KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Thursday, May 27, 2010

Watano wa familia moja wateketea kwa moto


WATU watano wa familia moja wamefariki dunia baada ya nyumba yao kuteketezwa kwa moto uliodaiwa kuwashwa kimakusudi kuteketeza familia hiyo huko Vijibweni Wilayani Temeke.
Tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia jana majira ya usiku, huko maeneo ya Vijibweni Temeke ambapo ajali hiyo imetokana na ugomvi wa kimapenzi kutoka kwa mmoja wa wanafamilia hiyo.

Watu hao wote kwa pamoja waliweza kupoteza maisha usiku huo baada ya nyumba hiyo kuteketea kwa moto wakiwa ndani kwao katika chumba kimoja kwa pamoja.

Wanafamilia hao walioteketea kwa moto ni baba wa familia, John Onesmo (32) ambaye ni mfanyabiashara wa samaki eneo la Feri, mke Catherine John (25), watoto wao wawili ambao ni Joyce John (5) na Oliver John na Esther Amos (20) ambaye ni mdogo wa Catherine.

Moto huo uliolipuliwa majira ya saa 6 usiku, ulidaiwa kulipuliwa na mchumba wake Ester aliyetambulika kwa jina la Shemsa Mpelela (22), kutuhumiwa kuchoma moto nyumba hiyo kwa kutumia mafuta aina ya petroli

Kwa mujibu ya maelezo ya majirani usiku huo walisikia mlipuko mkali na walidhani kuwa pikipiki imepasuka tairi ama mlio wa risasi na kuamka na kuona nyumba hiyo inawaka moto.

Majirani waliweza kuamka kwa kushirikiana kutaka kuwaokoa watu hao lakini ilishindikana kwa kuwa moto ulishapamba kuzingira nyumba hiyo na juhudi zilishindikana na watu hao kumaliza maisha ndani humo

Hata hivyo zimamoto lilichelewa kufika eneo hilo kutokana na ubovu wa barabara na gari lilikwama njiani.

Askari walipofika eneo la tukio na baada ya moto huo kuzimwa walipoingia ndani tayari watu hao walishapoteza maisha na John alikutwa amekumbatia watoto wake kitandani.

Tukio hilo ambalo moja kwa moja linahusishwa na ugomvi kati ya Ester na Shemsi majirani walidai kuwa mwaka jana Esther alipomaliza darasa la saba Manyoni, Singida, alikuja kwa dada yake huyo kuishi nae.

Ilidaiwa na majirani hao kuwa Ester alianza tabia ya kuwa na mahusiano ya kimapenzi na wanaume mahali hapo hali ambayo dada yake alikuwa akigombana nae hadi ilifikia hatua dada yake huyo kumrudisha kijijni kwao kutokana na tabia zake hizo.

Ilidaiwa kuwa Ester alirudi tena jijini kwa kurudishwa na nauli aliyotumiwa na Shemsi na kwenda kuishi nae Kigamboni nyumbani kwa Shemsi na alirudi na kuja tena kwa dada yake baada ya kutokea ugomvi wa kimapenzi ambao haujafahamika chanzo chake hali iliyopelekea Shemsi kumchoma kisu Ester shingoni na tumboni.

Na dada yake kwa kushirikiana na mume wake walijaribu kumtafuta Shemsi na hawakuweza kumpata na hawakujua yuko wapi.

Na usiku wa kuamkia jana baada ya tukio hilo kutokea dumu ambalo lilikuwa na mafuta hayo lilionekana pembezoni mwa nyumba hiyo ambayo ilikuwa haijaisha na kumalizika chumba hicho na kuhamia.

Polisi Mkoani Temeke limethitisha kutokea kwa tukio hilo na tayari linafanyia kazi tukio hilo la kusikitisha.

No comments:

Post a Comment