KARIBU MAISHANI
KARIBU MAISHANI
Tuesday, May 11, 2010
'Nipigie' ya AT Kuingia Sokoni
Mwanamuziki huyo aliyezaliwa mjini Zanzibar na kufanikiwa kusoma katika shule ya msingi Mwembe Shauri na Forodhani, alianza fani ya muziki mwaka 2007
Tayari mpaka hivi sasa ana albamu mbili ya kwanza ikijulikana kwa jina la Nikufundishe iliyokuwa na nyimba 12. Baadhi ya nyimbo katika albamu hiyo ni Mapenzi,wanichosha na raha zako.
Katika albamu hii mpya ya Nipigie kuna nyimbo ambazo ameshirikiana na wasanii kutoka Uganda na Kenya.
Wimbo wa Nipigie amemshirikisha Stara Thomas na katika nyimbo zingine amewashirikisha Nemless wa Kenya na Ngoni wa uganda.
Albamu ya Nipigie inategemewa kuingia sokoni punde baada ya maandalizi ya uzinduzi wa albamu hiyo yatakapokamilika.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment