KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Thursday, October 28, 2010

Wajue Wagombea 7 Wa Urais Tanzania


Fahmi Dovutwa -Mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha UPDP


Uchaguzi mkuu wa Tanzania utafanyika oktoba 31 jumapili ijayo, je unawajua wagombea wote saba wa urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania?
Jumapili ijayo Watanzaniawaliojiandikisha kupiga kura watatumia kura zao kumchagua rais mpya wa muungano wa Tanzania.

Jumla ya wagombea saba toka vyama saba tofauti wanawania nafasi hiyo muhimu ya kuliongoza taifa la Tanzania.

Je unawajua wagombea wote saba wa Urais? Kama huwajui basi wagombea urais ni hawa wafuatao.


Muttamwega Mgahywa: TLP
Mbunge wa jimbo la Mwibara, Mkoa wa Mara toka mwaka 1995. Katika bunge lililopita alikuwa Waziri Kivuli wa Ofisi ya Waziri Mkuu na Waziri kivuli katika Ofisi ya Makamu wa Rais.

Fahmi Nasoro Dovutwa: UPDP
Fahmi Nasoro Dovutwa amekuwa mwenyekiti wa chama cha UPDP( United Peole Democratic Party) toka mwaka 2000. Ni mjasirimali mwanasiasa anayegombea urais kwa mara ya kwanza.

Peter Kuga Mziray :APPT-MAENDELEO
Mziray ni Mchumi wa Kilimo mwenye shahada ya uzamili aliyoipata Moscow, Urusi. Alikianzisha chama cha APPT Maendeleo mwaka 1990 baada ya kujiengua NCCR-Mageuzi. Mara yake ya kwanza kugombea urais.

Hashim Rungwe: NCCR-MAGEUZI
Bwana Rungwe ni mwanasheria na wakili wa kujitegemea ambaye ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu na Baraza la Wadhamini wa chama cha NCCR-Mageuzi. Hii ni Mara ya kwanza kwake kugombea urais.


Dokta Wilbrod Slaa: CHADEMA
Kabla ya kuingia kwenye ulingo wa siasa, Dkt. Slaa alikuwa Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Tanzania, Kanisa Katoliki.
Amekuwa mbunge wa Karatu kwa tiketi ya CHADEMA kuanzia mwaka 1995 hadi sasa. Alikuwa makamu mwenyekiti wa CHADEMA kati ya mwaka 1998 na 2002 na baadae aliteuliwa kuwa katibu mkuu wa CHADEMA kuanzia mwaka 2002 hadi 2010. Hii ni mara yake ya kwanza kugombea urais.

Dokta Jakaya Mrisho Kikwete: CCM
Mgombea urais kupitia CCM. Anawania kuliongoza taifa la Tanzania kwa miaka mingine mitano baada ya muhula wake wa kwanza wa miaka mitano kuisha.

Prof. Ibrahim Haruna Lipumba: CUF
Kwa mara ya nne sasa Profesa Lipumba anagombea urais wa Tanzania tangu mfumo wa vyama vingi ulipoanzishwa Tanzania. Amewahi kuwa mwalimu wa vyuo vikuu vya Marekani na Tanzania na baadaye kuwa Mshauri wa uchumi wa Serikali ya Uganda kati ya miaka 1980 hadi 1990

No comments:

Post a Comment