KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Friday, July 23, 2010

Wanajeshi wa Uganda wauawa Somalia


Wanajeshi wawili kutoka Uganda wanaolinda amani nchini Somalia chini ya Muungano wa Afrika wameuawa mjini Mogadishu.

Askari hao waliuawa katika mapigano kati ya vikosi vya AU na wapiganaji wa kiislam wa al-Shabaab.

Msemaji wa Muungano huo amethibitisha kujeruhiwa kwa wanajeshi wengine watatu.

Kwa mjibu wa jeshi la Muungano wa Afrika majeshi yamelazimika kuondoka katika ngome yake katika mji wa Mogadishu na kuelekea vitongojini ili kuwasaka wapiganaji hao.

Suala la hali ya usalama nchini Somalia huenda likawa ajenda kuu katika kikao cha viongozi wa nchi na serikali wa Muungano wa Afrika kitakachoanza mjini Kampala, Uganda wikendi hii

No comments:

Post a Comment