KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Monday, September 27, 2010

Umoja wa Mataifa na AU kuunda tume ya pamoja


Umoja wa Mataifa na Muungano wa Afrika imebuni kamati ya pamoja itakayoshughulikia masuala ya amani na Usalama.

Kamati hiyo natarajiwa kukutana mara mbili kila mwaka ili kujadili masuala yanayopaswa kufanyika kwa wakati huo na pia kupanga mikakati ya siku zijazo.

Kamati hiyo inanuiwa kuimarisha ushirikiano katika harakati za kuzuia mizozo na masuala ya kutunza amani barani Afrika.

Jeshi la Pamoja la muungano wa Afrika na Umoja wa Mataifa limekuwa likihudumu katika jimbo la Darfur tangu mwaka wa 2008.

Umoja wa Mataifa vile vile hutoa msaada kwa jeshi la muungano wa Afrika linalohudumu nchini Somalia

No comments:

Post a Comment