KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Friday, May 28, 2010

Wayne Rooney akanusha hali yake si nzuri


Mshambuliaji wa England Wayne Rooney amepuuza taarifa kwamba bado anaendelea kusumbuliwa na maumivu wakati zimesalia siku chache kabla kuanza fainali za Kombe la Dunia.
Rooney, mwenye umri wa miaka 24, msimu uliopita alikuwa akisumbuliwa na matatizo ya kiwiko cha mguu na nyonga na siku ya Jumatatu alipatwa na maumivu ya kukakamaa shingo wakati England ilipoilaza Mexico mabao 3-1 katika mchezo wa Kimataifa wa kirafiki.

Lakini amesema: "Hali yangu ni nzuri na nipo imara. Tangu tulipokusanyika pamoja wachezaji wa England nimekuwa nikifanya mazoezi kila siku.

"Sijapata matatizo ya kiwiko cha mguu, taarifa iliyoandikwa ni upuuzi mtupu. Nilipata matatizo kidogo ya kukakamaa shingo lakini yamekwisha."

Rooney ndiye mchezaji muhimu zaidi kwa England katika mashindano ya Kombe la Dunia yatakayofanyika Afrika Kusini, baada ya kuonesha kiwango kikubwa cha kupachika mabao ambapo aliifungia Manchester United mabao 34 msimu uliomalizika.

Mshambuliaji huyo wa England alicheza dakika zote 90 dhidi ya Mexico katika uwanja wa Wembley, laikini alishindwa kuongeza bao katika jumla ya mabao 25 aliyokwishafunga akiichezea England katika mechi yake ya 59 ya kimataifa.

Amefunga mara moja tu katika mechi saba zilizopita akiichezea England, lakini anaamini kuihakikishia timu yake anauwezo wa kucheza ni muhimu zaidi ya kufunga mabao.

No comments:

Post a Comment