KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Tuesday, October 26, 2010

Mafuriko makubwa yaikumba Benin


Mafuriko mjini Cotonou


Theluthi mbili ya raia wa Benin wameathirika na janga baya zaidi la mafuriko kuwahi kulikumba taifa hilo la Afrika ya Magharibi.

Waandishi wa habari katika mji mkuu Cotonou, wanasema takribabn watu hamsini wamekufa kutokana na ugonjwa wa kipindupindu, wengi wao wakiwa ni watoto.

Mwanamuziki maarufu wa Benin Angelique Kidjo ameiambia BBC kuwa hajawahi kushuhudia maafa ya aina hiyo na kutoa wito wa kupatiwa misaada waathiriwa..


Akizungumza mjini New York Kidjo amesema nchi yake inahitaji sana msaada na kuongeza kuwa licha ya wasamaria wema nchini humo wamejitolea kusaidia, msaada unaotolewa hautoshi

No comments:

Post a Comment