KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Wednesday, January 12, 2011

Vodacom wazindua simu za wasioona,wasiosikia


KAMPUNI ya simu ya mkononi ya Vodacom Tanzania, imezindua simu maalum kwa ajili ya watu wenye ulemavu wa macho na matatizo ya kusikia zitakazoweza kuwasaidia kutumia simu hizo.
Akizungumza na wwanahabri wakati wa uzinduzi ,Meneja Mawasiliano wa kampuni hiyo, Nector Foya, alisema simu hizo ni tofauti na nyingine kwa kuwa zitawawezesha wateja kundi hilo kutmia simu hizo kama wengine na kupata huduma ambazo hazipo katika simu za kawaida.

Simu hizo zimewekwa maandishi makubwa katika Keypad, sauti kubwa katika spika na king'ora maalum nyuma ya simu kitakachowawezesha makundi hayo kukibonyeza wakati wa dharura.

Alisema Vodacom imemua hivyo kutokana na kugundua kuna watanzania wengi wanapata shida katika kutumia simu za kawaida ka kuwa na maandishi madogo, sauti ndogo na wengi huhitaji malekezo kutoka kwa watu wengine pindi anapohitaji kutumia simu

No comments:

Post a Comment