KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Wednesday, November 3, 2010

JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, inawashiklia watu 21 kwa kusababisha kuokea klwa vurugu eneo la Tandika



JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, inawashiklia watu 21 kwa kusababisha kuokea klwa vurugu eneo la Tandika hali iliyofanya upotevu wa amani maeneo hayo.


Watu hao wamedaiwa kuanzisha vurugu, fujo zilizotokea jana, kuanzia majira ya saa 5 asubuhi, hali iliyofanya kufunga barabara, matairi kuchomwa moto hovyo na kuharibu magari ya raia hovyo .

Watu hao walianzisha vurugu hizo mara baada ya kutangazwa kwa mshindi wa udiwani wa kata ya Tandika, Bi. Zena Mgaya wa CCM na matokeo hayo hayakupokelewa vizuri kwa madai ushindi huo si halali na kuanza vurugu hizo.

Watu hao walidhamiria kutangazwa kwa mshindi Adamu Mbezi wa CUF kuwa mshindio wa kiti hicho.

Hali hiyo ilifanya magari ya polisi yakiwa na mabomu na maji ya kuwasha kufika eneo hilo nna kusambaza watu katika maeneo hayo.

Hali ilibadilika na kuwa na utulivu naw atu hao waliwa katika makundi kuhamia maeneo mengine na kuziba barabara na kupasua vioo vya magari hali iliyofanya askari haomn kurudi upya na kuanza mapambano na waharifu hao

No comments:

Post a Comment