KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Saturday, November 27, 2010

Za mwizi arubaini


MWANAUME mmoja [45] [jina kapuni] mkazi wa Sinza, amejikuta akihaha huku na huku kurudisha amani katika ndoa yake baada ya kufumaniwa akiwa na msichana wa kazi bafuni wakika uroda.
Hayo yametokea juzi, majira ya alfajiri, ndani ya nyumba yake hiyo kumshinikiza msichana huyo amfate bafuni.

Ilidaiwa kuwa, mwanaume huyo alikuwa akimvizia msichana huyo aliyetambulika kwa jina moja la Lucy pindi mke wake anapokuwa akiingia zamu ya usiku kutokana na kazi yake anayoifanya.

Ilidaiwa siku ya tukio mwanamke huyo aliaga anakwenda kazini lakini njiani alipata simu iliyomtaka na kumuomba asiende muda huo k wa kuwa alimuomba amshikie zamu hiyo na yeye aingie zamu yake.

Ilidaiwa mwanamke huyo, alipopata simu hiyo ilibidi arudi nyumbani kwa muda na ajitayarishe kwa kuingia kazini jioni.

Mume huyo ilidaiwa, wakati mke wake anatoka alikuwa yu kitandani lakini alishangazwa alipoingia chumbani kwake hakumkuta mumewe huyo na alishangaa na kwenda kumuuliza msichana na huko pia hakukuta mtu na ndipo alipoanza kumuuita msichana huyo.

Kabla binti huyo hajaitikia, mwanamake alikwenda kumuangalia binti huyo bafuni labla atkuwa amekwenda kuoga lakini alichokiona huko ni nusu ya kuzimia na kumkuta mumewe akiwa na binti huyo na mwanamke huyo kuwaacha waendelee na shughuli yao hiyo.

HAta hivyo chanzo cha habari hii kilidai kuwa, mwanamke huyo huwa ana shida sana ya kukaa na wasichana wake wa kazi kwa kuwa wasichana hao wanapokuwa wamepata kukaa zaidi ya mwezi huwa wanamtaka mwanbamke huyo awarudishe nyumbani kwao na alikuwa haelewi tatizo lilikuwa wapi.

Ilidawa mwanamke huyo ana mtoto wa mwaka mmoja sasa na toka ajifungue mtoto huyo, inadaiwa alishabadilsha wasichana wa kazi zaidi ya mara tatu kw kuwa wasichana hao walikuwa hawawezi kukaa humo kwa sababu ambayo alikuwa hajaielewa.

Hivyo mwanamke huyo alichofanya ni kwenda chumbani kumchukua mwanae na kumbeba na kuchukua nguo mbili tatu na kuondoka kwenda nyumbani kwao maeneo ya Boko akapumzike huko.

Imedaiwa mwanaume huyo alikuwa hajui aanzie wapi na kuona aibu kumuoimba mradhi mke wake huyo kutokana na kiitendo hicho alichomfanyia mke wake.

Kwa muendelezo zaidi juu ya kisa hiki endelea kusoma mtandano huu kwakuhabalishwa zaidi kinachoendelea

No comments:

Post a Comment