KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Friday, May 28, 2010

Omar al-Bashir aapishwa nchini Sudan


Rais wa Sudan, Omar al-Bashir, leo ameapishwa kuendelea na mamlaka ya rais, licha ya utata uliozuka katika uchaguzi wa mwezi uliopita.


Kumekuwa na malalamiko dhidi ya Bashir kutokana na uchaguzi mwezi uliopita
Mahakama ya kimataifa ya uhalifu ya ICC inamtaka kiongozi huyo kufikishwa mbele yake, kutokana na visa vya uhalifu katika eneo la Darfur.

Wageni wa nchi nyingi walioalikwa hawakuhudhuria sherehe hizo za kuapishwa, lakini viongozi kutoka nchi tano za Afrika walishiriki.

Umoja wa Mataifa ulikuwa umetangaza hapo awali kwamba wajumbe wake wa amani katika nchi hiyo watahudhuria sherehe hizo.

Akiapishwa, rais Bashir alilihutubia bunge mjini Khartoum kwa kipindi cha nusu saa.

Marais wa Ethiopia, Chad, Malawi, Mauritania na Djibouti walikuwa ni miongoni mwa walioalikwa.

Shirika la kutetea haki za kibinadamu la Human Rights Watch (HRW), limeelezea kwamba ni wazi serikali zinazotaka kuhakikisha haki inatendeka katika kuutatua mzozo wa Darfur kamwe hazikutaka kushiriki katika sherehe za kuapishwa rais Bashir.

No comments:

Post a Comment