KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Thursday, October 28, 2010

Bado siku tano



KILA kona ya nchi, jiji na vitongoji vyake watanzania wamekuwa wakiisubiria kwa hamu siku ya Oktoba 31, ili waweze kuwachagua viongozi watakaowaongoza katika kipindi cha miaka kumi na tano ijayo.
Hali hiyo imefanya watanzania wengi kuzungumzia siku hiyo huku kila mmoja akiwa na shauku kubwa ya kuingia katika chumba cha kura cha kumchagua kiongozi wake anayempenda amuongoze kwa kuridhika na utendaji wake ama sera zake.

Katika hali hiyo uchaguzi wa mwaka huu, umekuwa na upinzani huku wengine wakiusisha uchaguzi huu kutawaliwa na udini hali inayofanya watu kuisubiri siku hiyo ili waweze kumaliza mizozo na ubishani ambao umetawaliwa kwa rika zote.

Hivyo pia watanzania wametakiwa watembelee vituo vyao vya kupigia kura kukagua majina yao ili kuhakiki kama jina lake lipo katika kituo husika.

Wagombea nao wamekuwa wakimwaga sera zao zao katiika wiki la lala salama na kuendelea kumwaga ahadi kemkem katika kutafuta kura.

MUNGU IBARIKI TANZANIA, UCHAGUZI UISHE KWA USALAMA, NA AMANI IENDELEE KUDUMU NDANI YA NCHI YETU

No comments:

Post a Comment