KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Monday, May 31, 2010

Askofu wa Ireland ajiuzulu Nigeria


Makao makuu ya kanisa la Kikatoliki Vatican imekubali hatua ya kujiuzulu kwa askofu wa Ireland aliyekuwa Nigeria kutokana na shutuma za kumdhalilisha kijinsia binti mmoja huko Niger Delta.

Richard Burke, askofu wa mji wa Benin, amekubali kuwa na uhusiano wa kimapenzi na binti huyo lakini amekana kwa binti huyo kuwa na umri mdogo uhusiano huo ulipoanza.

Katika taarifa iliyotolewa kwenye gazeti la kikatoliki la Ireland amesema, " Sababu ya kujiuzulu ni kutokuwa mwaminifu katika kiapo changu cha useja."

Askofu huyo amejiuzulu baada ya madai hayo kutolewa mwaka jana.

Dolores Atwood alidai kunyanyaswa kijinsia na askofu Burke wakati alipokuwa padri huko Warri kusini mwa Nigera kwenye mji wa Niger Delta.

Hata hivyo, amesema uhusiano wao ulianza mwaka 1989 alipokuwa miaka 40 na binti akiwa na umri wa miaka 21.

Amesema kwenye taarifa yake, " Nilijibu haraka iwezekanavyo kwamba sijawahi hata siku moja maishani mwangu kumnyanyasa mtoto kijinsia. Huu bado ni msimamo wangu. Huu ni ukweli."

Askofu Burke pia alimwomba radhi Bi Atwood na kuomba msamaha katika vituo vyake vya kanisa huko Warri na Benin.

Kanisa hilo limesema limekubali kujiuzulu kwake ambapo pia limetaja jopo litakalochunguza udhalilishaji wa watoto
uliofanywa na viongozi wa kikatoliki huko Ireland.

No comments:

Post a Comment