KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Friday, May 28, 2010

Waasi wajinufaisha na madini DRC


Ripoti iliyotolewa na baraza la usalama la Umoja wa Mataifa imesema makundi ya waasi mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo yanaendelea kukusanya ushuru kinyume cha sheria kutoka kwa watu wanaohudumu katika kiwanda cha kuchimba madini ya dhahabu.

Ripoti hiyo pia imewasilisha ushahidi kuthibitisha kuwa waasi hao wanatumia stakabadhi gushi za Umoja huo ili kuyauza madini hayo katika mataifa jirani.

Waasi wa CNDP vile vile wametuhumiwa kuweka vituo vya ukaguzi na kuwatoza wenye magari na raia kodi kinyume cha sheria.

Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo ina mali asili za madini nyingi lakini makundi ya waasi wenye silaha wanadhibiti biashara hii.

Makundi haya yanaarifiwa kupata faida kutokana na biashara hii ya mamilioni ya dola kutokana na madini na kudhibiti migodi kwa nguvu na kuomba hongo au kodi.

Mchango wa biashara ya madini umetambulika kuwa moja ya sababu zinazochochea vita na kuchangia ukiukwaji wa haki za binadamu mashariki mwa nchi hii tangu kuanza kwa vita.

No comments:

Post a Comment