KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Friday, November 19, 2010

Maadhimisho miaka 50 UDSM leo




WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda leo anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya miaka 50 tangu kuanzishwa kwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Profesa Rwekaza Mukandala, alisema sherehe hizo zitafanyika katika Ukumbi wa Nkurumah kuanzia saa 3 asubuhi leo na mgeni raanatarajiwa kwua Waziri Mkuu .

Mukandala alisema sherehe za maadhdimisho hayo ni moja ya fursa za kutafakari na kuangalia changamoto za chuo hicho na kuagnalia walikotoka na wanakokwenda juu ya maendeleo ya chuo hicho.

Aidha alisema kuna baadhi ya changamoto zinazowakabili chuoni hapo na wanatarajia kwuasilisha mbele ya mgeni rasmi ikiwa na pamoja ukosefu wa sehemu za kulala wanafunzi, na kuhitaji nyongeza ya motisha kwa walimu na wafanyakazi wka ujumla chuoni hapo

No comments:

Post a Comment