KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Friday, May 28, 2010

Magazeti binafsi rukhsa Zimbabwe

Magazeti manne ya binafsi yanayochapishwa kila siku Zimbabwe yamepewa kibali na tume iliyoundwa na serikali ya muungano ili kufanya marekebisho ya vyombo vya habari.


Magazeti manne yapewa kibali Zimbabwe
Vyombo vya habari vya Zimbabwe kwa sasa vimeshamiri magazeti ya serikali.

Kibali kimoja kimetolewa kwa Daily News, gazeti lililokuwa likimkosoa Rais Robert Mugabe, lililofungwa mwaka 2003.

Bw Mugabe na Waziri mkuu Morgan Tsvangirai wamekuwa katika serikali ya kugawana madaraka tangu mwaka 2008.

Tume ya habari ya Zimbabwe (ZMC) iliundwa Desemba 2009 chini ya makubaliano ya kufanya mabadiliko kwa vyombo vya habari, ikiwemo kutoa vibali kwa magazeti mapya, redio na televisheni.

Kwa sasa, vyombo vya habari vya binafsi nchini humo vinapewa vipingamizi vizito.

Shirika la habari la Reuters limemnukuu mwenyekiti wa ZMC Godfrey Majonga akisema, " Tuko hapa kuwapa Wazimbabwe fursa ya kupata habari."

Mwaka 2002, Bw Mugabe alianzisha sheria kali kwa vyombo vya habari ikiwataka waandishi wa habari na magazeti kujisajili kwa serikali na iwapo mtu akashindwa kutekeleza hilo hufungwa gerezani.

Waandishi wa habari pia huweza kufungwa gerezani kwa "kuchapisha taarifa za uongo."

Waandishi wa habari wa gazeti binafsi la Daily News walikamatwa, na kiwanda cha kuchapisha magazeti kililipuliwa kabla ya gazeti hilo kufungwa rasmi mwaka 2003.

No comments:

Post a Comment