KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Thursday, September 23, 2010

Michezo ya Jumuiya ya Madola Delhi yaanza




Michezo ya Jumuiya ya Madola 2010 imeanza vyema huku sherehe za ufunguzi zikifanyika katika uwanja wa Jawaharlal Nehru.

Wanamichezo kutoka nchi 71 walipita mbele ya uwanja huo waliongozwa na wenyeji wa 2006 na mwisho walikuwa wenyeji wa mwaka huu India.

Mwanamfalme wa Uingereza Charles na rais wa India Pratibha Patil alitangaza kuanza rasmi kwa michezo hio,lakini mwenyekiti wa kamati iliyoandaa michezo chair Suresh Kalmadi alizomewa na umati uliokuwepo uwanjani.

Licha ya matatizo yaliyotatiza maandalizi,sherehe ya ufunguzi iliyokua na washiriki 9,000 walioonyesha utamaduni wa India zilienda vizuri.

Katika taarifa yake,Kalmadi alisema kuwa India iko tayari kuwa mwenyeji wa michezo hio.


''Tumekuwa na changamoto nyingi lakini tumejitahidi na kukabiliana nazo," alisema.

Inakisiwa kuwa $6bn (£3.8bn) zilitumika - mara 60 zaidi ya kiwango kilichotengwa wakati walipopewa uwenyeji mwaka 2003

No comments:

Post a Comment