KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Thursday, September 23, 2010

“Tanzania bila ya Ukimwi inawezekana” yazaa mtunda





IMEDAIWA kuwa kasi ya wimbi ya mambukizi nchini Tanzania inapungua kwa kasi kutokana na juhudi zinazofanyika kumaliza maambukizi hayo.



Hayo yalibainishwa jana na Mwenyekiti wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (Tacaids), Dk. Fatuma Mrisho katika mjadala uliowakutanisha watalamu wa afya jijini Dar es Salaam kujadili mbinu mbalimbali kukabiliana na tatizo hilo.



Alisema kuwa kwa sasa kasi ya maambukizi inapungua na kutoa takwimu kuwa kuwa watu million 1.8 ndido wanaoishi na virusi kwa sasa nchini.

Alisema serikali kwa kushirikiana na taasisi mbalimbali inatumia kila aina ya mbinu kuhakikisha maambukizi yanapungua nchini.

Alisema Tacaids imepata mafanikio makubwa toka kuanzishwa kwake na lengo la kumaliza tatizo hilo na kubaki na Tanzania isiyo na ukimwi inavuka lengo.

Alisema Tacaids imekwua ikizunguka nchini kote kutoa elimu ya ukimwi ambayo kwa sasa imeonekana kuzaa matunda na wananchi kuelewa vizuri elimu hiyo.

Hata hivyo alibainisha kuwa katika maambukizi hayo wanawake ndio wameonekana kuambukizwa zaidi kuliko wanaume

No comments:

Post a Comment