KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Thursday, May 13, 2010

Kikwete azindua jengo la upasuaji wa moyo


RAIS Jakaya Kikwete ameweka jiwe la msingi katika jengo la tiba la magonjwa ya upasuaji wa moyo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, jijini Dar es Salaam.
Pia jengo hilo ni kituo cha mafunzo ya atiba ya magonjwa hayo nchini.

Udhamini wa Ujenzi huo umetokana na ahadi ya Rais Hu Jintao wa China, aliyoahidi kuisaidia Tanzania alipokutana na Rais Kikwete mwaka 2006 kwenye mkutano wa China-Africa jiji Beijing.

Kikwete alisema nchi ilikuwa inahitaji kwa miaka mingi kujenga kituo hicho na uwezo wa kutibu na kufanya upasuaji wa moyo nchini na sasa imeshukuru Rais Jintao kwa kujenga kituo hiko na Tanzani itakuwa imejikomboa katika changamoto hiyo.

Alisema nchi ilikuwa inatumia gharama kubwa sana za matumizi kusafirisha wagonjwa kuwapeleka nje ya nchi kwa ajili ya upasuaji wa moyo.

Hivyo hatua hiyo ni chachu ya matumaini na inawapeleka wataalamu 26 kutoka nchini kwenda India kupata mafunzoya upasuaji, wakiwemo madaktari bingwa wa upasuaji wa moyo wanne na madaktari wa moyo sita.

MWaka huu ilidaiwa kulikuwa na wagonjwa wapato 200 wa maradhi ya moyo na kati yao walioweza kubahatika kupelekwa nje ni 60 na wengine bado hawajapelekwa kutokana na gharama kuwa kubwa kuwatibu wagonjwa hao.

Hivyo kituo hicho kitaleta faraja ya nchi na Tanzania ditakuwea miongoni mwa nchi zitkazoweza kutibu magonjwa hayo.

No comments:

Post a Comment