KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Thursday, May 27, 2010

WATU 22 wamejeruhiwa katika ajali -Dar


WATU 22 wamejeruhiwa vibaya na kupelekea kufikishwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kutibiwa baada ya kupata majeraha yaliyotokana na daladala waliyokuwa wakisafirira kupinduka katika Barabara ya Nyerere Dar es Salaam jana asubuhi.
Watu hao walikuwa ndani ya basi la abiria lililokuwa likifanya safari zake kati ya Gongolamboto na Kivukoni na walipata ajali eneo la Tanangozi kwenye brabara hiyo ya Nyerere .

Basi hilo lilipinduka na abiria hao kulaliana na basi hilo lilijaza abiria kupita kiasi kutokana na shida ya usafiri majfira ya asubuhi.

Majeruhi hao waliweza kupata majeraha katika sehemu mbalimbali za mwilini zikiwemo usoni, mikononi, kishwani na sehemu mbalimbali za mwili.

No comments:

Post a Comment