KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Thursday, October 28, 2010

Kipindupindu chaua zaidi ya 250 Haiti



Idadi ya watu waliokufa kutokana na mlipuko wa maradhi ya kipindupindu nchini Haiti imezidi 250.

Zaidi ya watu 3,000 wameambukizwa, alisema Gabriel Thimote, mkurugenzi mkuu wa Idara ya afya wa Haiti.





Watu watano waligundulika kuwa na kipindupindu katika mji mkuu Port-au-Prince, lakini maafisa wa Umoja wa Mataifa alisema wagonjwa waligundulika mapema na kutengwa.





Maafisa wanasema maradhi hayo ni tishio kubwa kwa watu milioni 1.3 waliosalimika tetemeko la ardhi lililotokea mwezi Januari na ambao wanaishi kwenye mahema katika kambi zilizoko maeneo yanayouzunguka mji huu.




Hali itakuwa mbaya zaidi endapo tutakuwa na maelfu ya watu wakiwa wagonjwa kwa wakati mmoja," alisema rais wa chama cha madaktari wa Haiti, Claude Surena.






Lakini Bw Thimote alielezea matumaini yake kuwa mlipuko huyo utaweza kudhibitiwa

No comments:

Post a Comment