunge. Hoja hizo nzito zilianza kusikika tangu mwanzoni mwa mjadala wa makadirio ya bajeti ya wizara ya maliasili na utalii kwa mwaka 2011/2012.


Mbunge Christopher Ole-Sendeka wa jimbo la Simanjiro kupitia chama tawala cha CCM alisema tukio hilo limeidhalilisha serikali na vyombo vyake vya dola vyenye majukumu ya kusimamia usalama wa nchi.

“Kinachotia fedheha kuliko yote ni kwamba, waliofanya kazi hiyo walipewa zawadi nyingine ya kupandishwa vyeo. Nataka niseme wazi kuwa mkurugenzi wa wanyamapori wa sasa, ndugu Mbangwa, hawezi kukwepa lawama ya kutoroshwa wanyama hao,” alisema Ole Sendeka aliyeonekana kuungwa mkono na wenzake.
Hatua za serikali

Habari za kutoroshwa wanyama zilianza kusikika tangu mwanzoni mwa mwaka huu, lakini mjadala wa bajeti ya Wizara ya maliasili na utalii ndiyo imeibua maswali mazito dhidi ya serikali ambayo imelazimika kutoa majibu na kuchukua hatua.

Waziri wa maliasili na utalii Ezekiel Maige aliposimama kujibu hoja zilizotolewa na wabunge wa pande zote mbili alikiri kutokea kwa tukio hilo na kusema serikali imekuwa ikilifanyia uchunguzi kwa muda wa miezi kadhaa.

Vile vile waziri huyo alitangaza kuwasimamisha kazi maafisa waandamizi wa Idara ya wanyamapori, akiwemo mkurugenzi mkuu Obeid Mbangwa, ili kuwezesha uchunguzi ufanyike kubaini swala hilo lilifanyika katika mazingira ya gani.

Tanzania inategemea utalii kwa asilimia takriban 17 ya mapato yake, ambapo kwa mwaka huu utalii unatarajiwa kuvuna dola bilioni 1.7. Wanyama ni sehemu muhimu ya vivutio vya Tanzania.






Shambulio ofisi ya Uingereza Afghanistan
Kabul




Shambulio Kabul


Washambuliaji waliojitoa mhanga wameshambulia afisi za British Council katika mji mkuu wa Afghanistan, Kabul, na kuwaua takriban watu tisa na kushikilia eneo la afisi hizo kwa saa kadhaa.

Bomu liliotegwa ndani ya gari liliangamiza ukuta unaozingira ua na watu kadhaa waliokua wamebeba silaha nzito wakavamia sehemu za ndani.

Baada ya mapambano ya saa kadhaa Balozi wa Uingereza mjini Kabul alisema washambuliaji wote waliuwawa. .

Kundi la Taleban limesema shambulio hilo linaadhimisha uhuru wa Afghanistan kutoka Uingereza mnamo mwaka 1919.

Takriban askari polisi wanane wa Afghanistan na afisa mmoja wa usalama ambae inaarifiwa ni nimwanajeshi wa huduma maalum wa New zealand waliuwawa.

Waziri Mkuu wa Uingereza David Cameron alilaani mashambulio hayo "ya kioga" akisema ameongea na Waziri Mkuu wa New Zealand John Key kumshukuru kwa mchango wa vikosi maalum vya nchi yake katika kulinda eneo hilo.

Wizara ya mambo ya nje ya Uingereza imesema raia wote wa Afrika Kusini wamepigwa na mshtuko lakini wako salama baada ya kuhamishwa kutoka jengo hilo.

Balozi wa Uingereza William Patey amesema kuna majeruhi miongoni mwa wanajeshi wa zamani waNepali wa kikosi cha Gurkha-lakini hakuna aliyekufa.









ANC ya Afrika Kusini kumuadhibu Malema





Julius Malema, kiongozi wa Vijana wa ANC

Mkutano mkuu wa chama tawala cha ANC nchini South Africa umeamua kumuadhibu kiongozi wa vijana Julius Malema kwa kuchafua sifa ya chama hicho.

Tuhuma za hivi karibuni zinatokana na kauli zake kuwa Umoja wa Vijana wa ANC utafanya uwezalo kuanzisha mabadiliko ya utawala wa nchi jirani ya Botswana.

Bw Malema alikuwa ‘akipanda mbegu za mgawanyiko’ ndani ya chama, ANC imesema.

Ni kiongozi mashuhuri Afrika Kusini lakini maoni yake kuhusu kutaifisha madini na mashamba yamesababisha hisia tofauti kutoka kwa umma.

"Komredi Julius Malema amekuwa akituhumiwa kwa matukio kadhaa ya kuvunja katiba ya ANC ikiwemo kuiingiza ANC katika migogoro kupitia kauli na matamshi yake kuhusu Botswana na kupanda mbegu za mgawanyiko katika uongozi wa Chama," Chama hicho kilisema katika taarifa yake.

ANC kinasema suala lake sasa limo mikononi mwa Kamati ya Maadili ya ANC, ambayo itaamua tarehe, mahali na muda wa kusikiliza tuhuma hizo.

Mapema wiki hii, Bw Malema amekiomba radhi ANC kwa kusema kuwa utawala wa serikali ya Botswana ni wa vibaraka na ni tishio kwa Afrika.









Msaada wa Somalia utafika kwa walengwa





Bw Andrew Mitchell

Uingereza "haitovumilia" ufisadi unaozuia jitihada za kupambana na njaa Somalia, waziri mwandamizi mmoja alisema.

Andrew Mitchell alisema alizungumzia suala hilo na waziri mkuu wa Somalia alipotembelea nchi hiyo siku ya Jumatano.

Alisema umma wa Waingereza unaochangia fedha katika wiki za hivi karibuni unahakikishiwa msaada unawafikia wale wanaostahili na si kufikishwa kwa wasiokusudiwa.

Serikali hiyo imeahidi dola za kimarekani milioni 25 zaidi kwa ajili ya chakula na dawa kusaidia watu 400,000 ambao wako katika hatari ya kufariki dunia.

Bw Mitchell alikuwa akizungumza baada ya kurejea kutoka mji mkuu wa Somalia ulioathirika na vita- ziara ya kwanza iliyofanywa na waziri kutoka Uingereza kwa kipindi cha miaka 18.

Ameonya kuwa "wanakimbizana na muda" kutatua ukame uliokithiri nchini humo na bila hatua za haraka maelfu ya watoto wanaweza kufa kwa njaa.

Saturday, August 6, 2011

Al-Shabaab wanahama Mogadishu

Kikundi cha wapiganaji wa Kiislamu wa Somalia, al Shabaab, kinasema kuwa kimeondoka katika vituo vyake kadha ndani ya mji mkuu, Mogadishu.



Wakaazi wameiambia BBC kwamba waliona misafara ya wapiganaji ikiondoka katika mji huo.

Kuhama huko kunafuatia mapigano makali jana usiku.

Kikosi cha Umoja wa Mataifa kinachoisaidia serikali ya Somalia kimekuwa kikipigana na al Shabaab mjini Mogadishu katika siku za karibuni; ili kuweza kufikisha msaada wa chakula kwa wale walioathirika na ukame nchini Somalia.

Haijulikani kama wapiganaji hao wameondoka kabisa.

Msemaji wa serikali alielezea huo kuwa "ushindi wa dhahabu" kwa watu wa Somalia.

Lakini al Shabaab, ambayo inadhibiti sehemu kubwa ya kusini mwa nchi, ilisema wameondoka kufwatana na mikakati yao na iliahidi kufanya shambulio la kulipiza.

Baadhi ya wadadisi wanafikiri al Shabaab imepungukiwa na fedha kwa sababu wafadhili wao wa Arabuni wamewapunguzia msaada tangu al Shabaab kudhoofika kijeshi.

Wadadisi wanasema al Shabaab imewahi kuwahamisha wapiganaji wake mjini Mogadishu siku za nyuma, lakini safari hii inaonesha kuondoka kwao ni ushindi mkubwa kwa serikali.









Wengi wafa katika uvamizi Somalia






Mtoto ambaye ni mkimbizi wa ndani akila huko Mogadishu


Takriban watu watano wameuawa na wengine wengi kujeruhiwa baada ya watu wenye silaha kuvamia kambi na kuiba chakula kwenye mji mkuu wa Somalia.

Wakazi wa kambi ya Badbaado, nje ya Mogadishu, walikuwa wamepanga foleni kupata msaada wakati shambulio hilo lilipotokea.

Haikujulikana wazi ni nani alihusika na shambulio hilo japo taarifa nyingine zilisema ni askari wa serikali.

Maelfu ya Wasomali walioathirika na ukame wamewasili kwenye mji mkuu wakisaka chakula.

Katika kipindi cha miezi miwili ya nyuma peke yake takriban wakimbizi 100,000 wamefika kwenye mji mkuu huo .








Sudan 'yatishia helikopta ya UN'





Afisa mwandamizi wa umoja wa mataifa amesema, Sudan ilitishia kuidungua helikopta iliyokuwa ikijaribu kuyaondosha majeshi ya kutunza amani ya umoja wa mataifa waliojeruhiwa na mabomu ya ardhini kwenye eneo lenye mgogoro la Abyei.

Mkuu wa majeshi hayo Alain Le Roy alisema umoja huu umetumia saa tatu kujaribu kuishawishi serikali kuruhusu watu hao waondolewe kwa ndege.

Wanajeshi watatu waliojeruhiwa walifariki dunia wakati majadiliano yakiendelea, alisema.


Majeshi ya kutunza amani ya Umoja wa Mataifa


Majeshi hayo ya kutunza amani yalipelekwa mapema mwezi huu huko Abyei, eneo linalozozaniwa na Sudan na taifa jipya la Sudan Kusini.

Siku chache tu baada ya kufika Ethiopia, msafara wao uligonga mabomu hayo ya ardhini huko Mabok, kusini-mashariki mwa mji wa Abyei.

Mwanajeshi mmoja alikufa papo hapo wakati wengine watatu walifariki dunia baadae, alisema Bw Le Roy, msaidizi katibu mkuu wa majeshi ya umoja wa mataifa.

Alisema, " Hatukuruhusiwa kuondoa helikopta hiyo aina ya Medivac haraka iwezekanavyo."

"Walituzuia kuondoka kwa kututishia kuwa wataidungua helikopta."

Bw Le Roy alisema "hakuna anayeweza kusema" iwapo kuchelewa kuwaondosha wanajeshi hao kwa ndege kulichangia kwa vifo vyao.

Alisema, uchunguzi unafanywa kutokana na tukio hilo.











Ukame Kenya Waturkana 14 wafa kwa njaa




Takriban watu 14 wamekufa katika eneo la Kaskazini Mashariki katika eneo la Turkana nchini Kenya, vifo vya kwanza kutokea vinavyohusiana na njaa nchini Kenya katika eneo linalohusiana na ukame.

Mbunge wa Turkana, John Munyes, alisema vifo hivyo vimetokea katika vijiji vitatu baada ya serikali kushindwa kusafirisha chakula kwa ajili ya watu walioathiriwa na ukame.

Umoja wa Mataifa unasema zaidi ya raia wa Kenya milioni nne wanatishiwa na ukosefu wa chakula katika eneo lilikumbwa na ukame mbaya katika kipindi cha miaka 60.

Nchi nyingine zilizoathiriwa ni Somalia, Ethiopia na Djiblouti.

Mwandishi wa BBC Odiambo Joseph akiwa Turkana anasema ametembelea kijiji ambacho mamia ya watu wengi wao wakiwa wazee na dhaifu walikuwa kwenye mstri mrefu wa kugawiwa chakula.

Watu 14 waliokufa nchini Kenya walikuwa watu wazima, lakini watoto pia wana utapiamlo mkali, mwandishi wa BBC anasema.

'Watu wanahisi wametelekezwa'

Bw Munyes, ambaye ni Waziri wa Kazi katika serikali ya Muungano ya Kenya, alisema idadi ya vifo ingekuwa juu kama Shirika la Msalaba Mwekundu lisingekuwa linagawa chakula cha msaada Turkana.

"Ingekuwa ni janga," alisema.

Bw Munyes alisema vifo hivyo havikusababishwa na upungufu wa chakula bali ni ‘ukosefu wa utaratibu.’

Serikali imeshindwa kusafirisha chakula kwenye vijiji hivyo, alisema.

Mwandishi wa BBC anasema watu wengi Turkana wanahisi wametelekezwa na wametoa wito kwa jamii ya kimataifa kuiangalia kwa makini hali yao mbaya.

Umoja wa Mataifa unasema ukame umesababishwa na ukosefu wa mvua kwa miaka mingi mfululizo.

Umetangaza rasmi kuwa sehemu kadhaa za Somalia zinakabiliwa na njaa.

Karibu raia 1,300 wa Somalia wengi wao wakiwa wanawake na watoto wanaingia nchini Kenya kila siku wakitafuta chakula, Umoja wa Mataifa unasema.









Masoko ya hisa duniani yaporomoka




Bei za hisa duniani zimeshuka kwa kiasi kikubwa huku kukiwa na hofu kuhusu mwelekeo wa uchumi duniani.

Mjini New York, bei ya hisa za Dow Jones zilianguka kwa pointi mia tano kiasi kikubwa zaidi kushuhudiwa kwa karibu miaka mitatu.


Bei za hisa zimeshuka kwa kiwango kikubwa kwenye masoko duniani
Kushuka kwa bei ya hisa kumesababishwa na mgogoro wa madeni ya mataifa wanachama wa bara Ulaya huku ikiofiwa kuwa huenda Italy na Uhispania zitakabiliwa na matatizo hayo.

Pia kuna hofu kwamba huenda Marekani ikakumbwa na mdororo mwingine wa kiuchumi.

Mwandishi wa BBC mjini New York anasema kengele ya kuashiria kufungwa kwa soko la hisa mjini New York liliwapa afueni wafanyibiashara ambao siku nzima walishuhudia mauzo yakishuka kwa kasi mno.

Ikiwa chini ya miaka mitatu tangu msukosuko wa kiuchumi duniani kushuhudiwa sasa wasiwasi umezuka kuwa hali hiyo huenda inarejea.

Matukio haya bila shaka sio zawadi nzuri kwa Rais wa Marekani Barack Obama ambaye leo anasheherekea miaka 50 tangu azaliwe, na hasaa wakati uchaguzi unanukia.

Wawekezaji nchini Marekani na kote duniani wamekuwa wakiuza hisa zao na badala yake kubana pesa zao au kununua hati za dhamana za serikali ya Marekani.

Hofu kuhusu kasi ya kuimarika kwa uchumi wa marekani na pia kujikokota kwa uchumi wa nchi zingine za magharibi pia ni baadhi ya sababu za kuporomoka kwa bei za hisa.

Wadadisi wanasema kuwa hali hii huenda ikawa mbaya zaidi wakati serikali ya Marekani itakapotangaza takwimu zinazoonyesha viwango vya ukosefu wa ajira nchini humo. Dalili zinaonyesha kuwa takwimu hizo sio za kufurahisha.







Njaa ya athiri maeneo zaidi Somalia





Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa sehemu zingine tatu nchini Somalia zinakabiliwa na baa la njaa.

Kufikia sasa kuna maeneo tano nchini humo yanayokabiliwa na tatizo hili.

Baadhi ya sehemu hizo tatu zilikuwa maarufu sana kwa uzalishaji wa vyakula.

Sehemu hizo tatu mpya zinapatikana kusini mwa Somalia na karibu na mji mkuu wa Mogadishu.


Janga la njaa Somalia


Kati ya sehemu hizo tatu, Afgoye corridor ndio ilio na idadi kubwa zaidi ya watu ikiwa na urefu wa takrbani kilomita thelathini kwenye barabara kuu inayounganisha mji wa mogadishu na ule wa Afgoye.

Wakati somalia ilipokuwa nchi thabiti, mji huu wa Afgoye ulikuwa na shughuli nyingi wak

ati wa asubuhi, malori mengi yalikuwa yakisafirisha mboga na matunda hadi kwenye soko kuu mjini Mogadishu.

Nyakati za jioni, ili kuwa jambo la kawaida kuona idadi kubwa ya mifugo ikisafirishwa, kupitia mji huo hadi soka kuu la mifugo mjini Mogadishu.

Mwaka wa 2007, eneo hili liligeuka na kuwa makao ya zaidi ya watu nusu milioni waliokimbia mapigano mjini mogadishu kati ya wanajeshi wa ethiopia na wapiganaji wa waasi.

Tangu wakati huo mji wa Afgoye umekuwa kwa kiasi kikubwa kutokana na kuongezeka kwa nyumba za mabanda na zile za kifahari.

Eneo hili la Afgoye corridor limewavutia wafanyabiashara wengi, kampuni ya simu ya mkononi na kampuni kadhaa za uchukuzi zimefungua ofisi zao katika sehemu hii.

Kutokana na kuongezeka kwa shughuli nyingi katika eneo hili, sasa limekuwa mji mkubwa ambao raia wake wanapata huduma za kimsingi kama vile shule na hospitali.

Mji wa pili uliotangazwa kuwa unakabiliwa na baa la njaa ni mji wa Balad, ulioko kilomita 40 kaskazini mwa mogadishu.

Mto shabelle umepita katikati mwa mji huo na shughuli nyingi za kilimo zinaendelea viungani mwake.

Eneo hili lilikuwa likizalisha kiasi kikubwa cha pamba ndiposa kiwanda cha kutengeneza nguo kilijengwa mjini humo.

Na mji wa tatu ni ule wa Adale, mji mdogo ulioko pwani, kaskazini mwa mogadishu.

Mji huo una sehemu nyingi zenye ufuo mzuri na wakuvutia na ni maarufu kwa shughuli za uvuvi.

Miji hii mitatu kwa sasa inathibitiwa na kundi la la wapiganaji wakiislamu la al shabaab.








Itachukua miaka 30 kuisafisha Ogoniland




Eneo la Ogoniland linaweza kuchukua miaka 30 kurejea katika hali ya kawaida baada ya mafuta kuharibu mazingira, ripoti ya UN imesema.

Ripoti hiyo ambayo imekuwa ikisubiriwa kwa muda mrefu inasema kurejesha mazingira yake ya asili kutathibisha kuwa ni eneo litakalochukua muda mrefu zaidi na kubwa zaidi kusafishwa duniani.

Ripoti hiyo imekutas kuwa athari za mazingira yanatishia afya ya jamii kwa angalau vijiji kumi katika eneo hilo.

Kampuni kubwa ya mafuta ya Shell imekiri kuhusika na matukio mawili ya kuvuja kwa mafuta yaliyoharibu mazingira katika jamii hizo mwaka 2008 na 2009.

Jamii moja ilisema itadai fidia ya mamia ya maelfu ya dola. Shell imesema italimaliza shauri hili kwa sheria za Nigeria.

Ripoti ya UN report, iliyotokna na uchunguzi wa miaka miwili, imethibitisha kuwapo kwa utata kwa sehemu kwa sababu iligharamiwa na kampuni ya Shell.

'Si ya kulaumu'

Mapema, Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa (Nep) liliwasilisha matokeo ya utafiti wake kwa Rais wa Goodluck Jonathan.

Nigeria ni mojawapo ya nchi zinazotoa mafuta kwa wingi duniani.

"Hii si tathmini iliyotayarishwa kulaumu mdau yeyote anayefanya kazi katika eneo la Ogoniland," Msemaji wa Unep Nick Nuttall amekiambia kipindi cha BBC cha Network Africa.

"Kile ambacho tuna matumaini nacho kwa makini ni kuwa hili litafunga ukurasa wa huzuni, hali tete na wakati mwingine habari za ghasia, zilizokuwa zikijirudia kwa miongo kadhaa.

"Tunatumaini kuwa hii itajenga aina fulani ya kushirikiana kati ya wadau mbalimbali katika eneo hili la dunia."

Mwandishi wa BBC Jonah Fisher mjini Lagos anasema tayari imejulikana kuwa ripoti hiyo inakuwa ikiangalia kisheria athari za miongo kadhaa za mafuta yaliyovuja kwa jamii za watu wanaoishi eneo la Ogoniland.

Alisisitiza pia kuwa kukubali kuwajibika kwa kampuni ya Shell kwa matukio ya kuvuja kwa mafuta mara mbili haihusiani na ripoti ya Unep.

Mafuta katika eneo la Ogoniland: Historia ya madhara
•1958: Mgomo wa mafuta katika Ogoniland
•1990: Vuguvugu la watu walioathirika Ogoni (Mosop)laundwa, likiongozwa na Ken Saro-Wiwa
•1993: Waogoni 300,000 waadnamana dhidi ya kutojali kwa serikali na kampuni ya Shell
•1993: Shell yajitoa Ogoniland baada ya mfanyakazi wake kupigwa
•1994: Viongozi wanne wa jumuiya ya Ogoni wauawa na kundi la vijana. viongozi wa Mosop akiwemo Ken Saro-Wiwa, wakamatwa
•1995: Bw Saro-Wiwa na wengine wanane wahukumiwa na kunyongwa; Dunia nzima yaishtumu serikali
•2003-2008: Jumuiya ya kimataifa yaelekeza macho yake kwa mgogoro wa kivita ulioanzishwa na jumuiya nyingine katika Niger Delta
•2011: Shell yakubali kuwa inawajibika katika matukio mawili ya kuvuja kwa mafuta katika eneo la Ogoniland spills
Madhara kwa viumbe

Martin Day, wakili anayewawakilisha watu wa Bodo katika eneo la Ogoniland, aliiambia BBC siku ya Jumatano kuwa eneo kubwa la limeharibiwa na mafuta akiimanisha kuwa jamii ya wafugaji haiwezi tena kuendesha maisha yake kama zamani.

"Matokeo yake, kwa hali hii hawawezi kuvua samaki," alisema. "Wameachwa, wengi wao, katika hali ya umaskini mkubwa."

Bw Day ameelezea kuwa uvujaji huo wa mafuta umekuwa miongoni mwa matukio yenye athari mbaya zaidi duniani lakini akasema umedharauliwa mpaka kampuni yake ilipotishia kuishtaki kampuni ya Shell katika mahakama nchini Uingereza.

Hili, alisema, litaweka mfano wa kisheria kwa jamii nyingine ambazo maisha yao yameathiriwa na makampuni ya magharibi.

Matatizo ya kimazingira yaliyosababishwa na biashara ya mafuta katika eneo Ogoniland kwanza yalianza kuzungumzwa na mwanaharakati Ken Saro-Wiwa, ambaye alinyongwa mwaka 1995 na serikali ya kijeshi ya Nigeria, na kuanzisha cheche za kimataifa kuhusu eneo hilo.

Kampeni hizo zimeilazimisha kampuni ya Shell kusimamisha shughuli za kuchimba mafuta kutoka eneo la Ogoniland lakini inaendelea kuendesha mabomba ya mafuta katika eneo hilo.

Ripoti iliyopita ya Unep iliwashutumu wenyeji wa eneo hilo kwa njama za wizi kuwa kwa 90% zimesababisha kuvuja kwa mafuta na kuleta athari na vuguvugu la wanaharakati wa eneo hilo.

Kabla ya ripoti hiyo harakati za Bw Saro-Wiwa kwa ajili ya uhai wa watu wa Ogoni (Mosop) zilishutumu hilo zikisema hawajashauriana na wenyeji vya kutosha.

Mwandishi wa BBC anasema huku SHELL ikiwa imegharamia ripoti hiyo, kutajwa popote kwa kampuni hiyo kubwa ya mafuta kwenye matokeo ya utafiti kutahitaji uchunguzi wa kina.










Video 'ikionyesha mateka Nigeria'


Video moja imetolewa inayodaiwa kumwonyesha raia wa Uingereza na mwenzake kutoka Italia waliotekwa mwezi Mei kwenye jimbo la Kebbi lililopo kaskazini magharibi mwa Nigeria.

Katika video hiyo, iliyotumwa kwenye shirika la habari la AFP nchini Ivory Coast, ilisema watekaji nyara hao ni kutoka kundi la al-Qaeda.

Inaonyesha mateka hao wakiwa wamezibwa macho na kupiga magoti, huku watu watatu wakiwa wamekamata silaha na kusimama nyuma yao.

Ofisi ya wizara ya mambo ya nje ya Uingereza ilisema ilikuwa ikichunguza kama video hiyo ni ya kweli na kusihi kusiwe na dhana.

Taarifa hiyo ilisema, " Tunajuta kutolewa kwa video kama hii kwa umma na tunasihi vyombo vya habari kuacha kutoa taarifa zisizothibitishwa wakati kama huu wenye utata."

Wizara ya mambo ya nje ya Italia imesihi video hiyo izuiwe na kusema ilikuwa ikifanya kazi kwa karibu na wenzake wa Uingereza na Nigeria.

Ikiwa itathibitishwa, itakuwa mara ya kwanza kwa kundi la al-Qaeda kwa upande wa Afrika kaskazini kufanya shughuli zake Nigeria, nchi maarufu barani Afrika na moja ya nchi zinazozalisha mafuta kwa wingi duniani.

Al-Qaeda inafanya shughuli zake zaidi katika eneo la jangwa la Sahara kaskazini mwa Nigeria, Niger, Mali na Algeria.

Wawili hao walikamatwa na watu wenye silaha jioni ya Mei 12 katika hoteli huko Birnin Kebbi, mji mkuu wa jimbo la Kebbi lililo mpakani na Niger.








Umoja wa mataifa wa laani Syria



Baraza la usalama la umoja wa mataifa kwa mara ya kwanza limetoa taarifa inayolaani ukiukaji wa haki za binadamu nchini Syria.

Kauli hiyo imetolewa miezi kadhaa baada ya mashauriano ya kina ambayo yalikuwa yamesababisha migawanyiko kwenye baraza hilo kuhusu matukio nchini humo.



Hata hivyo Lebanon imesitakuunga mkoto taarifa hiyo rasmi.

Taarifa hiyo haijatosheleza matakwa ya nchi za ulaya lakini hata hivyo imekuwa na uzito kando na ilivyo tarajiwa.

Hata hivyo baraza hilo limesisitiza kuwa suluhu ya mzozo unaoendelea nchini humo itapatikana kupitia machakato wa kisiasa utakaoongozwa na raia wa syria wenyewe.

Kauli hiyo imezima matumaini kuwa dola za kigeni zitaingilia kati mzozo unaoenedlea nchini humo.

Wanadiplomasia wanasema taarifa hiyo rasmi ya baraza la usalama ni onyo kwa utawala mjini Damascas.

Lakini Lebanon, hawajaunga mkono taarifa hiyo, suala ambalo halikutarajiwa ukizingatia ushawishi mkubwa wa Syria nchini humo.







Museveni aitisha kikao kujadili uchumi



Rais Yoweri Museveni ameitisha kikao cha dharura cha mawaziri kujadili jinsi ya kukabili nhali mbaya ya uchumi nchini humo.


Viongozi wa upinzani wamekuwa wakilalamikia kudorora kwa uchumi
Baraza hilo la mawaziri linakutana katika kipindi ambacho viongozi wa upinzani wamekuwa wakilalamikia kupanda kwa gharama za maisha.

Bidhaa muhimu kama vile sukari zimeanza kukosekana madukani hali ambayo inawaathiri watu wenye kipato cha chini nchini humo.

Mwandishi wa BBC mjini Kampala anasema bei ya sukari imepanda kiasi kwamba kile kiasi kilichoko aidha kinafichwa ama kuniauzwa bei kali ambayo sio ile ya kawaida.

katika maduka makubwa watu hawakubaliwi kununua zaidi ya kilo moja.

Hali hii inatishia uchumi wa taifa ambao kwa sasa kwa mujibu wa gavana wa benki kuu ya taifa kiwango cha ukuaji wa uchumi wa Uganda kitadidimia kwa asili mia 5 kutokana na kiwango kikubwa cha mfumuko wa bei za bidhaa.

Mfumuko wa bei unakaribia asili ia 20, kiwango kikubwa zaidi kwa kipindi cha maiaka 10.

Pia kiwango cha ubadilishanaji wa pesa za Uganda kwa dola kumepanda kiasi kuwa dola 1 inanunua shilling za Uganda 2,634.

Msemaji wa serikali na waziri wa habari bi Mary okurut amesema kikao hicho maalum cha mawaziri kitajadili mikakati ya kukabili hali hii ya uchumi.

Kuhusu kutoweka kwa sukari madukani, waziri Okurut amesema kuwa serikali imeomba ruhusa kutoka jumuiya ya Afrika mashariki ikubaliwe kuagizia sukari kutoka nje ya ukanda huu.

Uganda ina viwanda vitatu vinavyozalisha sukari, lakini ni kimoja tu kwa sasa kinachofanya kazi.

Viwili vilivyosalia, kimoja kimefungwa kwa sababu mitambo yake inafanyiwa ukarabati ilhali kingine kwa kuwa hakipati miwa inayotosheleza uzalishaji.









Mubarak wa Misri akana mashtaka




Aliyekuwa Rais wa Misri Hosni Mubarak amekana mashtaka ya rushwa na kuamuru kuuliwa kwa waandamanaji, siku ya mwanzo ya kesi yake iliyofanyika mjini Cairo.

Waandishi walisema, alipelekwa akiwa kwenye kitanda cha hospitali na kuwekwa ndani ya kizimba mahakamani humo, jambo lililowashtusha wengi waliokuwa nje.

Bw Mubarak mwenye umri wa miaka 83 anashtakiwa na watoto wake wawili wa kiume, ambao pia walikana mashtaka yanayowakabili, na pia aliyekuwa waziri wa mambo ya ndani Habib al-Adly na waliokuwa maafisa wengine sita.

Hukumu ya kuamuru mauaji ya waandamanaji ni adhabu ya kifo.

Takriban askari na polisi 3,000 wamezambazwa kuhakikisha kuna utulivu katika chuo cha mafunzo cha polisi ambapo kesi hiyo inasikilizwa.

Awali ilikuwa isikilizwe kwenye kituo cha mkutano cha Cairo lakini mamlaka husika zikahamisha eneo na kuunda mahakama ya muda ndani ya chuo hicho kutokana na suala la usalama.

Inakadiriwa watu 600 walitazama kesi hiyo ndani na nje ya mahakama, na mamilioni ya wengine wengi wakitazama kupitia televisheni.









Wahamiaji wa Libya wafa




Walinzi wa pwani huko Italia wamekuta miili ya watu 25 katika boti iliyokuwa imejaa wakimbizi wanaokimbia kutoka Libya.

Boti hiyo yenye mita 15 ilifunga gati katika kisiwa cha Lampedusa kusini mwa Italia iliyokuwa imebeba watu 271 waliookoka, shirika la habari la AFP liliripoti.

Miili ya watu hao 25 ilikutwa kwenye chumba chenye injini ya boti.

Maafisa walisema watu hao wameonekana kufariki dunia kutokana na kukosa hewa ya kutosha.

Maelfu ya wakimbizi kutoka Afrika magharibi wamewasili kwenye kisiwa hicho katika wiki za hivi karibuni.

Walinzi hao wa pwani waliingia katika boti hiyo siku ya Jumatatu na kugundua miili ya watu hao.

Vyombo vya habari vya Italia vimeripoti kuwa watu waliokuwa katika chumba hicho chenye injini walijaribu kutoka lakini walikwama kutokana na idadi ya watu waliokuwemo na huenda wakawa wamekabwa na harufu kali ya moshi kutoka kwenye injini.








Treni mpya ya kasi yaanza Afrika Kusini




Treni iendayo kasi barani Afrika, imeanza safari yake mpya kuelekea mji mkuu, Pretoria, kutoka Johannesburg katika jitahada za kurahisisha usafiri baina ya miji hiyo mikubwa ya Afrika Kusini.


Gautrain


Treni hiyo ijulikanayo kwa Gautrain inachukua chini ya dakika thelathini kwa safari ya umbali huo wa kilometa 54.

Kwa gari mwendo wa safari hiyo huchukua hadi saa mbili wakati watu wengi wakiwa wanatumia usafiri kwenda ama kurejea kazini.

Safari ya treni hiyo ya Gautrain kwa njia ya kueleka uwanja wa ndege ilizinduliwa wakati wa mashindano ya Kombe la Dunia mwaka 2010, ambapo maelfu ya mashabiki wa soka waliitumia kusafiria.

Lakini kwa kufika Pretoria, inaonekana itatumia zaidi na wasafiri wa kawaida nchini Afrika Kusini ili kukabiliana na foleni katika barabara yenye magari mengi nchini humo.

Mamia ya watu walimiminika katika kituo cha treni cha Rosebank mjini Johannedburg tangu mapema saa kumi na moja na nusu alfajiri kuwahi treni ya kwanza iliyoelekea Pretoria.

Kulikuwa na matatizo kidogo yalijitokeza, ikiwemo matatizo ya kiufundi katika behewa moja, lakini wahandisi wamesharekebisha tatizo hilo, kwa mujibu wa maafisa wa Gautrain.

Serikali imesema lengo lake ni kuufanya usafiri wa treni ndio uti wa mgongo wa mfumo wa usafiri wa umma, kwa mujibu wa Waziri wa Usafiri, Sbu Ndebele.

Treni hiyo ya Gautrain imegharimu randi bilioni 24 sawa na dola bilioni 3 kuijenga.

Kasi ya treni hiyo ni kilometa 160 kwa saa.

Gautrain inatarajiwa kupunguza idadi ya magari katika barabara ya N1 Ben Schoeman inayounganisha Pretoria na mji wa kibiashara wa Afrika Kusini wa Johannesburg kwa asilimia 20.










Mwandishi wa BBC awekwa kizuizini Misri






Shaimaa Khalil
Mwandishi wa BBC, Shaimaa Khalil, aliyekamatwa katika eneo la wazi la Tahrir kwenye mji mkuu wa Misri, Cairo ameachiwa huru.

Mazingira yake ya kuwekwa kizuizini siku ya Jumatatu mpaka sasa haiko wazi, lakini ilitokea baada ya wanajeshi, walioungwa mkono na polisi walipokwenda kwenye eneo walipokusanyika watu wengi kwa wiki tatu.

Walioshuhudia wameliambia shirika la habari la AFP kuwa waandamanaji walipigwa na simu zao za mkononi kuvunjwa.

Walisema, mtu yeyote aliyeonekana kupiga picha alishambuliwa.

BBC imetoa wito kwa mamlaka ya nchi hiyo kumwachia Khalil haraka iwezekanavyo.

Shirika hilo limesema katika taarifa yake, " Tuna wasiwasi sana juu ya kuwekwa kizuizini kwa Shaimaa Khalil huko Cairo. Ni mwandishi mzuri wa habari, akifanya tu kazi yake. Tunafanya kila liwezekanalo ili aachiwe."
Mwandishi wa BBC awekwa kizuizini Misri





Shaimaa Khalil
Mwandishi wa BBC, Shaimaa Khalil, aliyekamatwa katika eneo la wazi la Tahrir kwenye mji mkuu wa Misri, Cairo ameachiwa huru.

Mazingira yake ya kuwekwa kizuizini siku ya Jumatatu mpaka sasa haiko wazi, lakini ilitokea baada ya wanajeshi, walioungwa mkono na polisi walipokwenda kwenye eneo walipokusanyika watu wengi kwa wiki tatu.

Walioshuhudia wameliambia shirika la habari la AFP kuwa waandamanaji walipigwa na simu zao za mkononi kuvunjwa.

Walisema, mtu yeyote aliyeonekana kupiga picha alishambuliwa.

BBC imetoa wito kwa mamlaka ya nchi hiyo kumwachia Khalil haraka iwezekanavyo.

Shirika hilo limesema katika taarifa yake, " Tuna wasiwasi sana juu ya kuwekwa kizuizini kwa Shaimaa Khalil huko Cairo. Ni mwandishi mzuri wa habari, akifanya tu kazi yake. Tunafanya kila liwezekanalo ili aachiwe."

Monday, August 1, 2011

Rais wa Fifa Sepp Blatter na Rais wa Brazil Dilma Rousseff



Hivi sasa barabara mpya zinajengwa, viwanja vya ndege navyo vinaanza kupata sura mpya inayohitajika. Kumekuwa na kuchelewa kwa hapa na pale, lakini waandalizi hivi sasa wameonesha matumaini katika kazi za maandalizi. Na tofauti na uamuzi wa kuizawadia Qatar nafasi ya kuandaa Kombe la Dunia la mwaka 2022, kwa Brazil kupata nafasi hiyo ya kuandaa, hakuna cha kutiliwa mashaka kwani kandanda ndio nyumbani kwake Brazil.


Tuangalie nchi za Afrika zilivyopangwa.

Mzunguko wa kwanza utakayo kuwa na mechi 12 za nyumbani na ugenini kati ya tarehe 11 hadi 15 mwezi wa Novemba, ambapo washindi watasonga mbele katika patashika za mzunguko wa pili.

Seychelles na Kenya

Guinea Bissau na Togo

Djibouti na Namibia

Mauritius na Liberia

Visiwa vya Comoro na Msumbiji

Equatorial Guinea na Madagascar

Somalia na Ethiopia

Lesotho na Burundi

Eritrea na Rwanda

Swaziland na jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo

Visiwa vya Sao Tome na Principe na Congo

Chad na Tanzania
- - -


Kwa makundi nchi hizo zimepangwa hivi:

Kundi A

Afrika Kusini
Botswana
Jamhuri ya Afrika ya Kati
Somalia na Ethiopia
- - -

Kundi B

Tunisia, Visiwa vya Cape Verde, Sierra Leone, Equatorila Guinea na Madagascar


- - -
Kundi C
Ivory Coast
Morocco
Gambia
Chad/Tanzania
- - -
Kundi D
Ghana
Zambia
Sudan
Lesotho/Burundi
- - -
Kundi E
Burkina Faso
Gabon
Niger
Sao Tome and Principe/Congo
- - -
Kundi F
Nigeria
Malawi
Seychelles/ Kenya
Djibouti/Namibia
- - -
Kundi G
Egypt
Guinea
Zimbabwe
Comoros Islands/Msumbiji
- - -
Kundi H
Algeria
Mali
Benin
Eritrea/ Rwanda
- - -
Kundi I
Cameroon
Libya
Guinea Bissau/Togo
Swaziland/Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo
- - -
Kundi J
Senegal
Uganda
Angola
Mauritius/Liberia

Mechi zitachezwa kati ya tarehe 1 mwezi wa Juni, 2012 na tarehe 10 mwezi wa Septemba 10, 2013.


Washindi wa kila kundi watasonga mbele hadi raundi ya tatu, wakicheza mechi za nyumbani na ugenini kati ya tareh 11 hadi 15 mwezi wa Oktoba, 2013 na washindi ndio watafuzu kucheza katika fainali za Kombe la Dunia mwaka 2014 nchini Brazil.











Muafaka kuhusu deni la marekani





Rais Barack Obama ametangaza kuwa viongozi wa chama cha Republican na chake cha Democratic wameafikiana kuhusu mpango wa kulipia deni la serikali.
Rais Obama

Marekani itapunguza matumizi yake kwa dola trilioni moja

Bw Obama amesema chini ya makubaliano hayo nchi hiyo itapunguza matumizi yake kwa dollar trilioni moja katika kipindi cha miaka kumi ijayo.

Hata hivyo mpango huo utapigiwa kura kwenye baraza za senate hii leo.

Muafaka huo umefikiwa ikiwa imebakia siku moja tuu kabla ya makataa ya kuongeza kiwango cha kukopa fedha za kulipia madeni yake.

Kwa wiki kadhaa, viongozi wa vyama hivyo wamekuwa wakivutana kuhusu njia bora ya kufuata kukabili madeni ya marekani.

Hali ambayo ilitishia kukwamihsa shughuli za serikali.

Baraza la senate lina hadi kesho kupiga kura kuongeza kiwango hicho cha kukopa hadi dola trilioni 14 lau sivyo shughuli za serikali zitakwama.

Rais Obama amesema kuwa mpango ulioafikiwa sio ule aliotarajia lakini amelazimika kuukubali ilikuwezesha huduma za serikali kuendelea na madeni yake yalipwe.

Utawala wa Rais Obama ulikuwa unakabiliwa na shinikizo kali kutoka kwa wapinzani kutoka chama cha Republican ambao walikuwa wanapinga pendekezo lake la kuwepo na mpango ambao utasitiri hali hadi mwisho wa mwaka ujao.

Chama cha Republicans kilitaka mpango huo uwepo hadi katikati ya mwaka ujao. Lakini sasa vyama hivyo vimekubaliana kuunda kamati maalum itakayotoa mapendekezo mapya mwezi Novemba.


















Bush Welcomes President-Elect Obama To White House




In This Photo: George W Bush, Michelle Obama, Barack Obama, Laura Bush
(AFP OUT) U.S. President George W. Bush (L) and Laura Bush (2nd-L) greet U.S. President-elect Barack Obama (R) and his wife Michelle Obama (2nd-R) on the South Portico of the White House November 10, 2008 in Washington, DC. This is the first visit for Barack Obama to the White House before he is sworn into office as President of the United States. First lady Laura Bush took soon to be first lady Michelle Obama on a tour of the White House as the President and Mr. Obama walked along the colonnade to the Oval Office where they will have a meeting. On January 20th Obama will be sworn in as the 44th president of the United States.



Michelle Obama, Laura Bush




In this handout image provided by the White House, First Lady Laura Bush (L) meets with U.S. President-elect Barack Obama's wife Michelle Obama in the private residence of the White House November 10, 2008 in Washington, DC. This is the first visit for Barack Obama to the White House before he is sworn into office as President of the United States. First lady Laura Bush took soon to be first lady Michelle Obama on a tour of the White House as the President and Mr. Obama walked along the colonnade to the Oval Office where they had a meeting. On January 20th Obama will be sworn in as the 44th president of the United States.







Rais Obama atofautiana na upinzani.







Rais Barack Obama

Rais Barack Obama amekuwa na kikao kilichokumbwa na mjala na maneno makali wakati wa kujadili nakisi ya bajeti ya kitaifa.

Mmoja wa wabunge wa upinzani aliyeshiriki kikao hicho ambacho kilikuwa cha nne na kushirikisha wabunge wa upinzani kutoka chama cha republican amenukuliwa akisema kwamba rais Obama alionekana mwenye kero na kuapa kutoridhia masharti ya upinzani na liwalo liwe.

Hata hivyo mmoja wa wabunge wa Democrats amesema taarifa kwamba rais aliondoka kwa ghathabu kutoka kikao hicho zilitiliwa chumvi.

Awali mmoja ya mashirika ya kutathmini viwango vya uchumi wa dunia ilionya dhidi ya uchumi wa Marekani kudorora zaidi ikiwa taifa halitatua nakisi ya bajeti inayokisiwa kufikia dola trilioni 14.











Bajeti ya Marekani imekwama







Mjadala kati ya wanasiasa, kuhusu bajeti, na jinsi ya kuzidisha kiwango cha mkopo wa serikali ya Marekani ungali umekwama.
Biramu linaloonesha deni la taifa nje ya ofisi ya kodi za mapato, Marekani.

Ufumbuzi unatakiwa ufikiwe kabla ya Jumaane, ambapo Wizara ya Fedha itaanza kupungukiwa na fedha za kulipia matumizi ya serikali.

Ijumaa usiku, baraza la wawakilishi, ambalo wabunge wake wengi ni kutoka chama cha Republican, lilipitisha mswada kuzidisha kiwango cha mkopo na kupunguza matumizi ya serikali, lakini mswada huo ulikataliwa na baraza la Senate, lenye wajumbe wengi wa chama cha Democrat.

Hali ya uhasama na mashindano imetanda Washington huku Jumaane inakaribia.

Wanasiasa bado wanavutana wakati wanahitaji kupatana ili kuepuka wasi-wasi na pengine matafaruku katika uchumi wa Marekani, ikiwa muafaka haukufikiwa kabla ya tarehe ya mwisho, yaani tarehe mbili Agosti.

Mswada uliopendekezwa na wabunge wa chama cha upinzani cha Republican Ijumaa, katika baraza la wawakilishi, ulizimwa katika baraza la Senate, ambako wajumbe wa chama cha Democrat sasa wanashindana na upinzani, na wanajaribu kusukuma mbele pendekezo lao wenyewe.

Lakini mswada huo piya, uliopendekezwa na kiranja wa chama cha Democrat, Harry Reid, unafanyiwa kazi ili ukubalike kwa wengi.

Vikao kati ya wanasiasa vitaendelea weekendi nzima na huenda makubaliano yakafikiwa dakika ya mwisho, na hatimaye kuwatuliza raia na masoko.










Kadi ya kupimia damu yavumbuliwa







Kibanzi kinaweza kupima virusi vya ukimwi

Utafiti mmoja wa kisayansi umesema, chombo ambacho ni rahisi kubebeka na chenye bei nafuu cha kupimia damu kinaweza kuleta mafanikio mapya katika kubaini ugonjwa hasa katika maeneo ya vijijini.

Kulingana na utafiti uliofanywa na jarida la Nature Medicine, chombo hicho kiitwacho mChip kina ukubwa wa kadi ya benki na huweza kutambua maradhi katika kipindi cha dakika chache tu.

Upimaji wa sampuli za awali za maradhi kama ukimwi na kaswende nchini Rwanda zilionyesha takriban asilimia 100 kuwa sahihi.

Kifaa hicho kilichotengenezwa Marekani kitagharibu dola moja ya kimarekani.

Gharama yake ni ndogo zaidi ukilinganisha na upimaji unaofanyika kwenye maabara ambao ndio unaotumika kwa sasa.

Kibanzi au chip hiyo ina maeneo 10 ya kutambua, na kinaweza kupima ugonjwa zaidi ya moja kwa damu kidogo tu inayotokana kwa kujichoma na sindano ndogo.

Majibu yanaweza kuonekana kwa macho tu au kwa chombo cha kutambua chenye bei nafuu.

Samuel Sia, Profesa kutoka chuo kikuu cha Columbia ambaye ndiye kiongozi wa uundwaji wa kibanzi hicho alisema, " Wazo kuu lilikuwa ni kuweza kupima maradhi mengi na iweze kuwafikia wagonjwa popote duniani, badala ya kuwalazimisha kwenda kwenye zahanati kutoa damu na kusuburi majibu kwa siku kadhaa."

Upimaji mwingi uliofanywa kwa sampuli za awali za kifaa hicho zilifanyika mjini Kigali, Rwanda.

Zilionyesha kuwa sahihi kwa asilimia 95 baada ya kupimwa kwa virusi vya ukimwi na sahihi kwa asilimia 76 baada ya kupima kaswende.

Watafiti wana matumaini ya kutumia mChip kujaribu kuongeza uwezekano wa kupima maradhi yanayoambukizwa kwa njia ya kujamiiana kwa wajawazito, hasa barani Afrika.

Aina nyingine ya kibanzi hicho nacho kimeundwa kupima saratani ya kibofu.










Jeshi la Syria linashambulia Hamah








Jeshi la Syria limeshambulia kwa mizinga sehemu za mji wa Hamah, baada ya kuuzingira kwa miezi kadha.
Jeshi la Syria

Kwa mujibu wa wakaazi wa Hamah, watu kama 10 wameuwawa.

Taarifa nyengine zinasema waliouwawa ni kama 20.

Mji ambao umekuwa na maandamano makubwa zaidi nchini Syria sasa unashambuliwa.

Jeshi limeuzingira mji wa Hamah kwa miezi sasa, na leo alfajiri lilianza kuushambulia kwa mizinga.

Mkaazi mmoja wa Hamah anasema habari wanazopata kutoka hospitali ni kuwa watu wengi wameuwawa na kujeruhiwa.

Jeshi lilishambulia kutoka sehemu kadha, lakini kuna ripoti kuwa vifaru kama 16 vimeungana na upinzani.

Wanajiji walisherehekea hayo, lakini piya kuna khofu kuwa huo pengine ni mtego ili kuruhusu vifaru zaidi kuingizwa.

Inaonekana kuwa serikali inauogopa mji wa Hamah, kwa sababu ya mashambulio yaliyofanywa huko miaka ya '80, ambapo watu kama elfu 10 waliuliwa na jeshi la Rais Hafidh Assad, baba yake rais wa sasa.

Shambulio la leo linaonekana kama ujumbe kutoka kwa serikali, kuwa haitovumilia maandamano makubwa, hasa kabla ya mwezi wa Ramadan ambapo maandamano yanatarajiwa kuwa makubwa zaidi.

Lakini watu wametoka mabarabarani wakipiga kelele kuwa hawatokubali mauaji tena.









At least 95 people have been killed


At least 95 people have been killed after the army launched an attack on the flashpoint protest city of Hama in central Syria, a human rights activist has said.
A view shows the smoke rising in the city of Hama in this still image taken from video on Sunday.




A view shows the smoke rising in the city of Hama in this still image taken from video on Sunday. REUTERS photo

At least 95 people were killed on Sunday when the military launched an attack on the flashpoint protest city of Hama in central Syria, a human rights activist said.


Ammar Qorabi, who heads the National Organisation for Human Rights, reported the toll and also said army attacks across the country on Sunday killed at least 121 people and wounded dozens more.

Earlier, Rami Abdel Rahman of the Britain-based Syrian Observatory for Human Rights reported a death toll in Hama of 45, but said that number could rise because of the number of seriously wounded and a lack of medical supplies.

"The army and security forces entered Hama this morning and opened fire on civilians, killing 45 and wounding several more," Rami Abdel Rahman of the Britain-based Syrian Observatory for Human Rights said by telephone.

One Hama resident reached by phone told AFP that the army entered the city at around 6:00 am (0300 GMT).

Another said: "Five tanks are now deployed outside the governor's palace," and spoke of intermittent gunfire, while a third resident reported seeing four BTR-type armoured personnel carriers.

Elsewhere, "six people were killed and 50 wounded by security forces in the eastern city of Deir Ezzor and three were killed and dozens wounded at Harak in the southern Deraa region," Abdel Rahman said.

The oil hub of Deir Ezzor and Hama have been rallying points for pro-democracy protests since mid-March, while Hama has a bloody past.

In 1982, an estimated 20,000 people were killed in Hama when the army put down an Islamist revolt against the rule of President Bashar al-Assad's late father, Hafez.

The president replaced the governor of Hama after a record 500,000 protesters rallied in the opposition bastion on July 1 calling for the fall of the regime.

Activists said at the time it was the single largest demonstration of its kind since the pro-democracy movement erupted on March 15.

Since security forces gunned down 48 protesters in the city on June 3, Hama has escaped the clutches of the regime, activists say. The next day, more than 100,000 mourners were reported to have taken part in their funerals.

On Saturday, Abdel Rahman said troops shot dead three people who stoned a military convoy heading to quell growing anti-regime dissent in Deir Ezzor.

He said about 60 military vehicles including tanks, personnel carriers and trucks crammed with soldiers deployed in the city.

"The troops opened fire to frighten residents after reaching the governor's office," he said, quoting witnesses.

There were mounting fears the army was preparing to crack down on Deir Ezzor, increasingly at the forefront of anti-regime protests.

A man identifying himself as a Syrian army colonel told AFP in Nicosia that he had defected and has "hundreds" of troops under his command ready to confront the regular army in Deir Ezzor.

Riad al-Asaad warned the authorities against carrying out any operation in Deir Ezzor.

"I warn the Syrian authorities that I will send my troops to fight with the (regular) army if they do not stop the operations in Deir Ezzor," Asaad said.

"I am the commander of the Syrian Free Army," he said, adding that he commanded "hundreds" of troops and was calling from inside Syria "near the Turkish border."

His claim could not be independently verified.

Deir Ezzor, the main oil- and gas-producing region in Syria, which produces 380,000 barrels of oil per day, has seen almost daily demonstrations against the regime.

Meanwhile an opposition figure who declined to be named told AFP that 15 conscripts broke ranks from the troops who entered the central city of Homs on Saturday and fled.

"They have sought protection with residents," the source said.

On Friday, at least three people were killed in Deir Ezzor when security forces opened fire on 300,000 mourners at the funerals of three people killed the previous day, according to activists.

A total of 20 people were killed and 35 wounded on Friday across Syria as hundreds of thousands of demonstrators held anti-regime protests, rights groups said.

Syrian opposition figures meeting in Algeria on Saturday spoke out against any foreign intervention as the bloody crackdown continued.

"We refuse all foreign intervention, we refuse to carry weapons," said Adnane el-Bouch, a Syrian lawyer living in Algeria, during a meeting of a Syrian support committee at Amnesty International premises.

"It's a peaceful revolution... our weapons are cameras and mobile phones."

Since anti-regime protests broke out, the crackdown on dissent has resulted in the deaths of more than 1,500 civilians and more than 360 members of the security forces, according to a Syrian Observatory toll.

More than 12,000 people are also reported to have been arrested in the crackdown, and thousands of others have fled the country, rights groups say.










Soko kuu lateketea Kampala







Moto Kampala

Wachuuzi kama elfu kumi katika soko kuu la Owino mjini Kampala, wamepoteza mali zao zilizoteketea kwenye moto uliotokea Jumapili alfajiri.

Hii ni mara ya pili moto kutokea hapo katika kipindi cha miaka miwili.

Polisi walisema wanachunguza tukio hilo.

Salim Uhuru diwani wa mtaa huo alisema "hii ni mara ya pili soko limeshika moto. Ripoti ya polisi ya kwanza bado haijatoka na sasa moto umetokea mara ya pili. Hatujui kama moto umetokana na stima, au walichoma au jambo la kawaida. Hatujui."

"Lakini tunaomba wachuuzi warudi sokoni kwa sababu habari tulizopata ni kuwa watu wameshanunua ardhi hii. Na wakinunua ardhi hii, kutufukuza wanachochoma vitu vya watu," aliongeza.

"Lakini sisi kama madiwani wa eneo hili, tumewaambia wachuuzi warudi katika maduka yao. Hakuna mtu aliyewahi kuokoa mali yake. Yote imeungua."











Umoja wa Afrika kujadili Somalia








Somalia ukame

Umoja wa Afrika umetangaza kuwa utafanya mkutano wa viongozi ili kuchanga msaada kwa watu wa Somalia walioathirika na ukame.

Taarifa hiyo imetolewa baada ya malamiko kadha katika vyombo vya habari vya Afrika, kwamba viongozi wa Afrika wameshindwa kuwasaidia Wasomali wanaokabili njaa.

Makamo Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika, Bwana Mwencha alitoa tangazo la mkutano, wakati akizuru kikosi cha usalama cha umoja huo mjini Mogadishu.

Umoja wa Mataifa unasema watu milioni 12 wanahitaji msaada wa haraka katika eneo hilo.









Boko Haram kuzungumza na serikali Nigeria











Serikali ya Nigeria imetangaza kwamba inataraji kufanya mazungumzo na kikundi cha waislamu wenye siasa kali, cha Boko Haram.

Kamati imeteuliwa kuchunguza mtafaruku katika eneo la kaskazini-mashariki mwa nchi, baada ya watu kadha kuuwawa katika mapambano ya karibuni baina ya Boko Haram na jeshi.

Kamati hiyo ya wajumbe 10 imepewa kama wiki mbili kutoa mapendekezo.

Kamati imeagizwa kutazama swala la usalama katika eneo la ghasia la kaskazini-mashariki, na kuanza mazungumzo na kikundi cha Boko Haram, cha Waislamu wa msimamo mkali.

Hivi karibuni wapiganaji wa kikundi hicho, wamefanya mashambulio kadha, hasa dhidi ya askari wa usalama.

Wanajeshi wamezidishwa huko, na wengine wamelipiza kisasi, na wakati mwengine kuuwa raia.

Rais wa Nigeria, Goodluck Jonathan, anapenda kusema kuwa sera yake ni kuuma na kupuliza.

Lakini hadi sasa kuuma sana kumezidi kuharibu mambo; huku maelfu wamelihama eneo.

Mfano ambao rais anataka kujaribu tena ni ule uliotumiwa katika eneo la Niger Delta; ambako baada msamaha wa serikali, pamoja na fidia kubwa kwa wapiganaji, eneo hilo sasa ni shuwari.

Hadi sasa, Boko Haram hawakuonesha ishara kuwa wanataka kuzungumza.

Siku za nyuma walishikilia kuwa jeshi lazima liondoke kwanza, kabla ya mazungumzo kuanza.










INTERVIEW OF BOKO HARAM SUPREME LEADER USTAZ MOHAMMED YUSUF
Boko Haram is an Islamic radical and militant group operating in North and Central Nigeria, on the demographic border region between the Muslims in Nigeria, living mainly in Northern Nigeria and the Christian inhabiting mainly the South of the country. The term "Boko Haram" comes from the Hausa word BOKO meaning "Western or non-Islamic education" and the Arabic word HARAM meaning "sin".
Boko Haram was founded in 2002 in Maiduguri, central Nigeria, by Ustaz Mohammed Yusuf. In 2004 it moved to Kanamma, Yobe State of Nigeria, on the far North-East in the edge of the Sahara desert on the border with Niger where other Islamic militant groups like MAGHREB al-Qaeda are operating too. In Kanamma Boko Haram set up a base called "Afghanistan", used to attack nearby police outposts, killing police officers. Ustaz Mohammed Yusuf is hostile to democracy and the secular education system, vowing that "this war that is yet to start would continue for long" if the political and educational system was not changed. Ustaz Mohammed Yusuf himself was killed by Nigerian troops on 07/31/2009 (see - Bauchi 07.26.09).
Boko Haram includes members who come from neighboring Chad and speak only in Arabic and not one of the Local Nigerian languages to demonstrate their loyalty to the Islamic Kuraan. In a 2009 BBC interview, Yusuf stated that the belief that the world is a sphere contrary to Islam and should be rejected, along with Darainism and the theory that rain comes from water evaporated by the sun.

Incase you missed the interview of Boko Haram SUPREME LEADER USTAZ MOHAMMED YUSUF during interrogation by Nigeria's SSS(State Security Service) here is a transcript of the interview.








Bahrami amsamehe aliyempofua





Ameneh Bahrami



Mwanamke wa Iran ambaye alipofoka aliposhambuliwa kwa tindi kali, amemsamehe mwanamme aliyemshambulia, saa chache tu kabla ya mfungwa huyo akitarajiwa naye kupofolewa, kama adhabu yake.

Majid Movahedi alikutikana na makosa ya kumrushia tindi kali usoni Ameneh Bahrami, baada ya bibi huyo kukataa posa yake mara kadha.

Baada ya hukumu kutolewa, Ameneh Bahrami alisema yeye mwenyewe atamimina tindi kali kwenye macho ya Bwana Movahed.

Mashirika ya kupigania haki za kibinaadamu yalilalamika juu ya hukumu hiyo.

Bi Bahrami sasa ameliambia shirika la habari la Iran, kwamba, ingawa Mungu anataja adhabu ya malipo, lakini piya anasema kuwa kumsamehe mkosa ni muhimu zaidi.

Bi Bahrami anadai fidia kwa majaraha yake.












Man United yailaza Barcelona 2-1




Bao la ushindi alilofunga Michael Owen dakika ya 76 liliiwezesha Manchester United kuwalaza mabingwa soka wa bara la Ulaya Barcelona 2-1 katika mchezo wa kirafiki wa kujiandaa kwa patashika za Ligi Kuu, uliofanyika mjini Washington DC.


Michael Owen baada ya kufunga bao la ushindi

Mbele ya mashabiki karibu 82,000, Nani alitangulia kuipatia Manchester United bao la kuongoza katika dakika ya 22.

Barcelona, ikicheza bila ya Lionel Messi, ilisawazisha katika dakika ya 70 kwa mkwaju wa Thiago Alcantara.

Owen alimiminiwa pande la Tom Cleverley na kupachika bao la ushindi wakati United wakikamilisha ziara ya Amerika Kaskazini na kushinda mechi zake zote tano ilizocheza.

Owen aliandika katika mtandao wa kijamii wa tweeter baada ya mchezo huo: "Kama ilivyo kawaida ya Barca, upande wa upinzani unapata shida sana kumiliki mpira! Na ndivyo ilivyokuwa katika mchezo wa leo! Nashukuru nimefanikiwa kufunga bao."

United walifungwa na Barcelona katika fainali ya Kombe la Ubingwa wa Ulaya katika uwanja wa Wembley mwezi wa Mei, ilionekana mabingwa hao wa soka wa England wakipata nafasi ndogo ya kulipiza kisasi.

Kikosi hicho cha Sir Alex Ferguson kitarejea nyumbani kujiandaa kwa mchezo wa kuwania Ngao ya Jumuia dhidi ya washindi wa Kombe la FA, Manchester City siku ya Jumapili ijayo katika uwanja wa Wembley.

Meneja msaidizi wa Manchester United Mike Phelan alisema: "Mechi ya usiku huu haikuwa ya kuwania kitu chochote. Ilikuwa muhimu kwamba wachezaji tuliowapanga walikuwa wanaelewa nini kinachohitajika unapopambana na timu bora duniani.

Pamoja na Messi kutocheza, Barcelona iliamua kutomchezesha Xavi, Carlos Puyol na Gerard Pique katika kikosi chao kilichoanza.








Watu 11 wauwawa katika ghasia Uchina






Xinjiang China





Vyombo vya habari vya Uchina vinasema kuwa watu 11 wameuwawa katika kisa cha pili cha ghasia katika majuma mawili, kwenye jimbo la magharibi la Xinjiang.

Shirika la habari la taifa, Xinhua, lilisema watu wanane walikufa jana usiku katika mji wa Kashgar, wakati wanaume wawili walipoliteka lori na kuwapiga visu wapita njia.

Kabla ya shambulio hilo, kulitokea miripuko miwili.

Xinhua imeripoti kuwa leo piya kulitokea mripuko mwengine, uliouwa watu watatu.

Kulitokea ghasia za kikabila katika jimbo la Xinjiang, miaka miwili iliyopita, kati ya watu wa kabila la Uighur, ambao ni Waislamu, na ni wachache, na wanachukia utawala wa Beijing.

Wa-Uighur wanaoishi uhamishoni, wanasema kulikuwa na amri ya kafyu huko Kashgar, na watu kama mia-moja wamekamatwa.












Kasumba inapitia Afrika Mashariki







Ripoti ya Umoja wa Mataifa inasema kuwa wanaofanya magendo ya mihadarati Afrika sasa wanapitia Afrika Mashariki,
kwa sababu ya vikwazo vingi Asia na Mashariki ya Kati, na hivo kuleta uvunjaji wa sheria na matumizi zaidi ya mihadarati katika eneo hilo la Afrika Mashariki.

Inakisiwa kuwa biashara ya mihadarati ilifika dola bilioni 68 dunia nzima, katika mwaka wa 2009.

Ofisi ya Kupambana na Mihadarati na Uhalifu ya Umoja wa Mataifa, inasema ina wasiwasi kuwa Afrika Mashariki imekuwa njia inayotumiwa na wafanya magendo, kwa sababu kanda hiyo haina uwezo wa kupambana na magendo na uraibu wa mihadarati.

Inasema madawa ya kulevya na idadi ya walanguzi waliokamatwa, inaonesha kuwa wafanya magendo hayo, hasa magengi kutoka Afrika Magharibi, wanazidi kusafirisha kasumba kutoka Afghanistan na Pakistan kupitia Afrika Mashariki, kisha kupeleka Ulaya na kwengineko.

Afghanistan ndio mzalishaji mkubwa kabisa wa kasumba, na asilimia 40 hupitishwa Pakistan, kabla ya kuelekezwa kwengineko.

Ripoti hiyo ya Umoja wa Mataifa inasema katika miezi mitatu ya mwanzo ya mwaka huu, shehena mbili za kasumba, kila moja zaidi ya kilo mia moja, zimeripotiwa Kenya na Tanzania.

Inaeleza kuwa sababu ya magendo hayo kuzidi ni rushwa, umaskini na uwezo haba wa idara za kuweka sheria