KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Thursday, May 27, 2010

Liyumba jela miaka miwili


MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, imemuhukumu kifungo cha kwenda miaka jela aliyekuwa Mkurugenzi wa Utumishi na Utawala wa Benki Kuu (BOT) Amatus Liyumba (62) baada ya kupatikana na hatia ya matumizi mabaya ya ofisi ya Umma.

Hukumu hiyo ilitolewa jana mahakamani hapo na Hakimu Lameck Mlacha wa Mahakama hiyo kwa kushirikiana na jopo la mahakimu watatu waliokuwa wakiongozwa na Hakimu Mkazi Edson Mkasimongwa wakati upande wa mashitaka ulikuwa ukiongozwa wakili Hilaly Mkate.

Katika hukumu hiyo mahakimu walionekana kutofautiana kwa maamuzi juu ya hakumu hiyo ambapo mmoja katika mahakimu waliokuwa wakisikiliza kesi hiyo kutofautiana na wenzake kwa kusema mshitakwia hakuwa na hatioa ya kosa hilo.

Hata hivyoo hukumu iliyotumika kumfunga mshitakiwa huyo ni ile iliyoonekana maoni yanayofanana na kukubalika na mahakimu wawili na kutumia hiyo kwa kuwa mahakimu wote waliona mshitakwia alikuwa ana hatia na kuacha ya mmoja ambapo alikuwa na maamuzi ya peke yake na kutumia usemi wa wengi wape.

Hivyo Liyumba alisomewa hukumu mbili mahakamani hapo na ya kwanza iliyosomwa na Hakimu Lameck Mlacha ilisema amemfunga mshitakwia huyo kwa kuridhika na ushahidi uliotolewa na mashahidi watano upande wa mashtaka kati ya mashahidi wanane waliosikilizwa katika shauri hilo.

Alisema watano kati yao walitoa ushahidi na kuidhihirishia na waliisisitizia mahakama kuwa gharama katika Mradi wa Ten Milambo ulisababishwa na matumizi mabaya ya madaraka na kuharibu mali ya umma.

Mashahidi hao walisema kuwa mshtakiwa alikuwa akisaini na kutoa maelekezo katika mradi huo uliokuwa chini ya uongozi wa idara aliyokuwa akiiongoza mshitakiwa.

Hakimu Mlacha alisema kuwa mahakama imebaini kuwa mshtakiwa alikuwa akitoa maelekezo kinyume na utaratibu wa BOT kiasi cha kuwa na nguvu ya kubadili uhalisia wa mradi..

Baada ya hukumu hiyo wakili aliyekuwa akimtetea mshtakiwa Bw. Majura Magafu aliiomba mahakama hiyo kuwa na huruma na mshitakiwa japo ameonekana kupatikana na hatia kwa kuwa mshitakiwa alikuwa ni mtumishi wa serikali na ameitumikia BoT kwa uadilifu na kwa muda mrefu kwa miaka 35.

Katika maombi hayo pia aliiomba mahakama hiyo kuangalia umri wa mshitakiwa apunguziwe adhabu kwa kuwa anategemewa na familia yake na atayari alishakuwa mstaafu.

Awali Mwendesha Mashtaka Wakili wa Serikali, Bw. Prosper Mwangamila alidai mbele ya mahakama hiyo kuwa Amatus Liyumba, alitenda makosa hayo kati ya mwaka 2001 na 2006 akiwa mtumishi wa Benki Kuu ya Tanzania [BoT] alitumia vibaya madaraka ya ofisi yake katika ujenzi wa majengo pacha ya benki hiyo na kuisababishia hasara serikali y a shilingi bilioni 221.

Ndugu, jamaa na marafiki walianza kuangaua kilio mahakamani hapo bada ya kutolewa hukumu hiyo na ndugu yao kulalamika kuwa hukumu hiyo haikua sahihi na kudai ushahdi uliotolewa haukuchambuliwa ipasavyo.

Liyumba aliweza kusotatu rumande kwa zaidi ya mwaka mmoja na miezi mitatu baada ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamana yaliyomtaka kutoa Sh bilioni 110.

Hivyo Liyumba alipandishwa kwenye gari la washitakiwa lililokuwa na namba STK 4373, majira ya saa 7.43 mchana kwenda kuanza maisha yake mapya gerezani kwa muda wa miaka miwili.

No comments:

Post a Comment