KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Monday, September 27, 2010

Mdahalo vijana wang'ara



MDAHALO uliowashirikisha wagombea ubunge wa vyama pinzani umevutia kwa wagombea hao kila mmoja kumwaga sera zake na kutetea ilani za vyama vyao katika uchaguzi mkuu ujao.
Wagombea hao vijana kutoika chama cha Wananchi [CUF], Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na Chama cha Wananchi (CUF), wameonyesha uwezo mkubwa wa kuzinadi sera zao na ushujaa wa kujibu maswali ya papo kwa papo.

Mdahalo huo ulifanyika juzi katika Hoteli ya MovenPick ya jijini Dar es Salaam na kurushwa moja kwa moja na kituo cha Televisheni cha ITV na kuhudhuriwa na wadau wapatao 200.

Wagombea hao wote kwa pamoja waliwasilisha hoja na kuahidi kubadili na kufanya marekebisho ya katiba na mfumo wa utawala nchini pindi watakapoingia Ikulu.

Katika kuwasilisha hoja hizo mgombea ubunge jimbo la Kawe kupitia Chadema, Bi. Halima Mdee alsiema pia watashughulikia swala la ufisadi na kuahidi kuunda mahakama maalum itayowashughulikia mafisadi hao.

Nae John Mnyika [Chadema] Ubungo alisema watakapopewa ridhaa hiyo na wananchi wataweza kuekebisha kero za ajira zinazoisumbuba nchi na kurekebisha vikwazo vyote vinavyosababisha vijana kukosa ajira wanapotoka vyuoni.

Nae Zitto Kabwe, mgobmea ubunge Kigoma Kaskazini kupitia Chadema, alisema chama hicho kikipata ridhaa ya wananchi itaboresha katika sekta ya madini ambayo chama hichdo hawakubaliani na serimali ya chama cha Mapinduzi.

Kwa Upande wa wagombe kutoka CUF akiwemo Miraji Mitubuliko, alisema kitapitia upya mikataba ya madini, na kueleza kuwa wataunda serikali tatu ambayo itaruhusu masuala ya Zanzibar kuamuliwa na Wanzibar wenyewe

No comments:

Post a Comment