KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Monday, May 31, 2010

Ajeruhiwa Akiamulia Ugomvi wa Mume na Mke

MWANAUME mmoja aliyetambulika kwa jina la Samson amejeruhiwa katika sehemu zake za usoni wakati akijaribu kuamulia ugomvi uliokuwa ukiendelea kati ya mume na mkewe ambao ni majirani zake.
Mwanaume huyo amejeruhiwa katika ugomvi uliokuwa ukiendelea kati ya mume na mke katika nyumba waliyokuwa wamepanga huko maeneo ya Yombo jijini Dar es Salaam.

Chanzo chetu cha habari kilidai kuwa, ugomvi kati ya wanandoa hao ulianza majira ya saa 2 za usiku jana ndani ya chumba chao walichopanga katika nyumba hiyo.

Alidai kuwa walianza kusikia mwanaume akiongea kwa jazba akimfokea mke wake kwa chanzo ambacho hawakikufahamu mapema kwa wakati huo.

Alidai kuwa kutokana na hasira alizonazo mume wa dada huyo alianza kumpa kichapo mke wake na mwanamke huyo akisikika kuugulia na kilio cha mbali ili hali watu wasisikie kama alikuwa analia ndani humo.

Kadri dakika zilivyozidi kusogea mwanamke huyo uvumilivu ulimshinda na alianza kusikika akitoa sauti ya kilio kuashiria kibano alichokuwa akikipata kilikuwa kimemkolea.

Ndipo kelele za mwanamke huyo ziliwafanya baadhi ya wasamaria kwenda kugonga mlango wao ili waweze kumsaidia mwanamke huyo.

Mke huyo alijitahidi na aliweza kuufungua mlango na kutoka nje na alipotoka nje mume wake alimkamata na kumrudisha ndani na ndipo wasamaria wakaingia ndani humo kumtaka mume huyo aache kumpiga kwakuwa kwa muda huo ulikuwa ni muda wa watu kupumzika.

Samson aliingia ndani humo kwa lengo la kugombelezea ugomvi huo na mume huyo hakuwa tayari kusikiliza la mtu na ndipo wakati Samson yupo katika pilika pilika ya kumnusuru mwanamke huyo kuepukana na kipigo hicho, mume huyo aliamua kumrushia stuli Samson ambayo ilitua barabara kwenye sehemu zake za uso.

Mume huyo hakutosheka alipasua chupa ya bia na kumpiga nayo Smason usoni na kumjeruhi vibaya.

Kwa kuwa Samson alishajeruhiwa aliamua kujinusuru kwenye ugomvi huo kuachia wengine wakagombelezee na yeye kwenda zahanati ya karibu kwa matibabu.

Chanzo cha ugomvi kwa wanandoa hao hakikufahamika hadi tunaondoka eneo la tukio.

No comments:

Post a Comment