KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Monday, May 31, 2010

Mahakama ya ICC 'yabadili mwenendo'


Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema, mahakama ya kimataifa ya uhalifu wa kivita (ICC) imefanikiwa kulazimisha serikali kubadili mwelekeo wao tangu iundwe miaka minane iliyopita.

Ban Ki-moon ameuambia mkutano unaofanyika Uganda unaojadili kuhusu mahakama hiyo iliyopo Hague kwamba imepunguza uwezekano wa watu kuepuka adhabu na kuweka misingi mipya juu ya haki za waathiriwa.

Lakini ametoa wito wa nchi wanachama kushirikiana.

ICC ina kesi tano zinazoendelea, zote zikiwa kutoka barani Afrika. Mpaka sasa hakuna aliyepatikana na hatia ya madai ya kuhusika na uhalifu wa kivita.

Bw Ban aliwaambia viongozi, " Kwa wakati ule wachache wangeamini kwamba mahakama hii ingekuwa hapa ilipo, inafanya kazi vizuri, inafanya utafiti na kuendesha mashtaka ya uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya binadamu.

"Katika karne hii mpya ya uwajibikaji, wale wanaofanya uhalifu mkubwa zaidi dhidi ya binadamu watashughulikiwa ipasavyo."

Bw Ban amesema wakati sasa umepita wa dunia kuchagua baina ya amani na haki- sasa mataifa yanatakiwa kukabiliana nayo bega kwa bega.

Lakini mwandishi wa BBC Karen Allen kwenye mji mkuu wa Uganda, Kampala, amesema hatua ya kutoa hati za kukamatwa dhidi ya viongozi waliopo madarakani, akiwemo Rais Omar al-Bashir wa Sudan kwa madai ya uhalifu wa kivita mjini Darfur, imezua wakosoaji wengine kusema mashtaka kama hayo yanakatisha tamaa harakati za kuleta amani katika eneo hilo.

Viongozi kutoka zaidi ya nchi 100 wanashiriki mkutano huo, kujadili mafanikio ya ICC na kutoa mapendekezo ya kuimarisha sheria zake.

No comments:

Post a Comment