KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Thursday, May 27, 2010

Mwanafunzi anyofolewa sehemu zake za siri -Manyara


MTOTO wa kike aliyekuwa akisoma darasa la pili mkoani Manyara amenyofolewa sehemu zake za siri na kisha maiti yake kuwekwa kwenye kiroba kabla ya kutupwa kwenye kichaka mkoani humo.
Tukio hilo la kusikitisha liligundulika jana, huko eneo la Mbuyu wa Wajerumani mkoani Manyara baada ya wananchi kugundua maiti ya mtoto huyo wa kike aliyekuwa akisoma darasa la pili ikiwa imefichwa kwenye kiroba.

Wiki moja nyuma walezi wa mtoto huyo waliripoti katika vituo vya polisi kuwa mtoto huyo alipotea katika mazingira ya kutatanisha.

Katika juhudi za kumsaka mtoto huyo jana wananchi waliona kiroba kilichotelekezwa porini na kukichunguza ndipo ndani yake waligundua mwili wa mtoto huyo ukiwa humo.

Kutokana na tukio hilo, Jeshi la Polisi Mkoa wa Manyara linawashikilia waliokuwa walezi wa mtoto huyo ambao ni Fatma Juma na Hamad Athuman ambao ilidaiwa walimuomba mtoto huyo kwa mzazi wao waje kumlea.

Imedaiwa kuwa watuhumiwa hao ambao kwa sasa wako chini ya ulinzi wa polisi ni wafanyabiashara wa madini wa muda mrefu

Wanashikiliwa na uchunguzi zaidi kuhusiana na tukio hilo unafanywa na polisi ili kubaini kama tukio hilo limeendana na mambo ya ushirikina kama watu wanavyodai na kuhisi ama la.

No comments:

Post a Comment