KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Monday, September 27, 2010

Wanafunzi mbaroni kwa mauaji



WANAFUNZI wanne wakiume wa Shule ya Msingi Ufukoni iliyopo Kigamboni jijini Dar es Salaam, wenye umri kati ya miaka 15 hadi 17 wametiwa mbaroni kwa tuhuma za mauaji ya mwanafunzi wa darasa la tano Jesica Ngosi (10).
Akitoa taarifa hiyo kwa wanahabari, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, David Misime, alisema kuwa, tukio hilo la mauaji lilitokea juzi majira ya saa 2 usiku.

Kamanda Misime alisema kuwa wanafunzi hao wanashikiliwakwa kuhusika katika tuiko hilo na mwili wa mwanafunzi huyo ulikutwa ukiwa na majeraha mbalimbali mwilini yaliyotokana na kuchomwa na vitu vyenye ncha kali.

Aliendela kusem kuwa kabla ya mauaji hayo marehemu aliondoka nyumbani hapo na binamu [17] jina limehifadhiwa, mkazi wa Tungi Kigamboni na binamu yake huyo alirudi majira ya saa mbili usiku akiwa mwenyewe na alipoulizwa mwenzake huyo alikwua wapi alijibu amekwenda kucheza na wenzake wengine wka kwua walimuita.

Alisema kutokana na jibu hilo, dada wa marehemu alipatwa na wasiwasi baada ya kumuona binamu yao huyo akihha kutafuta maji na kunawa mikono na kuvua shati lake na kuanza kulisafisha hali ambayo ilimshangaza na alipotoka kwenda kumtafuta mtoto huyo alimzuia na dada huyo aliendelea kumsaka mdogo wake huyo na binamu yake kumfata nyuma na alimkataza asipite njia ya makaburini walipofanya tukio hilo.

Ndipo dada huyo alipoamua kurudi nyuma kwanza kwenda kutoa taarifa kwa baba yao kufuatia tukio hilo na kwa pamoja akiwa na baba yake walipofuatilia njia hiyo walikuta mwili huo ukiwa mfu na ukiwa na majeraha maeneo ya shingoni, sehemu zake za matiti kwa kuchomwa na vitu vyenye ncha kali.

Baada ya hapo walitoa taarifa kituo cha polisi na polisi walianza msako kumsaka kijana ambae ni binamu wa marehemu na kumkuta akiwa chumbani kwake akiwa amejitundika kamba tayari kwa kujinyonga na alipohojiwa na skari alikiri kuhusika na aatukio hilo na kueleza likuwa na wenzake wengine watatu na waliweza kukamatwa mara moja.

Kamanda Misime amesema kuwa majina ya wanafunzi hao kwa sasa yanahifadhiwa kwa sababu za kipolisi na yatawekwa bayana pindi upelelezi utakapokamilika

No comments:

Post a Comment