KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Friday, May 28, 2010

Daktari wa Rwanda akamatwa Ufaransa.

Maafisa wa polisi nchini Ufaransa hatimaye wamemkamata daktari kutoka Rwanda, Eugene Rwamucyo, kwa kutuhumiwa kuhusishwa na mauaji ya watu wengi mwaka 1994.


Daktari Rwamucyo alikamatwa kutokana na hati iliyotolewa na serikali ya Rwanda
Eugene amekuwa akitafutwa na polisi ya kimataifa, Interpol, tangu mwaka 2006.

Aliachishwa kazi katika hospitali moja ya kaskazini mwa Ufaransa, mwezi uliopita.

Maafisa wa serikali ya Rwanda, wanaodai kwamba daktari Rwamucyo alihusishwa na uhalifu katika mazingira ya vita wakati wa mauaji hayo ya watu wengi, wameelezea kufurahia hatua hiyo.

Daktari Rwamucyo amekanusha madai hayo, akisema ni kampeni na njama ya serikali ya Rwanda kumharibia sifa.

Alikamatwa mjini Sannois, kaskazini mwa Ufaransa, mara tu baada ya kuhudhuria mazishi ya afisa mmoja wa zamani wa serikali ya Rwanda, na ambaye pia alikuwa ameshitakiwa kwa mauaji ya watu wengi.

Habari hizo ni kwa mujibu wa maafisa wa serikali wa Ufaransa.

Hatua ya kukamatwa kwake inafuatia juhudi za Ufaransa kuwakamata washukiwa wa mauaji ya watu wengi nchini Rwanda, huku uhusiano wa kidiplomasia ukiendelea kuimarika kati ya nchi hizo mbili.

No comments:

Post a Comment