KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Friday, May 28, 2010

Juhudi za kufukua miili Uganda zaendelea


Maafisa wa shughuli ya uokoaji nchini Uganda wanasema wanajitahidi kufukua mamia ya miili ya watu waliozikwa hai kufuatia maporomoko ya ardhi katika wilaya ya Bududa miezi mitatu iliyopita.

Kwa mujibu wa ripoti ya serikali zaidi ya watu mia mbili hawajulikani waliko, huku miili mia moja ikiwa imefukuliwa.

Kiongozi wa shughuli hiyo Luteni Kanali Wilson Kabera, amedokeza shughuli hiyo imetatizika kutokana na mvua kubwa na pia matatizo ya kuharibika kwa mitambo na mashini zinazotumika kufukua miili hiyo.

Zaidi ya watu elfu nane walihama makwao kutokana na maporomoka hayo ya ardhi.

No comments:

Post a Comment