KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Monday, September 27, 2010

Meli ya Ugiriki yatekwa nyara- Somalia


Maharamia wa Kisomali


Jeshi la muungano wa ulaya linaloshika doria katika pwani ya somalia, limesema meli moja ya mizigo ya Ugiriki imeshambuliwa na kutekwa nyara na maharamia.

Jeshi hilo la EU limesema meli hiyo kwa jina Lugela lilikuwa umbali wa maili 900 kutoka pwani ya somalia wakati ilipotuma mawasiliano ya dharura.

Tangu wakati huo, hakuna habari zozote kuhusu meli hiyo iliyokuwa imesheheni bidhaa za chuma. Wanajeshi hao wa EU wanasema meili hiyo ilibadilisha mkondo wake na kuelekea Somalia.

Meli hiyo ilikuwa na mabaharia 12 raia wa Ukraine.

No comments:

Post a Comment