KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Thursday, May 27, 2010

Masikini mtoto huyu!


MTOTO Mohamed Ridhiwani mwenye umri wa miezi mitano amefariki dunia baada ya kutumbukia kwenye ndoo iliyojaa maji huko maeneo ya Sabasaba, Mtoni Mtongani jijini Dar es Salaam.
Akitoa taarifa juu ya tukio hilo kwa waandishi wa habari, Kamanda wa Polisi Mkoa Temeke, Bw. Elias Kalinga alisema kuwa tukio hilo lilitokea jana majira ya saa 12:00 jioni.

Amesema kuwa mtoto huyo alikuwa amelazwa kitandani ndani chumbani na mama yake.

Amesema mtoto huyo wakati yuko katika usingizi alianguka kutoka kitandani alikokuwa amelala na kutumbukia kwenye ndoo ya maji iliyokuwa karibu na kitanda hicho bila ya mama yake kuwa na taarifa.

Hivyo kutokana na mtoto huyo kuwa na umri huo alishindwa kujitetea na kufariki dunia baada ya kunywa maji mengi.

Wazazi wake waligundua tukio hilo mtoto huyo akiwa tayari ameishafariki. Taarifa zilipelekwa kituo cha polisi kwa uthibitisho na polisi mkoani Temeke walithibitisha tukio hilo.

Maiti ya mtoto huyo ilichukuliwa na kwenda kuhifadhiwa katika Hospitali ya Wilaya ya Temeke.

No comments:

Post a Comment