KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Saturday, October 2, 2010

TPL nayo yaahidi elimu bure, sekondari zote kuwa bweni



MGOMBEA urais kwa tiketi ya Chama cha Tanzania Labour (TLP), Mutamwega Mgaywa, amewaomba watanzania wampe ridhaa aweze kuingia Ikulu na kuahidi kuboresha elimu kwa kuanzisha mfumo shule zote za sekondari kuwa za bweni na elimu hiyo kupatikanA bure
Mgombea huyo anaahidi hayo katika kampeni zake zinazoendelea nchi nzima na kusema ataweka mfumo huo kuboresha elimu hiyo kwa kuwa wanafunzi wengi huwa hawafanyi vizuri kutokana na kutembea umbali mrefu kufata shule hizo.

Amesema pia elimu ya chuo kikuu itakuwa bure watakaowajibika kulipia ni kwa wale watakaofeli masomo hayo kurudisha gharama waliyosomeshwa

No comments:

Post a Comment