KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Tuesday, October 26, 2010

Meya wa Nairobi mbaroni kwa ufisadi


Jiji la Nairobi




Meya wa mji mkuu wa Kenya-Nairobi ametiwa nguvuni kuhusiana na sakata la ununuzi wa kipande cha ardhi kiliyopangiwa kuwa eneo la makaburi viungani mwa jiji hilo.

Anatarajiwa kufikishwa mahakamani siku ya Jumanne kujibu mashtaka ya ufisadi.

Katika sakata hiyo maafisa wa baraza la jiji la Nairobi wanashutumiwa kupanga njama za kufuja takriban dola milioni tatu nukta mbili kwa kisingizio cha kununua kipande cha ardhi chenye ukubwa wa ekari 120 wakati thamani halisi ya hiyo ilikuwa ndogo.

Msemaji wa tume ya kupambana na ufisadi nchini Kenya Nicholas Simani amethibitisha kukamatwa kwa meya huyo Geofrey Majiwa na kukanusha madai kuwa maafisa wake walivamia makaazi yake bila kibali cha mahakama.

No comments:

Post a Comment