KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Thursday, May 27, 2010

Msafara wa Kikwete Mmmh! chupuchupu


MAGARI aliyokuwa amepanda Rais Jakaya Kikwete, katika ziara yake ya siku moja jijini Dar es Salaam, yalileta hitilafu baada ya magari hayo kuchomoka matairi yake katika maeneo tofauti yakiwa safarini.
Tukio la kwanza lilitokea jana maneneo ya Kimara Mwisho wakati Rais alipokuwa akitoka Kimara Bonyokwa katika ziara yake ya siku moja kutembelea maeneo yaliyokuwa na matatizo ya ukosaji maji kwa muda mrefu.

Msafara huo ulilazimika kusimama ghafla kutokana na gari alilokuwa amepanda kuchomoka tairi lake la mbele na baadaye Rais alilazimika kuhamishwa kutoka gari hilo kwenda jingine na bendera kuhamishwa kutoka gari hilo na kuwekwa gari alilopanda kwa mara ya pili.

Zoezi hilo ambalo lilishuhudiwa na wananchi na wakazi wa maeneo kufurika eneo la tukio kumshuhudia Rais wao akitoka gari moja kuingia jingine na walinzi wake pia kulazika kuhama ndani ya gari hilo.

Katika tukio la pili ya hitilafu msafara huo wakati unatoka eneo la Keko Toroli, ghafla ulisimama katika eneo la bandarini karibu na ofisi za BP baada ya gari alilokuwemo rais kuwa na hitilafu katika tairi lake la nyuma upande wa kulia lililochomoka.

Hivyo Rais alilazimika kuhamishwa tena kutoka kwenye gari hilo kwenda jingine.

Hivyo ndivyo ilivyokuwa katika msafara huo wa Rais na kuingia dosari na Rais kunusurika na ajali ambayo labda ingeweza kumpotezea maisha au kupoteza viungo kutokana na magari hayo kuleta hitilafu katikati ya msafara.

No comments:

Post a Comment