KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Saturday, October 2, 2010

JK aahidi Chuo Kikuu Shinyanga



MGOMBEA urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi, Jakaya Mrisho Khalfani Kikwete, anaendelea na kampeni zake kuomba ridhaa kwa wananchi huku kuwaahidi wananchi kujenga chuo kikuu mkoani Shinyanga ahadi aliyoitoa juzi akwia wilayani Bukombe.




Kikwete aliwaahidi wananchi hao katika kampeni zake hizo kuwa, ni lazima ujenzi wa chuo hicho kikuu shinyanga ufanyike na kusema ujenzi wa chuo hicho utaanza pindi tu utakapokamilika ujenzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma na Butiama.

Pia aliahdi barabara za kiwango cha rami katika wilaya za Kahama na kwingineko mkioani humo kwa kuwa fedha za kukamilisha ujezni huo ziloishakuwa tayari na kukiri watendaji ndio wanachelewesha ujenzi huo.

Hivyo pia alitumia fursa hiyo kuwaagiza viongozi wa serikali ambao wanachelesha ujunzi huo na kuwakanya kuacha marumbano yanayofanya ucheleweshaji wa barabara hizo kwani wananchi wanahitaji ahadi hiyo

No comments:

Post a Comment