KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Monday, May 31, 2010

Ufaransa imekusudia kuipa Afrika msukumo mpya wa biashara


Ufaransa imekusudia kuipa Afrika msukumo mpya wa biashara katika mkutano wa siku mbili unaofunguliwa mjini Nice.

Rais Nicolas Sarkozy ndio mwenyeji wa mkutano unaohusisha Afrika na Ufaransa kwa mara ya kwanza.
Viongozi 38 wa Afrika na watendaji 250 wa biashara wanahudhuria mkutano huo.

Viongozi wa kijeshi kutoka nchi mbili zilizokuwa koloni la Ufaransa, Guinea na Niger, ni miongoni mwa nchi zinazohudhuria.

Ufaransa inachuana na China na mataifa mengine yanayoibuka kwa kutafuta masoko Afrika.

Matatizo ya uharamia, ugaidi na mabadiliko ya hali ya hewa ni miongoni mwa yatakayojadiliwa.

Nchi za Afrika zinataka ziwe na nguvu zaidi katika baraza la usalama la Umoja wa Mataifa na kongamano la G20, kwahiyo pia kutakuwa na mjadala wa namna ya kufanikiwa kutekeleza hayo.

Kundi la Civil liberties limesema miongoni mwa wakuu wa nchi 38 wa Afrika walioalikwa ni viongozi wawili tu ambao hawakuweza kushutumiwa kuhusika na kukiuka haki za binadamu.

Madagascar-ikiwa bado katika mgogoro wa kisiasa haikualikwa, na Zimbabwe ilikataa kupeleka mjumbe wake baada ya Ufaransa kumzuia Rais Robert Mugabe kuhudhuria mkutano huo.

Gazeti la France Le Monde limeripoti, katika hatua ya kuonyesha kuwa Ufaransa haijahusisha nchi zinazozungumza kifaransa peke yake, Rais Sarkozy atafanya mazungumzo ya pamoja na viongozi wa Nigeria na Afrika Kusini, nchi mbili zinazozungumza kiingereza na zenye uzito barani humo.

No comments:

Post a Comment