KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Thursday, June 10, 2010

watatu wa Somalia wajiuzulu

Mawaziri
Somalia
Mawaziri watatu wa serikali ya mpito ya Somalia wamejiuzulu. Akizungumza mjini Mogadishu hapo jana, waziri wa ulinzi Mohammed Siad amesema kuwa anajiondoa kutoka serikalini kwa kuwa imeshindwa kuweka uongozi thabiti nchini humo.

Mawaziri wengine waliojiuzulu wakiwa London ni Mohammed Abdillahi wa elimu na Hassan Maalim wa ofisi ya rais.

Wadadisi wanasema kuwa hatua ya kujiuzulu kwa mawaziri hao inahujumu serikali hiyo ya mpito ambayo tayari imekumbwa na matatizo mengi.


Somalia
Zaidi ya thuluthi mbili ya Somalia inashikiliwa na wapiganaji wa kiislamu. Nchi hiyo haijawahi kupata serikali thabiti tangu 1991.

No comments:

Post a Comment