KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Saturday, November 27, 2010

Mgomo baridi ustawi wa jamii


NI SIKU kadhaa saa toka kuanze kwa migogoro ndani ya chuo hicho na jana kupelekea wanafunzi wa Chuo cha Ustawi wa Jamii cha jijini Dar es Salaam kufanya mgomo baridi wakidai marekebisho ya mambo mbalmbali chuoni hapo.
Uanzishwaji wa mgomo huo ulitokana na Madai ya huduma mbovu za vyoo na mfumo wa utumiaji wa hosteli za chuoni hapo urekebishwe.

Madai mengine yakiwemo na kutoridhika na uongozi wa sasa chuoni hapo, ikiwemo na wanafunzi wenzao wapatao 400 hawajapatiwa udahili.

Kufuatia mgomo huo. Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Jordan Rugimbana alifika chuoni hapo majira ya mchana na kukutana na uongozi wa chuo hicho huku wanafunzi wakiwa wamebeba mabango mbalimbali yenye ujumbe tofauti tofauti.

Serikali hiyo ya wanafunzi chuo hapo ilisema kuwa wamejipanga kwenda Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kukutana na Waziri wa Afya, kutafuta muafaka kuhusiana na chuo hicho.

Pia walisema, matatizo chuoni hapo yanatokana na ucheleweshaji wa kuundwa kwa bodi na waliipa serikali muda wa wiki moja kutatatua matatizo hayo

No comments:

Post a Comment