KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Saturday, June 18, 2011

Frederick Chiluba amefariki



Rais wa zamani wa Zambia, Frederick Chiluba, amefariki, akiwa na umri wa miaka 68.

Bwana Chiluba amekuwa na ugonjwa moyo kwa miaka kadha.



Rais Chiluba aliiongoza Zambia kwa mwongo mzima katika miaka ya '90, na baada ya kustaafu alishtakiwa kwa sababu ya rushwa.

Frederick Chiluba alipata urais wa Zambia mwaka wa 1991, wakati Afrika inaanza kuingiia katika demokrasi ya vyama vingi.

Kabla ya hapo alikuwa kiongozi wa wafanyakazi.

Aliahidi kuleta mabadiliko lakini alipochukua uongozi Zambia ilikuwa imeshafilisika, naye aliacha rushwa kustawi.

Alipojaribu kujiongezea muhula wa tatu wa madaraka, alipingwa.

Piya alilaumiwa kuwa akipenda maisha ya anasa.

Baada ya kuondoka madarakani mwaka wa 2001, mrithi wake, Levy Mwanawasa, alimshtaki kwa shutuma za rushwa.

Baada ya kesi ya miaka 6 kuhusu ubadhirifu wa mali ya taifa, Frederick Chiluba aliambiwa hakuwa na makosa. .

Lakini katika kesi nyengine iliyofanywa katika mahakama makuu ya London, Chiluba alikutikana na hatia ya kuiba mamilioni ya dola ya fedha za serikali ya Zambia, kwa kutumia akaunti kwenye mabenki ya London.









Marekani inazungumza na Taliban






Nchini Afghanistan Rais Karzai amethibitisha kuwa Marekani na mataifa mengine yanafanya mazungumzo ya awali na Taliban.







Watu walikisia kuwa Marekani ina mawasiliano na Taliban.

Lakini hilo ndio kwanza kuthibitishwa na kiongozi.

Rais Karzai amesema mazungumzo yanafanywa na Taliban, na kwamba jeshi la mataifa ya nje, hasa Marekani yenyewe, linafanya majadiliano.

Haijulikani nani wanaiwakilisha Marekani, na kama wanazungumza ana kwa ana na Taliban, au kuna mtu kati.

Kinachozungumzwa piya hakijulikani.

Msimamo rasmi wa Taliban ni kuwa majeshi ya kimataifa lazima kwanza yaondoke nchini kabla ya kujadili amani, na itazungumza na serikali ya Afghanistan tu.

Hayo hayalingani na yale aliyosema Rais Karzai.

Haifai kutaraji suluhu ya haraka kutokana na mawasiliano ya hivi sasa.

Utabiri wa pande zote, Nato, serikali ya Afghanistan na Taliban yenyewe, ni kuwa mapigano makali yataendelea kiangazi cha mwaka huu, na pengine miaka kadha ijayo.











Makanisa ya Sudan yanalaani mapigano





Baraza la makanisa ya Sudan linasema lina wasiwasi mkubwa juu ya mauaji makubwa ya raia katika majimbo ya Abyei na Kordofan Kusini.




Katika taarifa yake, baraza hilo linasema watu wameuwawa bila ya kufikishwa mahakamani.

Majimbo hayo kwenye mpaka baina ya Sudan Kusini na Kaskazini, hivi karibuni yamekumbwa na mapigano baina ya jeshi la kaskazini, la kusini na makundi mengine.

Makanisa yameulaumu Umoja wa Mataifa kwa kushindwa kuwalinda raia, na yamezilaani serikali za kaskazini na kusini Sudan, kwa kutumia nguvu kutatua hitilafu baina yao.








Mfalme anapendekeza mabadiliko Morocco








Viongozi wa wanaharakati wanaotaka mabadiliko nchini Morocco wanapanga kufanya maandamano Jumapili, ingawa Mfalme Mohammed ametangaza mabadiliko ya katiba.

Mfalme wa Morocco alisema mabadiliko anayopendekeza yatapunguza madaraka yake na kuzidisha nguvu za waziri mkuu na bunge.

Wadadisi wanataka katiba mpya iandikwe na kamati itayochaguliwa siyo wajumbe wataoteuliwa na mfalme.

Watu wengine wameyakaribisha mapendekezo hayo, na maelfu ya wananchi walitoka mababarani baada ya hotuba ya mfalme Ijumaa usiku, wakipepea bendera na kupiga honi za magari.










Obama atetea hatua ya kutuma jeshi Libya






Rais Barack Obama hahitaji idhini ya bunge la congress kuwatuma wanajeshi wa Marekani kuhusika katika operesheni za Nato nchini Libya.


White House inasema wanajeshi wa Marekani wanahusika katika majukumu madogo sana nchini Libya
Kulingana na maelezo ya ikulu ya White House, Rais Obama ana uhuru kutuma wanajeshi hao kama kiongozi wa taifa.


Lakini kulingana na sheria iliotungwa wakati wa vita vya Vietnam, rais wa Marekani lazima apate idhini ya bunge la congress kutuma wanajeshi kuhudumu katika nchi ya kigeni ikiwa muda huo utachukua zaidi siku sitini.

Wabunge nchini Marekani wanasema Rais Obama amekiuka sheria hio kwa kuwa muda wa siku sitini ulikwisha mwezi May 20.

Lakini White House imewasilisha taarifa katika bunge hilo, ikielezea kuwa jukumu la wanajeshi wa Marekani ni la kusaidia tu kikosi cha Nato.

White House imesema majukumu ya jeshi la Marekani nchini Libya sasa hivi hayajafikia kiwango ambacho kimewekwa kwenye sheria hiyo ya mwaka wa 1973 ambapo rais atalazimika kuomba idhini ya congress.

Wanjeshi wa Marekani wanasaidia kuongeza ndege za Nato mafuta na katika shughuli za kijasusi nchini Libya, kulingana na maelezo ya White House.

Taarifa hiyo imesisitiza kuwa wanajeshi wa Marekani hawapo kwenye makabiliano na jeshi la Libya, kwa hivyo hawako vitani.

Kulingana na katiba ya Marekani, bunge la congress ndio lenye uwezo wa kutangaza vita.

Ifikiapo jumapili wiki hii, Marekani itakuwa imehusika kwenye harakati hizo za Nato nchini Libya kwa jumla ya siku tisini.







Juhudi zaidi kupambana na Ukimwi-UN






Mpango wa Umoja wa Mataifa kuhusu ukimwi (UNAID)unasema kuwa takriban watu milioni sita na nusu katika mataifa machanga wanatumia tiba dhidi ya Ukimwi likifahamu kwamba wapo wengine milioni tisa wanaohitaji dawa bila ya kuwa na uwezo wa kupata dao hiyo.




kuepuka gharama baadaye



Suala la tiba limezuka kuwa suala nyeti tangu majaribio ya mwezi uliopita kuonyesha kuwa unapotumia dawa mapema inasaidia na vilevile kuna uwezekano wa kutoambukiza wengine.


Tiba ni muhimu



Shirika hilo linakadiria hadi watu milioni 34 wanaishi na virusi huku ni watu milioni 30 waliofariki tangu maradhi haya yagunduliwe tareh 5 juni mwaka 1981.

Ingawa kiwango cha maambukizi kinashuka, mpango wa Umoja wa Mataifa una wasiwasi juu ya kupunguwa kwa uwekezaji katika kupambana na janga la ukimwi tangu mwaka jana.

Shirika hilo limeonya kua endapo hali hiyo itaendelea hivyo basi gharama zinazotokana na maradhi hayo zitakuwa kubwa zaidi baadaye.

Onyo hili linatokea wakati viongozi wa serikali mbalimbali wanajiandaa kwa mkutano wa kujadili ukimwi wiki ijayo mjini New York.











Wagombea mtoto baada ya kupeana talaka





WALIOKUWA wanandoa kwa muda wa miaka minne mfululizo wamejikuta wakihatarisha maisha ya mtoto wao kwa kumjeruhi kwa kumgombani kama mpira wa kona huku kila mmoja akihitaji kubaki na mtoto huyo baada ya kutalakiana
Sakata hilo la kugombea mtoto lilitokea juzi maeneo ya Tabata Kimanga ambapo watalaka hao walikuwa wakigombani mtoto wa kiume aliyekuwa na umri wa miaka mitatu

Hali hiyo ilizuka tu mwanaume huyo anayefahamika kwa jina la Muhsin [36] kumpa talaka mke wake aliyefahamika kwa jina moja la Feti [28]

Sakata la kugombani mtoto huyo lilizuka wakati mwanamke huyo alipofika nyumbani kwake hapo kuchukua kilichochake akiwa na jopo la wasindikizaji ili aweze kupisha maisha mapya ya mume wake huyo

Hali ilibadilika baada ya mke huyo kuandaa nguo za mtoto huyo ili aweze kuondoka nae anakoenda na ndipo aliamsha mashetani yaliyolala ya mwanaume huyo na kumtaka amuache mtoto huyo hali iliyofanya mwanamke huyo apinge na kutaka kukimbia nae ndipo walipoanza kugombania motto kila mmoja akivuta mkono wake na kumuweka mtoto huyo katika kipindi kigumu ambapo mtoto huyo alikuwa katika hali mbaya ya kuvutwa kati ya wazazi wake hao wawili

Hali hiyo ilifanya majirani waishio karibu na nyumba hiyo kuingilia kati hata hivyo haikusaidia kitu huku kila mmoja akihitaji kuishi na mtoto huyo

Hata hivyo mwanaume huyo hakukubaliana na hali hiyo hali iliyofanya akaripoti kwa Mwenyekiti waSerikali za mtaa anapoishi na kupigia simu baadhi ya wazee wa familia wa pande zote mbili ili aweze kupata msaada juu ya sakata hilo

Imedaiwa mwanaume huyo alikuwa anagoma mtoto huyo asiondoke kwa kuwa mwanamke huyo alishatangaza kuondoka nchini hali iliyofanya mwanaume huyo kugoma mtoto huyo kuondoka na mama yake huyo
Hadi nifahamsihe inaondoka maeneno hayo majira ya saa 10 jioni iloiacha wanandoa hao wakiwa katika hali ya ututa huku kila mmoja akihitaji kuishi karibu na mtoto huyo








Dar yakithiri kwa uchafu wa mazingira




MKOA wa Dar es Salaam umekubuhu kwa uchafuzi wa mazingira hali iliyofanya wakazi waishio humo kushangaa kuitwa jiji kutokana na kero za uchafuzi wa mazingira ambao ungeweza kuzuilika kukua siku hadi siku


Dar es Salaam imekuwa iko shagala bagala katika mitaa yake ya jiji hali inayofanya kukosa hadhi ya kuitwa jiji kutokana na mazingira yake hayaridhishi machoni mwa watu


Mazingira yamekuwa hovyo kwa baadhi ya mitaa ya jiji kwa kuonekana kwa baadhi ya wakazi kushindwa kudumisha suala la usafi wa mazingira wanayowazunguka.

Jiji hilo hali huwa mbaya zaidi hasa pindi mvua zinaponyesha na wakazi hao kuacha uchafu wa vyooni, mitaro kutirrika barabarani hali inayofanya uchafunzi wa mazingira uzidi kuongezeka.
Mamlaka husika wa afya na usafi wa jiji pia wameonekana kuchangia kwa asilimia kubwa uchafuzi huo wka kushindwa kutekeleza majukumu yao ipasavyo


Hivi sasa wafanyabiashara ndogondogo wamekuwa wakijiendeshea shughuli zao mahali popote wanapojisikia na sehemu ambazo si rasmi na kufanya kuacha taka ngumu katika maeneo ya jiji na mamlaka husika kufumbia macho suala hilo na inasikitisha majalala ya kutupia taka yakiwa katikati ya barabara, kati ya nyumba na nyumba hali inayofanya uchafuzi wa mazingira na ili hali mamlaka hizo kutumia mamilioni ya fedha za walipa kodi kushughulikia taka hizo hizo









Gen.Nyamwasa atishiwa kufukuzwa





Mashirika yanayopigania haki za binadamu nchini Afrika ya kusini yamechukuwa hatua za kisheria kuitaka serikali ya nchi hiyo ibadili hadhi ya ukimbizi aliyopewa mkuu wa zamani wa majeshi ya Rwanda.



Lt.Gen Kayumba Nyamwasa na Rais Kagame kulia


Wamesema kuwa serikali ilichukuwa hatua ya haraka kumpa hifadhi Luteni Generali Faustin Kayumba Nyamwasa il hali alishirikiana na Rais Paul Kagame katika kukomesha mauwaji ya kimbari ya mwaka 1994 nchini Rwanda.

Lakini akakimbilia nchini Afrika ya kusini mwaka jana baada ya kukorofishana na Bw.Paul Kagame.

Yeye anatakikana na Uhispania pamoja na Ufaransa kwa madai ya mchango wake katika mauwaji ya kimbari ya siku 100.

Baada ya kukimbilia Afrika ya kusini aliponea chupuchupu jaribio la kumua.Serikali ya Rwanda ilikanusha madai ya kwamba ilihusika katika jaribio hilo.

Afrika ya kusini ilimwitisha balozi wake aliyekueko mjini Kigali baada ya tukio hilo.

Hukumu akiwa uhamishoni

Uhispania na Ufaransa zinamsaka Lt Gen Nyamwasa

, kwa tuhuma za kuongoza mauwaji ya Rais wa zamani wa nchi hiyo Juvenal Habyarimana, tukio lililoanzisha mauwaji ya kimbari.



Shirika lijulikanalo kama 'The Southern Africa Litigation Centre and the Consortium for Refugees and Migrant Rights' limesema kuwa haikubaliki kwa Afrika ya kusini kuruhusu mtu wa aina hiyo kupewa hadhi ya ukimbizi akiwa anashukiwa kushiriki vitendo vinavyokiuka haki za binadamu.

"sheria ya ukimbizi ina lengo la kuwalinda wanyonge, na siyo wale waliosababisha uonevu na kusababisha wengi kuingia katika hali kama hiyo, alisema Allan Wallis, wakili kwenye kituo cha Afrika kusini (The Southern Africa Litigation Centre.)

Serikali ya Rwanda nayo imekuwa ikiipa msukumo Afrika ya kusini imrejeshe Rwanda Lt Gen Nyamwasa atumikie kifungo gerezani cha miaka 24 kufuatia mahakama ya kijeshji kusikiliza na kumhukumu mnamo mwezi januari kwa tuhuma za kutishia usalama wa taifa, kukimbia jeshini bila ruhusa na uchafuzi wa jina la taifa.



Watu 800,000 waliuawa


Takriban watu wa kabila la Watutsi 800,000 pamoja na Wahutu wenye msimamo wa wastani waliuawa katika mauwaji hayo ya kimbari.


Bw.Kagame aliongoza vuguvugu la RPF ambalo lilikomesha mauwaji mnano mwaka 2000 na tangu hapo amekuwa ndiyo Rais wa nchi.


Baada ya mauwaji, aliahidi kuleta amani na utawala wa demokrasia lakini wakosoaji wanasema anaongoza utawala wa ki-imla.







Ngozi ya chura kuponya saratani




Wataalamu kutoka Chuo Kikuu cha Belfast wamejishindia tuzo kwa kazi waliyoifanya kuhusiana na ngozi ya chura

ambayo wamegundua inaweza kutibu zaidi ya maradhi makuu 70.


kupoza saratani


Watafiti hao walipokea tuzo yao kwenye sherehe iliyoandaliwa na Tuzo ya ubunifu kutoka taasisi ijulikanayo kama Medical Futures Innovation mjini London.

Wataalamu hao wakiongozwa na Profesa Chris Shaw wa taasisi ya Famacia ya Queens, wamegundua proteni mbili ambazo zinaweza kurekebisha kukuwa kwa mishipa ya damu.

Waligundua kuwa proteni kutoka aina ya chura ajulikanaye kwa jina la kitaalamu 'waxy monkey frog' hubana kukuwa kwa mishipa inayosambaza damu mwilini na inaweza kutumiwa kuua uvimbe unaotokana na saratani.

Profesa Shaw alisema kuwa mara nyingi uvimbe huo huweza kuchochewa kufikia kiwango fulani kabla ya kuhitaji damu zaidi ili kupevuka kuwa kivimbe ambacho husaidia kupitisha hewa ya oksijeni na lishe.

Kwa hiyo akaongezea kusema '' Ili kusitisha kukuwa kwa mishipa hii isikuwe hadi kuvimba kutafanya saratani isienee na hatimaye kuiondoa mwilini kabisa.

Hili lina uwezekano mkubwa wa kuifanya saratani yawe maradhi yasiyo uwa ila ya kuishi nayo.

Kundi hilo liligundua pia kuwa aina ya chura mkubwa ajulikanaye kama ''firebellied toad'' huzalisha proteni inayoweza kuchagiza mishipa kukuwa na inaweza kusaidia katika kutibu majeraha ya mgonjwa yapone kwa haraka zaidi.







Kevin Nolan ajiunga na West Ham







Nahodha wa Newcastle United, Kevin Nolan, amekamilisha utaratibu unaostahili na kujiunga na West Ham, ambako amepata mkataba wa miaka mitano.



Amepata mkataba kuichezea West Ham iliyoshuka daraja
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28, na aliyecheza chini ya meneja Sam Allardyce katika klabu ya Bolton, amejiunga na klabu hiyo ya ligi ya Championship pasipo kujulikano kwa kiwango gani cha fedha.

"Kupata nafasi ya kushirikiana tena na Sam kwa mara nyingine tena ni jambo kubwa kwangu," alielezea Nolan katika wavuti ya West Ham.

"West Ham wameonyesha juhudi katika kunitamani na kuwa na ari ya kuhakikisha nitawachezea."

Awali mashauri na Newcastle yalikwama kutokana na kutoafikiana Nolan atapata mkataba wa miaka mingapi.

"Ninafahamu klabu kilitoa ahadi nzuri kwa Kevin, lakini hawakuelewana kuhusiana na mkataba," meneja wa klabu ya Newcastle, maarufu kwa jina Magpies, Alan Pardew, alilieleza jarida la Shields Gazette.

"Ningelipenda kumshukuru Kevin kwa juhudi zake kama mchezaji na nahodha, tangu nilipochukua mamlaka msimu uliopita.

"Alionyesha kipawa cha uongozi, na ninamtakia kila la heri West Ham. Ni klabu nzuri, na ninahakika atastawi".

Nolan, ambaye anatazamiwa kuwa nahodha katika uwanja wa Upton Park, ametoa ahadi za kuwaridhisha mashabiki wote wa West Ham walionyesha uaminifu wao kwa kumpa mkataba wa miaka mitano.






Padri Asakwa, Adaiwa Kubaka





JESHI LA POLISI mkoani Morogoro linamsaka Padri wa Kanisa Katoliki Jimbo la Morogoro kwa tuhuma za kumbaka mwanafunzi wa kidato cha sita katika Shule ya Sekondari Alfa.


Taarifa hizo zilitolewa jana na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Adolphina Chialo

Chialo aliviambia vyombo vya habari kuwa, mwanafunzi huyo ambaye jina lake linahifadhiwa kwa sasa, aliripoti tukio hilo Mei 28, mwaka huu na kudai kufanyiwa unyama huo Machi 30 mwaka huu na Padri huyo akiwa jijini Dar es Salaam.

Chialo alisema kuwa maelezo ya mwanafunzi huyo yalisema Padri huyo alimwita mwanafunzi huyo aje jijini Dar es Salaam ili aweze kumpatie fedha za masomo ya ziada ikiwa ni utaratibu wake wa kumsaidia mara kwa mara kama yatima kutokana na mwanafunzi huyo kujitangaza kuomba misaada kwa wasamaria.

Alisema mwanafunzi huyo kuwa, Padri huyo alimpigia simu mwanafunzi huyo ya kumtaka kwenda jijini Dar es Salaam akachukue fedha za kumsaidia kimasomo na mwanafunzi huyo kudai hakuonyesha shaka kwa kuwa hakufikiria kama angefanyiwa hivyo na alifunga safari na kwenda huko.

Maelezo ya mwanafunzi huyo yalidai alipofika Dar es Salaam eneo la Manzese alipomuelekeza alianza kupatwa na mashaka pale Padri alipomtaka waingie chumbani na kumwambia hawezi kumpa fedha hizo hadharani.

Ilidaiwa alipofika chumbani mwanafunzi huyo Padri alifunga mlango kisha kumfanyia kitendo cha kumuingilia pasipo idhini yake na kumsihi asiseme tukio hilo kwa mtu yeyote.

Ndipo mwanafunzi huyo alitoa taarifa hiyo ili aweze kupatiwa msaada wa kisheria kwa kuwa alikuwa na wasiwasi na afya yake kwa kushindwa kuendelea kumsikiliza Padri huyo kwa maombi yake ya kumtaka asifichue tukio hilo popote kwani angelidhalilisha kanisa.








Maelfu ya watu wahama Kordofan Kusini




Mashirika ya misaada yazuiwa kuwasaidia walioathirika na vita
Zaidi ya watu elfu hamsini wamelazimika kuhama makaazi yao katika jimbo la kordofan kusini kufuatia mashambulizi ya anga kutoka jeshi la Sudan.


Shirika la wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR, limesema mashirika ya kutoa misaada ya kibinadamu pia yamezuia kuwasaidia watu walioathirika kufuatia mashambulizi hayo.

Msemaji wa Umoja wa Mataifa Fatoumata Lejeune-Kaba ameelezea kuwa makundi ya wapiganaji yameweka vizuizi barabarani na yanawazuia kupeleka misaada kwa watu waliohama makaazi yao.


Na Mkuu wa kanisa la Kianglikana, Askofu Rowan Williams amesema kuwa huenda hali katika jimbo la Kordofan Kusini ikazidi kuzorota sawa na hali ilivyo katika jimbo la Darfur.


Mzozo huo unaingia siku ya kumi sasa.

Inaripotiwa kuwa mapigano yamekuwa makali kati ya vikosi vya serikali na wanajeshi wa zamani wa jeshi la Kusini.

Sudan Kusini imebakisha siku kadhaa kabla nchi hiyo kubwa barani Afrika haijagawanywa.

Mwandishi wa BBC Peter Martell aliyeko mji mkuu Juba anasema ndege za jeshi la Sudan Kaskazini zimelipua eneo la kijeshi la anga lililoko Kauda katikati ya milima ya Nuba, kwenye makazi ya makundi yanayounga Sudan Kusini likiwaita waasi.

Umoja wa mataifa unaripoti kuwa milio mikubwa ya risasi iliweza kusikika huku mapigano yakisambaa katika jimbo la Kordonfan Kusini.

Kuna wasiwasi kuwa idadi ya watu waliokufa ikaongezeka, huku wafanyakazi wa misaada na viongozi wa dini katika eneo hilo wakisema kuwa wanaolengwa ni wale wanaoaminika kuipinga serikali ya Khartoum.

Watu wanachimba mahandaki wakiogopa mashambulizi zaidi.

Awali wafanyakazi wa misaada walisema mapigano yanazidi kuongezeka katika jimbo la Nuba, ambako ni makazi ya makabila ya waafrika ambao wana uhusiano zaidi na Sudan Kusini kuliko Kaskazini inayokaliwa na waarabu wengi.





Ugiriki yaweza kushindwa kulipa madeni


George Papandreou anasheherekea mwaka wake wa 59 kwa umri, na zawadi alioipokea ni kujiuzulu kwa manaibu wawili wa mawaziri katika chama cha kisoshalisti.



Waziri mkuu wa Ugiriki
Wakati waasi hao wakimuacha mkono, Rais Karolos Papoulias ametaka pawepo na uwajibikaji ili mgogoro wa uchumi usigeuzwe kuwa medani ya kisiasa.

Hali hiyo ya sintofahamu imemtia wasiwasi kamishena wa fedha wa Umoja wa Ulaya Olli Rehn ambaye azma yake ni kuona kwamba sarafu ya Euro haitoathiriwa na mgogoro wa hivi sasa.

Amezitaka serikali za umoja huo zipuuze tofauti zao wakati huu mgumu na zikubaliane juu ya fungu la kuiokoa Ugiriki kwa mara ya pili kufikia mwezi Julai.

Huu ni mwezi muhimu kwa Ugiriki ambayo ina pesa kidogo na itaishiwa mnamo mwezi huo ikiwa haitopokea kitita cha kwanza kama ilivyoahidiwa mnamo mwezi Mei mwaka 2010.

Friday, June 10, 2011

Malawi yazuwia ruzuku za wagonjwa wa HIV

Serikali ya Malawi imesimamisha kutoa ruzuku maalum kwa watumishi wa serikali wenye virusi vya HIV na UKIMWI kwa sababu inasema wanatumia fedha hizo kwa kunywa pombe na kuwapa makahaba.


mchango kwa wagonjwa wafujwa

Takriban watumishi wa serikali elfu 40 wamenufaika na mpango huo.

Serikali ya Malawi inawashtumu watumishi wa serikali nchini humo kwa kueneza zaidi virusi vya HIV na UKIMWI Kwa kutumia fedha hizo kujihusisha na vitendo vinavyohatarisha maisha.



Makahaba hupokea fedha za msaada

Kuanzia sasa kila mwezi watapokea posho ya chakula cha lishe bora badala ya kupokea fedha za ziada.

Afisa moja asema mpango huo umetumiliwa vibaya zaidi na watumishi wa serikali wanaojidai kua nao pia wamambukizwa na virusi vya HIV ili wajipatie fedha zaidi..Takriban asilimia 15 ya wakaazi wa Malawi wana virusi vya HIV,na idadi kubwa ya vifo kutokana na ugonjwa huo umepunguza kiwango cha maisha kufikia umri wa wastani wa miaka 36





Muafaka kuhusu serikali ya mpito Somalia





Wafuasi wa Waziri mkuu mjini Mogadishu

Waziri Mkuu Mohammed anatakiwa kujiuzulu chini ya siku 30

Viongozi wa Somalia wamekubaliana kusitisha uhasama wa kisiasa kati yao baada ya mzozo uliodumu miezi kadhaa.

Rais Sheikh Sharif Sheikh Ahmed na Spika wa Bunge Sheikh Sharif Aden wamekubaliana kuhairisha uchaguzi hadi mwezi Agosti mwaka ujao.

Utata huo wa viongozi umesababisha kuzorota kwa uhusiano kati ya serikali ya mpito na jumuiya ya kimataifa.

Jumuiya ya kimataifa ilikuwa inashinikiza uchaguzi ufanyike Agosti mwezi huu baada ya muhula wa serikali hii ya mpito kukamilika.

Viongozi hao wametia saini muafaka wa kusitsha usahama kati yao mjini Kampala Uganda kufuatia juhudi za upatanishi zilizoongozwa na mwenyeji wao Yoweri Museveni.

Kulingana na mkataba huo, Waziri Mkuu Mohammed Abdullahi Mohammed atatakiwa kujiuzulu chini ya siku thelathini baada ya kusainiwa mkataba huo. Rais Sharif atateuwa mtu mwengine kuchukua nafasi hiyo.

Hata hivyo hatua hiyo imepingwa vikali na wafuasi wa Waziri Mkuu Mohammed, ambao wamefanya maandamano makubwa mjini Mogadishu.

Waziri Mkuu Mohammed alikuwepo mjini Kampala lakini anasemekana kuwa amerudi nchini Somalia.

Kulingana na taarifa kutoka mwakilishi wa katibu mkuu wa umoja wa mataifa nchini Somalia, Balozi Augustine Mahiga, viongozi wa Afrika Mashariki chini ya shirika la maendeleo la IGAD, watasimamia mkataba huo kuhakikisha unatekelezwa.

Nchi za kigeni zinazofadhili mikakati ya amani nchini Somalia, mara kadhaa zimeelezea kero zao kuhusu uhasama wa mara kwa mara wa kisiasa kati ya viongozi nchini humo.

Tofauti hizo za kisiasa ambazo wadadisi wa siasa za Somalia wanasema zinachochewa na uchu wa madaraka, zinasemekana kuchangia uzembe wa jumuiya ya kimataifa wa kuisaidia nchi hiyo kujikwamua kutoka vita vilivyo dumu miaka ishirini.







Afrika Mashariki yakabiliwa na Njaa








Shirika moja la kimarekani limeonya kuwa janga kuu la uhaba wa chakula duniani linaendelea kubana mashariki mwa upembe wa Afrika.
Njaa



Uhaba wa chakula waathiri Afrika Mashariki

Shirika hilo lijulikanalo kama The Famine Early Warning Systems Network limeonya kuwa nchi zinazotia wasiwasi ni Ethiopia, Kenya na Somalia.


Limesema usaidizi mkubwa wa dharura unahitajika kuokoa maisha na kukabiliana na utapiamlo katika eneo hilo.

Shirika hilo pia limesisitiza kuwa usaidizi unaotolewa kwa sasa hautoshi.

Katika taarifa yake shirika hilo limesema kuwa eneo la upembe wa afrika limeathiriwa na upungufu wa mvua kwa misimu miwili hivyo kusababisha ukame mbaya zaidi tangu mwaka 1995







Uturuki haitawakataa wakimbizi wa Syria





Ambulensi za Uturuki

Magari ya kubebea wagonjwa ya Uturuki yakiwasaida waliojeruhiwa Syria

Waziri mkuu wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan, amesema nchi yake haitafunga mipaka yake kwa wakimbizi kutoka Syria, wakati mamia ya watu wamekuwa wakiitoroka nchi hiyo, kutokana na msukosuko wa kisiasa.

Bw Erdogan amesema anafuatia kwa makini matukio nchini Syria, na amemsihi rais Bashar al Assad kutekeleza mapendekezo ya mabadiliko ya kisiasa.

Mwandishi wa BBC aliye mpakani kati ya Uturuki na Syria ameelezea kwamba magari ya kubebea wagonjwa kutoka Uturuki yamekuwa yakivuka mpaka na kuingia Syria katika siku za hivi karibuni, na kurudi Uturuki yakiwa yamewabeba watu waliojeruhiwa katika maandamano ya kuipinga serikali ya Syria.

Ameelezea pia kuna raia wa Syria ambao wanaonelea badala ya kuvuka mpaka na kuingia Uturuki kama wakimbizi, ni afadhali kuishi katika hema hafifu walizojitengenezea, mita mia chache kutoka eneo la mpakani.








Rais Saleh wa Yemen 'aliumia' sana




Saleh

Rais wa Yemen Ali Abdallah Saleh anayedaiwa kujeruhiwa vibaya

Rais wa Yemen, Ali Abdullah Saleh, alijeruhiwa zaidi katika shambulio la makombora katika boma lake juma lililopita kuliko ilivyodhaniwa, maafisa wa Serikali wameambia vyombo vya Habari vya Marekani.

Maafisa wa Serikali waliambia shirika la Habari la AP kuwa Bwana Saleh alichomeka asilimia 40 ya mwili wake na anavuja damu katika fuvu lake kutokana na shambulio hilo la Ijumaa.

Rais anaendelea kupata matibabu nchini Saudi Arabia baada ya kushambuliwa katika Ikulu yake katika Mji Mkuu wa Yemen, Sanaa.

Afisa wa cheo cha juu Serikalini aliambia BBC kuwa hawatasema lolote kuhusiana na afya ya Rais Saleh.

"Sisi si madaktari. Na kama Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Marekani, Bi Hillary Clinton alivyosema jana, sisi tuko hapa na Sanaa na tunafanya kila juhudi kuhakikisha kuwa tunaleta mabadiliko kwa utaratibu, amani na bila ghasia, kama inavyosema Katiba ya Yemen," afisa huyo alisema.
Uwezo wa kutawala


Kaimu kiongozi, Makamu wa Rais Abd-Rabbu Mansour Hadi, alisema Bwana Saleh anatarajia kurejea baada ya siku chache.

Lakini wachunguzi wanasema kuwa kiwango cha majeraha ndicho kitakachoamua ni lini - na ikiwezekana - ikiwa atarudi katika taifa hili lenye umuhimu mkubwa ambalo amelitawala kwa zaidi ya miaka 33. Hali hiyo pia itaamua ni nani atakayechukua mamlaka iwapo yeye hatakuwa na uwezo wa kutawala.
Jaribio la kutaka Kuua

Haikujulikana kiwango cha alivyochomeka na kiwango cha majeraha alichokuwa nacho lakini Jumamosi wandani kadhaa wa Rais Saleh walisema kuwa alichomeka kwenye kifua na uso na kwamba mabaki ya kombora yalipenyeza chini ya moyo wake.

Rais alifanyiwa upasuaji Jumatatu ili kuondoa vipande vya mbao katika kifua chake na pia kumtibu majeraha ya moto kwenye uso na kifua, kama shirika la AP linavyoripoti.

Kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 69 hajaonekana tangu Ijumaa wakati makombora yalipotumika kushambulia Ikulu ya Rais na kuwaua watu saba na kuwajeruhi maafisa kadhaa wa vyeo vya juu Serikalini katika tukio ambalo maafisa hao wa Serikali wanasema ni jaribio la kutaka kuwaua.








Marekani yataka Gaddafi ang'olewe haraka








Marekani imeyaomba mataifa ya Magharibi na ya Kiarabu kuongeza juhudi katika azma ya kumng'oa kiongozi wa Libya Kanali Muammar Gaddafi.

Waziri wa mashauriano ya nchi za kigeni Bi Hillary Clinton amesema huu ndio wakati wa kumtimua Gaddafi.




Bi Clinton akihutubia mkutano wa Abu Dhabi

"Huu ni wakati wetu,mazingira yanaturuhusu.Gaddafi amefika kikomo'', Bi Clinton alisema katika mkutano wa viongozi wanaokutana mjini Abu Dhabi.



Bi Clinton pia aliwaambia wajumbe kuwa lazima juhudi zaidi zifanywe za kumbana Gaddafi na utawala wake kisiasa, kidiplomasia na kiuchumi.

Mkutano huo wa Abu Dhabi unatarajiwa kukamilisha mipango ya kuanzisha hazina maalum ya kuwasaidia waasi wa Libya.



Waakilishi wa nchi za Uingereza, Ufaransa, Marekani, Jordan, Kuwait na Qatar wanakutana ili kupanga jinsi Libya itakavyokuwa baada ya kumtimua Gaddafi uongozini.


Wakati huo huo Tripoli imekanusha madai ya uhalifu wa kivita ambayo yamewasilishwa mbele ya baraza la Umoja wa Mataifa kuhusu haki za binaadamu mjini Geneva.

Baraza hilo la Umoja wa Mataifa kwa wakati huu linajadili madai ya ukiukaji wa haki za binaadamu yanayodaiwa kutekelezwa na upande wa serikali pamoja na waasi.


Lakini mwanadiplomasia wa Libya Mustafa Shaban ameliambia baraza hilo kuwa upande wa serikali hauna hatia yeyote kwani ndio unaoshambuliwa.Na amelaumu vyombo vya habari, upinzani na mamluki wa kigeni kwa kukiuka haki za kibinadamu nchini Libya ikiwemo ukatili dhidi ya watu.










PRESIDENT OBAMA SUPPORTS WORLD FUTURE ENERGY SUMMIT HELD IN ABU DHABI





Abu Dhabi, 12 January 2011: In a guide to U.S. exhibitors attending the World Future Energy Summit, the President of the United States of America, Barack Obama, acknowledged the role of Abu Dhabi’s WFES in increasing economic growth and creating jobs. The letter follows on from Secretary of State Hillary Clinton’s visit to Masdar on Monday.

“Selected by the U.S. Department of Commerce as part of the U.S. Commercial Service’s Trade Fair Certification Program, this prominent trade exhibition is an excellent venue for developing new business,” wrote President Obama. “By opening new markets and promoting trade, we are creating new sales channels for U.S. products and services. The business relationships developed at this trade show will help increase economic growth and create jobs throughout the United States.”

President Obama’s recognition of WFES comes on the heels of a visit this week from U.S. Secretary of State Hillary Clinton to Abu Dhabi where she toured the Masdar Institute of Science and Technology – a graduate level institution dedicated to innovations in clean energy and established in partnership with the Massachusetts Institute of Technology. She emphasized the strong relationship between the United States and the United Arab Emirates and also praised Abu Dhabi’s commitment to the development of renewable energy and climate change mitigation.

“I want my country to know how advanced you are in pursuing clean renewable energy. I want the world to know that the US is partnering with you because we are betting on Abu Dhabi and the UAE,” said Secretary of State Hillary Clinton.

“We are betting that this incredible investment represented by Masdar is going to pay off,” added Secretary Clinton. “And when it pays off, it will not only mean a better life for the people in this country and in this region, it will have ripple effects throughout the world.”

WFES received a further message of support from the US Ambassador to the United Arab Emirates, HE Richard G. Olson in the guide to exhibitors.

“I am pleased to lend my endorsement to the U.S. Department of Commerce’s recognition of the World Future Energy Summit that has evolved as the world’s foremost and must-attend annual meeting for the renewable energy and environment industry,” wrote Ambassador Olson.

Focusing on renewable and future energy solutions, innovations, investments, policy and vision, WFES will be held at Abu Dhabi National Exhibition Centre, ADNEC, from 17th to 20th January 2011 and expects more than 25,000 attendees from around the world. The Summit that will cover a wide range of themes including energy policy, investment and funding, green buildings, clean transport, solar, wind and biofuels.