KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Monday, May 10, 2010

Roy Bennett aachiliwa huru Zimbabwe


Mahakama ya Zimbabwe imetupilia mbali mashitaka dhidi ya mwanasiasa wa upinzani nchini Zimbabwe Roy Bennett. Mashitaka hayo yalikuwa madai ya kupanga njama za kumuondoa madarakani rais Robert Mugabe.

Bw Bennett ni mshirika wa karibu wa Waziri Mkuu Morgan Tsvangirai.

Jaji wa mahakama amesema upande wa mashitaka umeshindwa kuthibitisha kuwa barua pepe zinazodaiwa kumhusisha bw Bennet na muuza silaha mmoja, zilikuwa halisi.

Kesi hiyo ilitishia kugawanya serikali ya umoja inayoongozwa na mahasimu wa muda mrefu, bw Mugabe na bw Tsvangirai.

Bw Bennett alikuwa nje kwa dhamana.

Bw Bennett ni kiongozi wa juu wa chama cha bw Tsvangirai, MDC, na alitakiwa kuchukua wadhifa wa naibu waziri katika serikali, wakati alipokamatwa mwezi Februari mwaka 2009.

No comments:

Post a Comment