KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Saturday, November 27, 2010

UDSM yaunga mkono kusudio la JK



Fredy Azzah

SIKU moja baada ya Rais Jakaya Kikwete, kueleza kusudio la serikali yake la kuunda tume huru ya kupitia upya Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), baadhi ya wahadhiri na viongizi wa serikali ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), wameunga mkono uamuzi huo huku wakitaja maeneo muhimu yanayopaswa kuzingatiwa.

Wakizungumza na Mwananchi jijini Dar es Saal jana, walilitaja mambo makubwa yanayotakiwa kufanyiwa kazi ili kuondoa matatizo ya mikopo kwa wanafunzi kuwa ni pamoja na utendaji wa HESLB.

Mambo mengine ni pamoja kutafuta njia sahihi ya kufanya utambuzi wa uwezo wa mwanafunzi, ili aweze kupewa mkopo unaolingana na hali yake ya maisha.

Pia baadhi ha waadhiri na wanafunzi hao, walisema bodi ya mikopo inapaswa iwe na ofisi huru katika kila kanda au katika mikoa yote.

Hali kadhalika, walishauri idadi ya watumishi wa bodi hiyo, iongezwe kulingana na mahitaji ya wanafunzi wanaojiunga na vyuo vikuu kila mwaka.

Kwa mujibu wa Waziri wa Mikopo wa Serikali ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Silvanus Joseph, alisema kigezo cha kuangalia mtu kasoma shule gani bila kujua aliyemsomesha kipaswa kutumika katika kutambua uwezo wa mwanafunzi.

Aliongeza kuwa, tume hiyo itapaswa kuongeza fedha ambazo zimekuwa zikitoa kwa ajili ya mafunzo kwa vitendo na pia kutatua tatizo la ucheleweshwaji wa fedha hizo.

"Lakini tunapata shida kuamini kama haya aliyosema Rais yatatekelezwa kweli, mwaka 2007 alisema hakuna mtoto atakayekosa elimu ya juu kwa sababu ya umasikini wake, lakini tumeshuhudia masikini hao wakikosa nafasi hiyo," alisema.

Alisema mapema mwaka huu, Rais Kikwete alisema fedha za bodi zitaanza kutoka moja kwa moja hazina, ili kuepuka ucheleweshwaji, lakini nalo halikutekelezwa.

Wakati akifungua Maadhimisho ya miaka 50 ya chuo hicho, Waziri Mkuu Mizengo Pinda aliahidi kushirikiana na viongozi wengine kuhakikisha kuwa tume hiyo inaundwa na mapendekezo yake kutumika katika kuboresha utendaji wa HESLB.

Muhadhiri wa Chuo hicho Profesa Yunus Mgaya, alisema, alisema bodi inapaswa ilipe karo yote kwa wanafunzi

No comments:

Post a Comment