KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Tuesday, September 14, 2010

Wanawake tumieni fursra hii



WANAWAKE wajasiriamali zaidi ya 100 wanatarajiwa kukutana kujadili maendeleao ya Taifa hususani ya wanawake.

Wanawake hao wanatarajiwa kukutana Septemba 16 na 17 mwaka huu kupitia kongamano lililoandaliwa na Tanzania Women Entrepreneurs Networking and Development Exposition (TWENDE)

Mwenyekiti wa jukwaa hilo, Mustafa Hassanali alisema jukwaa hilo linalotoa fursa kwa wanawake ya kuuza na kuonesha bidhaa mbalimbali wanazozalisha kutoka sehemdu mbalimbali na kuwapa fursa kufanya biashara za aina tofauti pamoja na taasisi za serikali.

Pia watashiriki katika semina elekezi ya biashara ya kuwaelimisha na kuwawezesha ufanikishaji katika biashara pamoja na kupata mafanikio na maendeleo kwa ujumla.

Hasannal aliwataka wanawake wengi kujitokeza katika jukwaa hilo, kuonyesha bishaa zao na kujifunza mbinu mbalimbali za kibiashara

No comments:

Post a Comment