KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Tuesday, April 27, 2010

Noriega asafirishwa hadi Ufaransa


Aliyekuwa kiongozi wa Panama, Manuel Noriega, amesafirishwa hadi Ufaransa, baada ya kufungwa kwa zaidi ya miaka 20 jela nchini Marekani.

Waziri wa mashauri ya nje wa Marekani, Hillary Clinton, alitia saini waranti ya "kusalimu amri", baada ya kutokuwepo tena vipingamizi vya kisheria kumzuia nchini Marekani.

Noriega, pasipo kuwepo mahakamani, alihukumiwa nchini Ufaransa mwaka 1999, kutokana na ulanguzi wa fedha, na kuna uwezekano pia wa kufunguliwa kesi mpya.

Noriega sasa anatazamiwa kufikishwa mbele ya maafisa wa mashtaka, ambao watamjulisha kuhusu waranti iliyotolewa ya kumkamata.

No comments:

Post a Comment