KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Friday, August 6, 2010

Staili Mpya ya Ajabu ya Urembo

Msanii mmoja wa nchini Uingereza ameibuka na staili ya ajabu ya urembo wa nyusi kwa kutumia miguu ya nzi waliofariki kwenye nyusi zake.
Staili hiyo ya ajabu iliyopewa jina la "Flylashes", ilitengenezwa na kuwekwa online na msanii Jessica Harrison.

Video ya staili hiyo imekuwa gumzo online lakini imekumbwa na shutuma kali toka kwa makundi ya kutetea haki za wanyama PETA.

Msanii huyo hakuelezea aliipataje miguu mingi ya nzi aliyoitumia na hakutaka kutoa maelezo yoyote alipotakiwa kufanyiwa hivyo.

No comments:

Post a Comment