KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Saturday, June 26, 2010

JK kuchukua fomu leo Dodoma, wanane nao kuchukua Zanzibar


















MWENYEKITI wa Chama cha Mapinduzi Taifa, Jakaya Mrisho Kikwete leo anatarajia kuchukua fomu ya kugombania Urais ambapo hadi sasa hana mpinzani ndani ya CCM huku Tanzania Zanzibar 8 wamejitokeza kuchukua fomu kugombea urais wa Zanzibar kupitia CCM.
Kikwete anatarajiwa kuchukua fomu asubuhi hii huko Dodoma kwa ajili ya kuomba kuwania kiti hicho kwa awamu ya pili kugombania ufais kwa tiketi ya chama cha Mapinduzi [CCM].

Hadi sasa kwa upande a Tanzania Bara hakuna aliyejitokeza kuchukua fomu mbali ya JAkaya Kikwete kwa tiketi ya CCM japo inasadikiwa wengine watajitokeza.

Kwa upande wa urais wa Tanzania Zanzibar, tayari vigogo nane wameshajitokeza kuchukua fomu hiyo kwa tiketi ya CCM.

Akiwemo Makamu wa Rais Tanzania Bara, DK, Mohamed Shein, Waziri Kiongozi Zanzibar, Shamsi Vuai Nahodha, Naibu Waziri Kiongozi, Ali Juma Shamhuna, Waziri Kiongozi mstaafu, Dk. Mohamed Gharib Bilal, Ali Abeid Karume na akiwemo na aliyekuwa Mkurugenzi wa Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo, Hamad Bakari Mshindo.

KAtika kuwania kiti hicho Dk. Shein anaonekana kuwekewa vikwazo mbalimbali huku ikidaiwa kuwa hana vigezo vya kugombania kiti hicho kwa kuwa jina lake haliko katika daftari la kudumu la wapiga kura Zanzibar kwakuwa yeye alijiandikisha katika kituo cha Oysterbay jijini Dar es Salaam.

Na vilevile kwa mijibu wa katiba ya Zanzibar, kifungu 26(2) C na kifungu 27(4) vinasema kuwa mtu anayestahili kuwa Rais anatakiwa kuwa na sifa za kuwa Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi

Hivyo kutokana na vifungu hivyo Shein ameonekana kutokuwa na sifa ya kugombania kiti hicho visiwani Zanziba

No comments:

Post a Comment