KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Friday, May 28, 2010

UEFA kuzindua sheria mpya


Shirikisho la mchezo wa Soka barani Ulaya UEFA, hii leo linatarajiwa kuidhinisha sheria mpya ambazo zitazuia vilabu kutumia fedha zaidi wanavyopata.

UEFA ambayo husimamia mhezo huo barani ulaya imetumia muda wa miaka mitatu kubuni sheria hizo ambazo zinatarajiwa kuidhinishwa wa kamati kuu ya shirikisho hilo.

Sheria hizo zitazuia vilabu kupata hasara kila mwaka na pia kuzuia wamiliki tajiri kuwekeza fedha nyingi kwa kununua wachezaji wapya. Hata hivyo sheria hiyo itaruhusu vilabu kutumia kiasi chochote cha pesa kununua wachezaji mradi tu wana fedha za kutosha.


Ikiwa sheria hizo zingelikuwa zinatumika kwa sasa, mabingwa wa ligi kuu ya Uingereza Chelsea hawangeruhusiwa kushiriki kwenye ligi ya klabu bingwa barani Ulaya msimu ujao.

No comments:

Post a Comment