KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Thursday, October 28, 2010

CCM kuishtaki Chadema

CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM), kimedhamiria kukishitaki Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kutokana na kutukanwa kwa mgombea urais wa chama hicho, Jakaya Kikwete juzi jijini Dar es Salaam wakati wa chama hicho kilipokuwa kikifanya mkutano wa
Taarifa hiyo ilitolewa jana na Meneja wa Kampeni wa CCM, Kanali mstaafu Abdulrahiman Kinana, alipokuwa akizungumza na waandishi a habari katika ofisi ndogo za chama hicho.

Alisema CCM kinakusudia kuwasilisha malalamiko Tume ya Taifa ya Uchaguzi [NEC] na katika ofisi za Msajili wa Vyama vya Siasa ktuokana na Chadema kutumia mkutano huo kumtukana mgombea wao hadharani pasipo na sababu za masingi.

Alisema kitendo kilichofanywa na Chadema mbele ya wananchi hadharani kwa kutukanwa matusi ya nguoni Kikwete matusi yaliyotoka kwenye kinywa cha mgombea ubunge jimbo la Temeke kupitia Chadema, Amos Dickson, ni udhalilishaji .

Alisema kutoa matusi katika mkutano wa hadhara ni kukiuka kanuni za uchaguzi hivyo ni lazima chama hicho kichukuliwe hatua

No comments:

Post a Comment